Siku ambayo kila nafsi itakuja jitetea, na kila nafsi italipwa sawa sawa na a'mali ilizo zifanya, nao hawatadhulumiwa.
Ewe Nabii! Watajie watu wako, kwa kuwahadharisha, Siku ambayo kila mtu atakuwa hana linalo mshughulisha ila kujitetea nafsi yake. Hayamshughulishi ya mzazi wala mwana. Siku hiyo ndiyo Siku ya Kiyama! Na Mwenyezi Mungu siku hiyo atailipa kila nafsi malipo ya vitendo iliyo tenda, ikiwa kheri au shari. Na Mola wako Mlezi hamdhulumu hata mtu mmoja.
Na Mwenyezi Mungu amepiga mfano wa mji ulio kuwa na amani na utulivu, riziki yake ikiufikia kwa nafasi kutoka kila mahali. Lakini ukazikufuru neema za Mwenyezi Mungu; kwa hivyo Mwenyezi Mungu akauvika vazi la njaa na khofu kwa sababu ya yale waliyo kuwa wakiyafanya.
Na Mwenyezi Mungu Subhanahu amewapigia mfano watu wa Makka kisa cha mji mmojapo. Watu wake walikuwa wamekaa kwa amani, hawana adui anaye waingilia. Wametua, hawana dhiki ya maisha, riziki inawajia kwa wasaa kutoka kila pahali. Wakazibeua neema za Mwenyezi Mungu, wasimshukuru kwa kumt'ii na kutekeleza amri zake. Mwenyezi Mungu akawapatiliza kwa masaibu yaliyo wazunguka kila upande. Wakaonja uchungu wa njaa na vitisho, baada ya utajiri na amani walio kuwa nayo. Na hayo kwa sababu ya kukakamia kwao katika ukafiri na maasi.
Na alikwisha wajia Mjumbe wa miongoni mwao wenyewe. Lakini wakamkanusha;basi iliwafika adhabu hali ya kuwa wamedhulumu.
Nao alikwisha wajia Mtume kutokana nao wenyewe. Ilikuwa ni waajibu wao wamshukuru Mwenyezi Mungu kwa hayo, lakini walimwambia mwongo, kwa inda na husda tu. Adhabu ikawatwaa nao hali wamo katika udhalimu, na kwa sababu ya hiyo dhulma.
Basi kuleni katika vile alivyo kupeni Mwenyezi Mungu, vilivyo halali na vizuri. Na shukuruni neema za Mwenyezi Mungu, ikiwa kweli mnamuabudu Yeye.
Ikiwa washirikina wanazikufuru neema za Mwenyezi Mungu na wanazigeuza kuwa ni nakama, basi nyinyi Waumini elekeeni kwenye shukra. Na kuleni katika alivyo kuruzukuni Mwenyezi Mungu na akakufanyieni kuwa ni vizuri kwenu, wala msijiharimishie nafsi zenu. Na ishukuruni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo juu yenu kwa kumt'ii Yeye tu peke yake, ikiwa kweli mnamkusudia Yeye tu kwa ibada.
Amekuharimishieni nyamafu tu, na damu, na nyama ya nguruwe,na mnyama aliye chinjwa kwa ajili isiyo kuwa ya Mwenyezi Mungu. Lakini anaye lazimishwa bila ya kuasi, wala kuruka mipaka, basi hakika MwenyeziMungu ni Mwenye kusamehe na Mwenye kurehemu.
Kwani hakika Mwenyezi Mungu hakukuharimishieni isipo kuwa nyamafu, na damu inayo tiririka kutokana na mnyama wakati wa kumchinja, na nyama ya nguruwe, na kilicho chinjwa kwa asiye kuwa Mwenyezi Mungu. Lakini mwenye kulazimishwa na shida ya njaa kula kitu alicho kuharimishieni Mwenyezi Mungu, bila ya kutaka, na wala bila ya kupita hadi ya kiasi cha kuondoa ile dharura, basi hakika Mwenyezi Mungu hayachukulii hayo. Kwani Yeye Subhanahu ni Mwenye kuwasamehe waja wake. Huwasamehe wanapo tumbukia katika makosa wasio endelea nayo. Naye ni Mwenye kuwarehemu kwa vile anawazuia vitu vinavyo wadhuru, na anawaruhusu kwa kuhifadhi uhai wao.
Wala msiseme uwongo, kwa kuropokwa na ndimi zenu: Hichi halali,na hichi haramu - mkimzulia uwongo Mwenyezi Mungu. Hakika wanao mzulia uwongo Mwenyezi Mungu hawatafanikiwa.
Na ilivyo kuwa Mwenyezi Mungu amekwisha kubainishieni kilicho halali na kilicho haramu, basi shikamaneni na hayo aliyo kubainishieni, wala msithubutu kuhalalisha na kuharimisha ovyo kufuata ndimi zenu. Mkawa mnasema: Hichi halali, na hichi haramu. Matokeo ya hizo kauli zenu ni kumzulia uwongo Mwenyezi Mungu, na kumkhusisha na asiyo yasema! Hakika wanao mzulia uwongo Mwenyezi Mungu hawapati kheri wala mafanikio.
Na Mayahudi tuliwaharimishia yale tuliyo kuhadithia zamani.Na Sisi hatukuwadhulumu, bali walikuwa wakijudhulumu wenyewe.
Wala hawakuharimishiwa ila Mayahudi tu vile vitu tulivyo kusimulia, ewe Nabii, kabla ya kuteremka Aya hizi. Na vitu hivyo ni kuwa kila mnyama mwenye makucha, na shahamu za ng'ombe na kondoo, ila ilio beba migongo yao au matumbo, au iliyo changanyika na mifupa. Na Sisi hatukuwadhulumu kwa kuwaharimishia hayo, lakini wamejidhulumu wenyewe kuyasabibisha hayo kwa kupita mipaka na ushari wao, na kuacha kusimama kwenye yalio halali...
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
అన్వేషణ ఫలితాలు:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".