Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Mealler fihristi


Anlam tercümesi Sure: Sûretu'l-Mürselât   Ayet:

Surat Al-Mursalat

وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa upepo unapovuma kwa mfululizo, huu baada ya huu.
Arapça tefsirler:
فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا
Na kwa upepo wenye kuvuma kwa ukali wenye kuangamiza.
Arapça tefsirler:
وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا
Na kwa Malaika waliopewa jukumu la mawingu, wakawa wayapeleka pale anapotaka Mwenyezi Mungu.
Arapça tefsirler:
فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا
Na kwa Malaika wanaoshuka, kutoka kwa Mwenyezi Mungu,
Arapça tefsirler:
فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا
na amri zinazopambanua baina ya haki na batili na halali na haramu.
Arapça tefsirler:
عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا
Na kwa Malaika wanaoupokea wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kuuteremsha kwa Manabii Wake, unaowapa viumbe wake udhuru kutoka kwa Mwenyezi Mungu na pia onyo kutoka Kwake, ili watu wasiwe na hoja.
Arapça tefsirler:
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ
Hakika jambo la Kiyama mnaloahidiwa pamoja na lile la kuhesabiwa na kulipwa ni lenye kuwa hapana shaka.
Arapça tefsirler:
فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ
Basi nyota zitakapofutwa na mwangaza wake ukaondoka,
Arapça tefsirler:
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ
na mbingu zitakapopasuka,
Arapça tefsirler:
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ نُسِفَتۡ
na majabali yatakapopeperuka na kukueanea huku na kule na yakawa ni mapepe yanayorushwa na upepo,
Arapça tefsirler:
وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتۡ
Na Mitume watapowekewa wakati na muda wa baina yao na ummah wao na kusemwe,
Arapça tefsirler:
لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ
«Ni Siku kubwa gani Mitume wameahirishiwa?»
Arapça tefsirler:
لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ
Wameahirishiwa Siku ya hukumu na uamuzi baina ya viumbe.
Arapça tefsirler:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ
Na nilipi lililokujulisha wewe, ewe binadamu, ni siku gani hiyo ya kutolewa uamuzi na ni zipi shida zake na vituko vyake?
Arapça tefsirler:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu makubwa Siku hiyo ni ya wale waliyoikanusha Siku hii iliyoahidiwa.
Arapça tefsirler:
أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ
Kwani hatukuawaangamiza walitangulia kati ya umma waliopita kwa kuwakanusha kwao Mitume, kama vile watu wa Nūḥ, ‘Ād na Thamūd?
Arapça tefsirler:
ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ
Kisha tutawakutanisha na wao wale waliokuja nyuma kati ya wale waliokuwa ni kama wao katika ukanushaji na uasi.
Arapça tefsirler:
كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ
Mfano wa uangamizaji huo mkali ndivyo tutakavyowafanya wahalifu kati ya makafiri wa Makkah, kwa kumkanusha kwao Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Arapça tefsirler:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa kila mwenye kuukanusha upweke wa Mwenyezi Mungu, unabii, kufufuliwa na kuhesabiwa.
Arapça tefsirler:
أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ
Je kwani sisi hatukuwaumba nyinyi, enyi mkusanyiko wa makafiri, kutokana na maji dhaifu yaliyo matwevu nayo ni tone la manii,
Arapça tefsirler:
فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ
tukayaweka maji haya kwenye mahali palipohifadhika, napo ni kizazi cha mwanamke,
Arapça tefsirler:
إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ
mpaka kipindi maalumu kinachojulikana na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka?
Arapça tefsirler:
فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ
Tukaweza kumuumba, kumtia sura na kumtoa. Basi bora wa wenye kuweza ni s isi.
Arapça tefsirler:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kukanusha uweza wetu.
Arapça tefsirler:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا
Je kwani hatukuifanya hii ardhi mnayoishi juu yake
Arapça tefsirler:
أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا
ikusanye juu ya mgongo wake walio hai wasiohesabika, na ndani ya matumbo yake wafu wasiodhibitika, na
Arapça tefsirler:
وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا
tukajaalia iwe na majabali yaliyojikita yaliyo marefu ili isitikisike na nyinyi, na tukawanywesha maji tamu yaliyo mazuri?
Arapça tefsirler:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa waliozikanusha neema hizi.
Arapça tefsirler:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Wataambiwa makafiri Siku ya Kiyama, «Endeni kwenye adhabu ya moto wa Jahanamu mliokuwa mkiukanusha duniani.
Arapça tefsirler:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ
Endeni mjifinike kwenye kivuli cha moshi wa moto wa Jahanamu ambacho hapo panachembuka vipande vitatu.
Arapça tefsirler:
لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ
Kivuli hiko hakimfanyi mtu ahifadhike na joto la Siku hiyo wala hakizuii muwako wa Moto chochote.
Arapça tefsirler:
إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ
Hakika moto wa Jahanamu unarusha macheche makubwa ya moto, kila cheche moja katika hayo ni kama jengo lililoimarishwa katika ukubwa na urefu wa kuenda juu.
Arapça tefsirler:
كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ
Kama kwamba hizo cheche za moto wa Jahanamu zinazopaa juu ni ngamia weusi ambao rangi yao imeingia kwenye umanjano.»
Arapça tefsirler:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali kwa wenye kukanusha mateso yaliyoahidiwa na Mwenyezi Mungu.
Arapça tefsirler:
هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ
Hii ndiyo Siku ya Kiyama ambayo wakanushaji hawatatamka maneno ya kuwanufaisha
Arapça tefsirler:
وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ
wala hawatapewa idhini ya kusema wakatoa nyudhuru, kwa kuwa hawatakuwa na udhuru wowote.
Arapça tefsirler:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali kwa wenye kuikanusha siku hii na yaliyomo ndani yake.
Arapça tefsirler:
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ
Hii ni Siku ambayo Mwenyezi Mungu Atatoa uamuzi baina ya viumbe, na ukweli na ubatilifu utapambanuka. Tutawakusanya nyinyi Siku hiyo, enyi makafiri wa ummah huu, pamoja na makafiri wa mwanzo miongoni mwa ummah waliopita.
Arapça tefsirler:
فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ
Basi mkiwa na hila za kujitoa na adhabu, tumieni hila zenu na mziokoe nafsi zenu na msukosuko wa Mwenyezi Mungu na mateso Yake.
Arapça tefsirler:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya Kiyama.
Arapça tefsirler:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ
Hakika ya wale waliomuogopa Mola wao duniani na wakaiogopa adhabu Yake kwa kufuata amri Zake na kujiepusha na makatazo Yake. Wao Siku ya Kiyama watakuwa kwenye vivuli vya miti vilivyonyoka, na chemchemi za maji zinazotembea,
Arapça tefsirler:
وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ
na matunda mengi yanayopendwa na nafsi zao ambayo wao wanastarehe nayo. Hapo waambiwe,
Arapça tefsirler:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
«Kuleni chakula chenye ladha na mnyweni kinywaji chenye kufurahisha kwa sababu ya matendo mema mliyoyatanguliza duniani.»
Arapça tefsirler:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Sisi, kwa mfano wa malipo hayo makubwa, tutawalipa watu wema katika matendo yao na utiifu wao kwetu.
Arapça tefsirler:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya Malipo na Hesabu, na kuzikanusha sterehe na mateso yaliyomo Siku hiyo.
Arapça tefsirler:
كُلُواْ وَتَمَتَّعُواْ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجۡرِمُونَ
Kisha Mwenyezi Mungu Akawaonya makafiri kwa kusema, «Kuleni aina ya vyakula vya ladha duniani na stareheni kwa matamanio yake yenye kumalizika kwa muda mchache, hakika nyinyi ni wahalifu kwa kumshirikisha kwenu Mwenyezi Mungu.»
Arapça tefsirler:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya kuhesabiwa na kulipwa.
Arapça tefsirler:
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرۡكَعُواْ لَا يَرۡكَعُونَ
Na wanapoambiwa hawa washirikina, «Mswalieni Mwenyezi Mungu na mnyenyekeeni,» hawanyenyekei wala hawaswali, bali wanaendelea kuonyesha kiburi chao.
Arapça tefsirler:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuzikanusha aya za Mwenyezi Mungu.
Arapça tefsirler:
فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ
Iwapo wao hawataiamini hii Qur’ani, basi wataamini kitabu gani na maneno gani baada yake? Na Qur’ani yenyewe ni Kitabu kilichobainisha kila kitu, kilicho wazi katika hekima zake, hukumu zake na habari zake, chenye kushinda katika matamko yake na maana yake.
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Sure: Sûretu'l-Mürselât
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Mealler fihristi

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Kapat