Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Mealler fihristi

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Anlam tercümesi Ayet: (109) Sure: Sûratu Yûsuf
وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ إِلَّا رِجَالٗا نُّوحِيٓ إِلَيۡهِم مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡقُرَىٰٓۗ أَفَلَمۡ يَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَيَنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۗ وَلَدَارُ ٱلۡأٓخِرَةِ خَيۡرٞ لِّلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
Na hatukuwatuma Mitume kabla yako isipo kuwa wanaume tulio wafunulia wahyi miongoni mwa watu wa mijini. Je! Hawatembei katika ardhi wakaona jinsi ulivyo kuwa mwisho wa walio kuwa kabla yao? Na hakika nyumba ya Akhera ni bora kwa wamchao Mungu. Basi hamfahamu?.
Wala Sisi hatukuacha mtindo wetu katika kuwateuwa Mitume tulipo kuteuwa wewe, ewe Nabii! Wala hali ya kaumu yako haikuwa mbali na hali ya kaumu nyengine zilizo tangulia. Kwani hatukuwateuwa Malaika kabla yako, bali tuliwateuwa wanaume wanaadamu katika watu wa mijini, ukawateremkia Ufunuo, yaani Wahyi. Tukawatuma kuwa ni wabashiri na waonyaji. Wenye kuongoka wakawaitikia, na wapotovu wakawafanyia inda! Je, watu wako wameghafilika na kweli hii? Je, wamekalishwa kitako wasiweze kutembea wakaona hao wa kale tulivyo wateketeza duniani? Na mwisho wao ni Motoni; wakaamini wenye kuamini tukawaokoa na tukawanusuru duniani. Na malipo ya Akhera ni bora kwa wenye kumkhofu Mwenyezi Mungu, wasimshirikishe wala wasimuasi. Zimeharibika akili zenu, enyi wakaidi, hata hamwezi kufikiri wala kuzingatia!
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Ayet: (109) Sure: Sûratu Yûsuf
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Mealler fihristi

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Kapat