قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ * - ترجمے کی لسٹ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

معانی کا ترجمہ آیت: (109) سورت: سورۂ یوسف
وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ إِلَّا رِجَالٗا نُّوحِيٓ إِلَيۡهِم مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡقُرَىٰٓۗ أَفَلَمۡ يَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَيَنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۗ وَلَدَارُ ٱلۡأٓخِرَةِ خَيۡرٞ لِّلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
Na hatukuwatuma Mitume kabla yako isipo kuwa wanaume tulio wafunulia wahyi miongoni mwa watu wa mijini. Je! Hawatembei katika ardhi wakaona jinsi ulivyo kuwa mwisho wa walio kuwa kabla yao? Na hakika nyumba ya Akhera ni bora kwa wamchao Mungu. Basi hamfahamu?.
Wala Sisi hatukuacha mtindo wetu katika kuwateuwa Mitume tulipo kuteuwa wewe, ewe Nabii! Wala hali ya kaumu yako haikuwa mbali na hali ya kaumu nyengine zilizo tangulia. Kwani hatukuwateuwa Malaika kabla yako, bali tuliwateuwa wanaume wanaadamu katika watu wa mijini, ukawateremkia Ufunuo, yaani Wahyi. Tukawatuma kuwa ni wabashiri na waonyaji. Wenye kuongoka wakawaitikia, na wapotovu wakawafanyia inda! Je, watu wako wameghafilika na kweli hii? Je, wamekalishwa kitako wasiweze kutembea wakaona hao wa kale tulivyo wateketeza duniani? Na mwisho wao ni Motoni; wakaamini wenye kuamini tukawaokoa na tukawanusuru duniani. Na malipo ya Akhera ni bora kwa wenye kumkhofu Mwenyezi Mungu, wasimshirikishe wala wasimuasi. Zimeharibika akili zenu, enyi wakaidi, hata hamwezi kufikiri wala kuzingatia!
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ آیت: (109) سورت: سورۂ یوسف
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ- ترجمہ علی محسن بروانی نے کیا ہے۔

بند کریں