Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Mealler fihristi

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Anlam tercümesi Ayet: (125) Sure: Sûratu'l-En'âm
فَمَن يُرِدِ ٱللَّهُ أَن يَهۡدِيَهُۥ يَشۡرَحۡ صَدۡرَهُۥ لِلۡإِسۡلَٰمِۖ وَمَن يُرِدۡ أَن يُضِلَّهُۥ يَجۡعَلۡ صَدۡرَهُۥ ضَيِّقًا حَرَجٗا كَأَنَّمَا يَصَّعَّدُ فِي ٱلسَّمَآءِۚ كَذَٰلِكَ يَجۡعَلُ ٱللَّهُ ٱلرِّجۡسَ عَلَى ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ
Basi yule ambaye Mwenyezi Mungu anataka kumhidi humfungulia kifua chake kwa Uislamu. Na anaye taka apotee hukifanya kifua chake kina dhiki, kimebana, kama kwamba anapanda mbinguni. Namna hivi Mwenyezi Mungu anajaalia uchafu juu ya wasio amini.
Ikiwa hao wamepotea, na nyinyi mkaongoka, basi ni kwa kutaka Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwa hukumu yake. Aliye muandikia hidaya humkunjulia kifua chake kwa nuru ya Uislamu. Na aliye muandikia kupotea kifua chake huwa na dhiki ya kweli kweli, kama kinavyo mbana kifua mwenye kupanda pahala pa juu, kama vile mbinguni. Pumzi humpaa, asiweze kitu! Na kwa hivi Mwenyezi Mungu huwaandikia ufisadi na kukatika tamaa hao ambao hawakujaaliwa kuwa na Imani katika shani yao. Masomo ya ilimu za sayansi yamethibitisha kuwa mwanaadamu kila akipanda juu kunadhoofika kuvuta pumzi kwake kwa pua. Mpaka akifika mnyanyuka wa futi 12,000 huwa hawezi kuvuta kwa pua, na huvuta pumzi kwa mdomo. Na hivyo huvuta kwa shida, na akifanya juhudi yoyote ya nguvu huzidi taabu ya kuvuta pumzi. Na hata kusema humletea shida katika pumzi.
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Ayet: (125) Sure: Sûratu'l-En'âm
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Mealler fihristi

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Kapat