Check out the new design

Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - Savahili Dili Tercüme - Rowad Tercüme Merkezi * - Mealler fihristi


Anlam tercümesi Sure: Sûretu'n-Nebe   Ayet:

An-Naba

عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
Wanaulizana kuhusu nini?
Arapça tefsirler:
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلۡعَظِيمِ
Kuhusu Ile habari kuu.
Arapça tefsirler:
ٱلَّذِي هُمۡ فِيهِ مُخۡتَلِفُونَ
Ambayo kwayo wanahitalifiana.
Arapça tefsirler:
كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
La! Karibu watakuja jua.
Arapça tefsirler:
ثُمَّ كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Tena la! Karibu watakuja jua.
Arapça tefsirler:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَٰدٗا
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
Arapça tefsirler:
وَٱلۡجِبَالَ أَوۡتَادٗا
Na milima kama vigingi?
Arapça tefsirler:
وَخَلَقۡنَٰكُمۡ أَزۡوَٰجٗا
Na tukakuumbeni kwa jozi?
Arapça tefsirler:
وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتٗا
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
Arapça tefsirler:
وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسٗا
Na tukaufanya usiku ni nguo?
Arapça tefsirler:
وَجَعَلۡنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشٗا
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
Arapça tefsirler:
وَبَنَيۡنَا فَوۡقَكُمۡ سَبۡعٗا شِدَادٗا
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
Arapça tefsirler:
وَجَعَلۡنَا سِرَاجٗا وَهَّاجٗا
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto.
Arapça tefsirler:
وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡمُعۡصِرَٰتِ مَآءٗ ثَجَّاجٗا
Na tukateremsha maji yanayoanguka kwa kasi kutoka mawinguni.
Arapça tefsirler:
لِّنُخۡرِجَ بِهِۦ حَبّٗا وَنَبَاتٗا
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea.
Arapça tefsirler:
وَجَنَّٰتٍ أَلۡفَافًا
Na mabustani yenye miti iliyokamatana.
Arapça tefsirler:
إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ كَانَ مِيقَٰتٗا
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake.
Arapça tefsirler:
يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِ فَتَأۡتُونَ أَفۡوَاجٗا
Siku litakapopulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi.
Arapça tefsirler:
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٰبٗا
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango.
Arapça tefsirler:
وَسُيِّرَتِ ٱلۡجِبَالُ فَكَانَتۡ سَرَابًا
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
Arapça tefsirler:
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا
Hakika Jahannamu inangojea!
Arapça tefsirler:
لِّلطَّٰغِينَ مَـَٔابٗا
Kwa walioasi ndio makazi yao.
Arapça tefsirler:
لَّٰبِثِينَ فِيهَآ أَحۡقَابٗا
Wakae humo karne baada ya karne.
Arapça tefsirler:
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرۡدٗا وَلَا شَرَابًا
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji.
Arapça tefsirler:
إِلَّا حَمِيمٗا وَغَسَّاقٗا
Ila maji ya moto sana na usaha.
Arapça tefsirler:
جَزَآءٗ وِفَاقًا
Ndio malipo mwafaka.
Arapça tefsirler:
إِنَّهُمۡ كَانُواْ لَا يَرۡجُونَ حِسَابٗا
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hesabu (juu ya matendo yao).
Arapça tefsirler:
وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابٗا
Na wakakanusha Aya zetu kwa nguvu.
Arapça tefsirler:
وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ كِتَٰبٗا
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
Arapça tefsirler:
فَذُوقُواْ فَلَن نَّزِيدَكُمۡ إِلَّا عَذَابًا
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
Arapça tefsirler:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا
Hakika wacha Mungu wanastahiki kufuzu.
Arapça tefsirler:
حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا
Mabustani na mizabibu.
Arapça tefsirler:
وَكَوَاعِبَ أَتۡرَابٗا
Na wake wazuri waliolingana nao.
Arapça tefsirler:
وَكَأۡسٗا دِهَاقٗا
Na bilauri zilizojaa.
Arapça tefsirler:
لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا كِذَّٰبٗا
Hawatasikia humo upuuzi wala uongo.
Arapça tefsirler:
جَزَآءٗ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابٗا
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
Arapça tefsirler:
رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلرَّحۡمَٰنِۖ لَا يَمۡلِكُونَ مِنۡهُ خِطَابٗا
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake, Arrahman (Mwingi wa rehema); hawamiliki usemi mbele yake!
Arapça tefsirler:
يَوۡمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ صَفّٗاۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنۡ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَقَالَ صَوَابٗا
Siku atakaposimama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila yule ambaye Mwingi wa rehema atamruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
Arapça tefsirler:
ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلۡحَقُّۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anayetaka, na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
Arapça tefsirler:
إِنَّآ أَنذَرۡنَٰكُمۡ عَذَابٗا قَرِيبٗا يَوۡمَ يَنظُرُ ٱلۡمَرۡءُ مَا قَدَّمَتۡ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلۡكَافِرُ يَٰلَيۡتَنِي كُنتُ تُرَٰبَۢا
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu ataona yale yaliyotangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningelikuwa udongo!
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Sure: Sûretu'n-Nebe
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - Savahili Dili Tercüme - Rowad Tercüme Merkezi - Mealler fihristi

Rowad Tercüme Merkezi Ekibi tarafından Rabvede'ki Tebliğ, İrşat ve Toplum Bilinçlendirme Derneği ve Dünya dillerinde İslami içerik ve hizmet cemiyeti işbirliğiyle tercüme edilmiştir.

Kapat