قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى


مەنالار تەرجىمىسى سۈرە: سۈرە ئىنپىتار   ئايەت:

Surat Al-Infitar

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ
Pindi mbingu zitakapopasuka na ukaharibika mpango wake.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ
Na pindi nyota zitakapoangukiana.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ
Na pindi Mwenyezi Mungu Atakapozifanya bahari kulipuka na maji yake kutoweka.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ
Na pindi makaburi yatakapogeuzwa kwa kufufuliwa waliokuwamo ndani yake.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ
Wakati huo itajua kila nafsi vitendo vyake vyote ilivyovifanya, vilivyotangulia na vilivyoahirika na italipwa kwa vitendo hivyo.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ
Ewe binadamu unayekanusha kufufuliwa! Ni kipi kilichokufanya uhadaike na ughurike kuhusu Mola wako Mpaji Mwenye kheri nyingi, Anayestahiki kushukuriwa na kutiiwa?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Kwani si Yeye Aliyekuumba, Akalisawazisha umbo lako, Akakuweka katika hali ya sawa na Akakurekibisha ili uweze kutekeleza nyadhifa zako,
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
katika sura yoyote ile Aliyoitaka Akakuumba?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Mambo hayako kama vile mnavyosema kwamba nyinyi mna haki ya kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Hesabu na Malipo.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ
Na mjue kuwa wako na nyinyi Malaika wachunguzi,
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
كِرَامٗا كَٰتِبِينَ
watukufu kwa Mwenyezi Mungu, waandishi wa yale waliyowakilishwa kuyadhibiti. Hakiwapiti, katika vitendo vyenu na siri zenu, chochote.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ
Wanayajua mnayoyafanya, ya kheri au ya shari.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ
Hakika wachamungu wanaotekeleza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa kwenye neema.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ
Hakika watu waovu waliopuuza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa katika Moto mkali.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Ukali wake, Moto huo, utawapata Siku ya Malipo.Na wala wao hawatakuwa ni wenye kughibu,
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ
wakawa hawamo ndani ya Moto wa Jahanamu, si kwa kutoka wala kwa kufa.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Kisha ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ
Siku ya Hesabu, hataweza yoyote kumnufaisha yoyote. Na amri zote Siku Hiyo ni za Mwenyezi Mungu Peke yake Ambaye hakuna mwenye kumshinda, wala hakuna mwenye kumtendesha nguvu, wala hakuna mwenye kushindana na Yeye.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
 
مەنالار تەرجىمىسى سۈرە: سۈرە ئىنپىتار
سۈرە مۇندەرىجىسى بەت نومۇرى
 
قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

تاقاش