Check out the new design

قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ محمد اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ سورت: یوسف   آیت:
فَلَمَّا جَهَّزَهُم بِجَهَازِهِمۡ جَعَلَ ٱلسِّقَايَةَ فِي رَحۡلِ أَخِيهِ ثُمَّ أَذَّنَ مُؤَذِّنٌ أَيَّتُهَا ٱلۡعِيرُ إِنَّكُمۡ لَسَٰرِقُونَ
Na alipowatayarishia Yūsuf na akawabebesha chakula ngamia wao, aliwaamuru watumishi wake wakakiweka kile chombo, ambacho alikua akiwapimia nacho watu, kwenye vyombo vya ndugu yake Binyamin kwa namna ambayo asitambue yoyote. Basi walipopanda kwenda zao, aliita mwenye kuita akisema, «Enyi wenye ngamia waliobebeshwa chakula, nyinyi ni wezi!»
عربی تفاسیر:
قَالُواْ وَأَقۡبَلُواْ عَلَيۡهِم مَّاذَا تَفۡقِدُونَ
Wakasema wana wa Ya’qūb, wakimwelekea yule aliyeita, «Ni kitu gani mnachokikosa?»
عربی تفاسیر:
قَالُواْ نَفۡقِدُ صُوَاعَ ٱلۡمَلِكِ وَلِمَن جَآءَ بِهِۦ حِمۡلُ بَعِيرٖ وَأَنَا۠ بِهِۦ زَعِيمٞ
Yule aliyeita na waliokuwana yeye walisema, «Tumekikosa kipimio ambacho mfalme anapimia nacho. Na zawadi za mwenye kukileta ni twesha ya ngamia mmoja ya chakula.» Na yule aliyeita akasema, «Na mimi naidhamini na kuitolea ahadi hiyo twesha ya ngamia ya chakula.»
عربی تفاسیر:
قَالُواْ تَٱللَّهِ لَقَدۡ عَلِمۡتُم مَّا جِئۡنَا لِنُفۡسِدَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا كُنَّا سَٰرِقِينَ
Ndugu zake Yūsuf wakasema, «Tunaapa kwa Mwenyezi Mungu, nyinyi mna uhakika kwa mliyoyashuhudia kutoka kwetu kwamba sisi hatukuja nchi ya Misri kufanya uharibifu, na si katika sifa zetu kuwa wezi.»
عربی تفاسیر:
قَالُواْ فَمَا جَزَٰٓؤُهُۥٓ إِن كُنتُمۡ كَٰذِبِينَ
Wale waliopewa jokumu la kukitafuta kipimio walisema kuwaambia ndugu zake Yūsuf, «Ni ipi adhabu ya mwizi kwenu nyinyi, iwapo nyinyi ni warongo katika kauli yenu: ‘sisi si wezi’?»
عربی تفاسیر:
قَالُواْ جَزَٰٓؤُهُۥ مَن وُجِدَ فِي رَحۡلِهِۦ فَهُوَ جَزَٰٓؤُهُۥۚ كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلظَّٰلِمِينَ
Ndugu zake Yūsuf wakasema, «Malipo ya mwizi ni kwamba yule ambaye kitapatikana kilichoibiwa kwenye mzigo wa ngamia wake basi yeye ndiye malipo yake.» Yaani atakabidhiwa, kwa sababu ya wizi wake, kwa yule aliyemuibia awe mtumwa kwake.»Malipo mfano huu, nayo ni ya kufanywa mtumwa, tunawalipa wenye kufanya dhuluma kwa kuiba. Hii ndiyo dini yetu na mwendo wetu kuhusu wezi.»
عربی تفاسیر:
فَبَدَأَ بِأَوۡعِيَتِهِمۡ قَبۡلَ وِعَآءِ أَخِيهِ ثُمَّ ٱسۡتَخۡرَجَهَا مِن وِعَآءِ أَخِيهِۚ كَذَٰلِكَ كِدۡنَا لِيُوسُفَۖ مَا كَانَ لِيَأۡخُذَ أَخَاهُ فِي دِينِ ٱلۡمَلِكِ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ نَرۡفَعُ دَرَجَٰتٖ مَّن نَّشَآءُۗ وَفَوۡقَ كُلِّ ذِي عِلۡمٍ عَلِيمٞ
wakarudi na ndugu zake Yūsuf kwake, akasimama mwenyewe kupekua mizigo yao. Akaanza na mizigo yao kabla ya mzigo wa ndugu yake, ili kuimarisha mpango wake wa kumfanya ndugu yake abakie pamoja na yeye, kisha akamalizikia kwenye vyombo vya ndugu yake na akakitoa chombo humo. Hivyo ndivyo tulivyomsahilishia Yūsuf mpango huu ambao ulimpelekea kumchukua ndugu yake kwenye mamlaka ya mfalme wa Misri. Kwani si katika dini yake kummiliki mwizi, isipokuwa kwamba matakwa ya Mwenyezi Mungu yamepelekea mipango hii na kutaka uamuzi kwenye sheria ya ndugu zake Yūsuf yenye hukumu ya mwizi kufanywa mtumwa. Tunawainua daraja tunaowataka ulimwenguni juu ya mwingine kama vile tulivyomuinua Yūsuf daraja. Na juu ya kila mwenye ujuzi kuna mjuzi zaidi kuliko yeye, mpaka ujuzi ukome kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, Mjuzi wa yaliyofichika na yanayoonekana.
عربی تفاسیر:
۞ قَالُوٓاْ إِن يَسۡرِقۡ فَقَدۡ سَرَقَ أَخٞ لَّهُۥ مِن قَبۡلُۚ فَأَسَرَّهَا يُوسُفُ فِي نَفۡسِهِۦ وَلَمۡ يُبۡدِهَا لَهُمۡۚ قَالَ أَنتُمۡ شَرّٞ مَّكَانٗاۖ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا تَصِفُونَ
Wakasema ndugu zake Yūsuf, iwapo huyu yuwaiba, ametangulia ndugu yake kuiba (wakimaanisha Yūsuf, amani imshukiye). Yūsuf akalificha hilo alilosikia la uzushi kutoka kwao ndani ya nafsi yake,na akauzungumzia moyo wake kwa kusema, «Nyinyi ni wabaya zaidi wa mahali kuliko huyo mliyomtaja, mliponifanyia njama zile zilizokua kutoka kwenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi wa sifa za urongo na uzushi mnazozitoa.»
عربی تفاسیر:
قَالُواْ يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡعَزِيزُ إِنَّ لَهُۥٓ أَبٗا شَيۡخٗا كَبِيرٗا فَخُذۡ أَحَدَنَا مَكَانَهُۥٓۖ إِنَّا نَرَىٰكَ مِنَ ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Wakasema kwa njia ya kubembeleza na kutaka kuhurumiwa ili watekeleze ahadi ya baba yao, «Ewe kiongozi, hakika yeye ana mzazi wa kiume mkubwa wa myaka anayempenda na asiyeweza kuwa mbali na yeye. Kwa hivyo mchukue mmoja wetu badala ya Binyamin. Sisi tunakuona ni miongoni mwa watenda wema kwa vile unavotutendea sisi na wasiokuwa sisi.»
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ سورت: یوسف
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ محمد اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے ترجمہ کیا ہے۔

بند کریں