قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ آیت: (141) سورت: سورۂ بقرہ
تِلۡكَ أُمَّةٞ قَدۡ خَلَتۡۖ لَهَا مَا كَسَبَتۡ وَلَكُم مَّا كَسَبۡتُمۡۖ وَلَا تُسۡـَٔلُونَ عَمَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Hao ni ummah waliopita miongoni mwa wale waliowatangulia nyinyi. Wao wana amali zao, na nyinyi muna amali zenu. Wala nyinyi hamtaulizwa kuhusu amali zao. Na wao hawataulizwa kuhusu amali zenu. Katika aya hii pana kukata njia ya kujifungamanisha na viumbe kwa kujiamabatisha nao, kutoghurika kwa kunasibiana na wao, kwa kuwa linalozingatiwa ni kumuamini Mwenyezi Mungu na kumuabudu Peke Yake na kuwafuata Mitume Wake, na kwamba mwenye kumkanusha Mtume yoyote katika wao, huwa amewakanusha Mitume wote.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ آیت: (141) سورت: سورۂ بقرہ
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے کیا ہے۔

بند کریں