قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ آیت: (28) سورت: سورۂ حج
لِّيَشۡهَدُواْ مَنَٰفِعَ لَهُمۡ وَيَذۡكُرُواْ ٱسۡمَ ٱللَّهِ فِيٓ أَيَّامٖ مَّعۡلُومَٰتٍ عَلَىٰ مَا رَزَقَهُم مِّنۢ بَهِيمَةِ ٱلۡأَنۡعَٰمِۖ فَكُلُواْ مِنۡهَا وَأَطۡعِمُواْ ٱلۡبَآئِسَ ٱلۡفَقِيرَ
ili kuyahudhuria yenye kuwafaa ya kusamehewa dhambi zao, kulipwa thawabu za utekelezaji wa ibada yao ya Hija na utiifu wao, kujipatia mapato katika biashara zao na mengine yasiokuwa hayo. Na ili wataje jina la Mwenyezi Mungu kwa kuchinja wanyama ambao kwao wanajisongeza karibu na Mwenyezi Mungu, miongoni mwa ngamia, ng’ombe, mbuzi na kondoo, katika siku maalumu: nazo ni siku ya kumi ya Mfungotatu na siku tatu baada yake, kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema Zake. Na wao wameamrishwa kwa kupendekezewa kula katika vichinjwa hivi na kumlisha kutokana nazo masikini ambaye umasikini wake umembana.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ آیت: (28) سورت: سورۂ حج
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے کیا ہے۔

بند کریں