Check out the new design

قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ محمد اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ سورت: آل عمران   آیت:
فَٱسۡتَجَابَ لَهُمۡ رَبُّهُمۡ أَنِّي لَآ أُضِيعُ عَمَلَ عَٰمِلٖ مِّنكُم مِّن ذَكَرٍ أَوۡ أُنثَىٰۖ بَعۡضُكُم مِّنۢ بَعۡضٖۖ فَٱلَّذِينَ هَاجَرُواْ وَأُخۡرِجُواْ مِن دِيَٰرِهِمۡ وَأُوذُواْ فِي سَبِيلِي وَقَٰتَلُواْ وَقُتِلُواْ لَأُكَفِّرَنَّ عَنۡهُمۡ سَيِّـَٔاتِهِمۡ وَلَأُدۡخِلَنَّهُمۡ جَنَّٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ ثَوَابٗا مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِۚ وَٱللَّهُ عِندَهُۥ حُسۡنُ ٱلثَّوَابِ
Na Mwenyezi Mungu Akaitikia maombi yao kwamba Yeye Hazipotezi juhudi za yoyote aliyetenda amali njema, awe ni mwanamume au ni mwanamke. Kwani wao, katika undugu wa kidini, kukubaliwa amali zao na kulipwa kwazo, ni sawa. Kwa hivyo, wale waliohama kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, wakatolewa kwenye majumba yao, wakaudhiwa katika kumtii Mola wao na kumuabudu kwao Yeye Peke Yake, wakapigana na wakauawa katikia njia ya Mwenyezi Mungu kwa kulikuza neno Lake, hao Mwenyezi Mungu Atawapa sitara kwa maasia waliyoyafanya kama Alivyowasitiri nayo duniani na Hatawahesabu kwayo. Na atawaingiza, tena Atawaingiza, kwenye mabustani ya Peponi ambayo inapita mito chini ya majumba yake ya fahari na miti yake. Hayo yakiwa ni malipo kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Na kwa Mwenyezi Mungu kuna malipo mazuri.
عربی تفاسیر:
لَا يَغُرَّنَّكَ تَقَلُّبُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ
Usihadaike, ewe Mtume, kwa yale waliyonayo wenye kumkufuru Mwenyezi Mungu, ya ukunjufu wa riziki, hali nzuri ya maisha na kuhama kwao kutoka mahali kwenda pengine kwa ajili ya biashara na kutaka faida na mali. Kwa muda mchache, yote hayo yatawaondokea na watakuwa ni wenye kufungika na kuwekwa dhamana kwa vitendo vyao viovu.
عربی تفاسیر:
مَتَٰعٞ قَلِيلٞ ثُمَّ مَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ
Hiyo ni starahe ndogo yenye kuondoka.Kisha marejeo yao Siku ya Kiyama ni Motoni. Na huo Moto ni tandiko ovu mno.
عربی تفاسیر:
لَٰكِنِ ٱلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ رَبَّهُمۡ لَهُمۡ جَنَّٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَا نُزُلٗا مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِۗ وَمَا عِندَ ٱللَّهِ خَيۡرٞ لِّلۡأَبۡرَارِ
Lakini wale waliomuogopa Mola wao , wakazifuata amri Zake na wakajiepusha na makatazo Yake, Mwenyezi Mungu Amewaandalia mabustani ya Pepo ambayo mito inapita chini ya majumba yake ya fahari na miti yake. Mabustani hayo yatakuwa ni makazi yao ya kudumu; hawatatoka humo. Na yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu ni makubwa zaidi na bora zaidi kwa watiifu kuliko yale ya starehe za ulimwengu ambazo hao waliokufuru wanatanga huku na kule kwa kuzitafuta.
عربی تفاسیر:
وَإِنَّ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ لَمَن يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكُمۡ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِمۡ خَٰشِعِينَ لِلَّهِ لَا يَشۡتَرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ ثَمَنٗا قَلِيلًاۚ أُوْلَٰٓئِكَ لَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ
Baadhi ya waliopewa vitabu wanamuamini Mwenyezi Mungu kuwa ni Mola Mmoja na Mungu Mwenye kuabudiwa, wanaiamini Qur’ani mliyoteremshiwa nyinyi na Taurati na Injili walizoteremshiwa wao, hali ya kumdhalilikia Mwenyezi Mungu na kumnyenyekea. Hawazibadilishi aya za Mwenyezi Mungu kwa thamani ndogo ya takataka za duniani wala hawayafichi Aliyoyataremsha Mwenyezi Mungu na wala hawayapotoshi kama wanavyofanya wengineo miongoni mwa waliopewa Vitabu. Hao watapata thawabu kubwa mbele ya Mola wao Siku ya kukutana Naye, na watapewa malipo yao kamili, bila ya kupunguzwa. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhesabu. Hakumshindi Yeye kuyadhibiti matendo yao na kuwahesabu wao kwayo.
عربی تفاسیر:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱصۡبِرُواْ وَصَابِرُواْ وَرَابِطُواْ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ لَعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata sheria Zake kivitendo, kuweni na subira juu ya kumtii Mola wenu na juu yaliyowashukia ya madhara na shida, na washindeni maadui zenu katika kusubiri wasipate kuwa wasubirifu zaidi kuliko nyinyi, na simameni wima katika kumpiga vita adui yangu na adui yenu. Na muogopeni Mwenyezi Mungu, katika hali zenu zote, ili mfaulu kupata radhi Zake ulimwenguni na Akhera.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ سورت: آل عمران
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ محمد اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے ترجمہ کیا ہے۔

بند کریں