قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ آیت: (93) سورت: سورۂ آل عمران
۞ كُلُّ ٱلطَّعَامِ كَانَ حِلّٗا لِّبَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ إِلَّا مَا حَرَّمَ إِسۡرَٰٓءِيلُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ مِن قَبۡلِ أَن تُنَزَّلَ ٱلتَّوۡرَىٰةُۚ قُلۡ فَأۡتُواْ بِٱلتَّوۡرَىٰةِ فَٱتۡلُوهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Vyakula vyote vizuri vilikuwa ni halali kwa wana wa Ya'qūb, amani imshukiye, isipokuwa vile ambavyo Ya’qūb alijiharamishia yeye mwenyewe kwa sababu ya ugonjwa uliompata. Na hayo yalikuwa kabla ya Taurati haijateremshwa. Taurati ilipoteremshwa, Mwenyezi Mungu Aliwaharamishia Wana wa Isrāīl baadhi ya vyakula vilivyokuwa halali kwao. Na hilo ni kwa sababu ya dhuluma zao na uovu wao. Waambie, ewe Mtume, «Ileteni Taurati na muyasome yaliyomo ndani yake iwapo muna hakika ya madai yenu kwamba Mwenyezi Mungu ameteremsha humo uharamu wa aliojiharamishia Ya'qūb nafsi yake, ili mpate kuujua ukweli wa yale yaliyokuja katika Qur’ani ya kwamba Mwenyezi Mungu Hakuwaharamishia Wana wa Isrāīl chochote kabla ya kuteremka Taurati, isipokuwa yale ambayo Ya'qūb alijiharamishia nafsi yake.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ آیت: (93) سورت: سورۂ آل عمران
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے کیا ہے۔

بند کریں