Check out the new design

قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ محمد اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ سورت: یٰس   آیت:
وَءَايَةٞ لَّهُمۡ أَنَّا حَمَلۡنَا ذُرِّيَّتَهُمۡ فِي ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ
Na ushahidi na hoja kwao kwamba Mwenyezi Mungu Peke Yake Ndiye Mstahiki wa kuabudiwa, Ndiye mneemeshaji neema nyingi, ni kwamba sisi tuliwabeba wale waliookoka miongoni mwa wanadamu katika jahazi la Nūḥ lililojazwa jinsi mbalimbali ya viumbe, ili maisha yaendelee baada ya mafuriko.
عربی تفاسیر:
وَخَلَقۡنَا لَهُم مِّن مِّثۡلِهِۦ مَا يَرۡكَبُونَ
Na tukawaumbia hawa washirikina na wasiokuwa wao kama vile jahazi la Nūḥ, miongoni mwa majahazi na vipando vingine wanavyovipanda vikawapeleka kwenye nchi zao.
عربی تفاسیر:
وَإِن نَّشَأۡ نُغۡرِقۡهُمۡ فَلَا صَرِيخَ لَهُمۡ وَلَا هُمۡ يُنقَذُونَ
Na tukitaka tutawazamisha , w'asipate mwenye kuwasaidia wasizame, na wala wao si wenye kuokolewa na kuzama.
عربی تفاسیر:
إِلَّا رَحۡمَةٗ مِّنَّا وَمَتَٰعًا إِلَىٰ حِينٖ
Isipokuwa tuwahurumie, tuwaokoe na tuwastareheshe mpaka muda ukome, huenda wao wakarejea na wakayarakebisha yale waliyoyafanyia kasoro.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱتَّقُواْ مَا بَيۡنَ أَيۡدِيكُمۡ وَمَا خَلۡفَكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Na washirikina wanapoambiwa, «Jihadharini na jambo la Akhera na vituko vyake, hali za dunia na mateso yake, kwa kutarajia rehema ya Mwenyezi Mungu kwenu,» wanapuuza na hawalikubali hilo.
عربی تفاسیر:
وَمَا تَأۡتِيهِم مِّنۡ ءَايَةٖ مِّنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِمۡ إِلَّا كَانُواْ عَنۡهَا مُعۡرِضِينَ
Na huwajii, hawa washirikina, na alama yoyote iliyo wazi kutoka kwa Mola wao, ili uwaongoze kwenye haki na uwabainishie ukweli wa Mtume, isipokuwa wanaipa mgongo na wasinufaike nayo.
عربی تفاسیر:
وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ أَنفِقُواْ مِمَّا رَزَقَكُمُ ٱللَّهُ قَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لِلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَنُطۡعِمُ مَن لَّوۡ يَشَآءُ ٱللَّهُ أَطۡعَمَهُۥٓ إِنۡ أَنتُمۡ إِلَّا فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ
Na waambiwapo makafiri, «Toeni ile riziki ambayo Mwenyezi Mungu Amewaneemesha nayo,» wanasema kuwaambia Waumini, wakijenga hoja, «Je, tumpe chakula yule ambaye lau Mwenyezi Mungu Alitaka Angalimpa chakula? Hamkuwa nyinyi, Waumini, isipokuwa mko mbali waziwazi na haki, kwa kutuamrisha sisi hilo.»
عربی تفاسیر:
وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَٰذَا ٱلۡوَعۡدُ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Na wanasema hawa makafiri kwa njia ya kukanusha na kuwa na haraka, «HukuKufufuliwa kutakuwa lini, iwapo nyinyi ni wakweli katika hilo mnalolisema?»
عربی تفاسیر:
مَا يَنظُرُونَ إِلَّا صَيۡحَةٗ وَٰحِدَةٗ تَأۡخُذُهُمۡ وَهُمۡ يَخِصِّمُونَ
Hawangojei hawa washirikina wanaolifanyia haraka agizo la Mwenyezi Mungu kwao, isipokuwa mvuvio wa fazaa wakati Kiyama kitakaposimama, kitawachukua ghafla, na hali wao wanagombana katika mambo ya maisha yao.
عربی تفاسیر:
فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ تَوۡصِيَةٗ وَلَآ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِمۡ يَرۡجِعُونَ
Hawataweza hawa washirikina wakati wa kuvuviwa barugumu kumuusia yoyote kitu chochote, wala hawataweza kurejea kwa watu wao, bali watakufa wakiwa kwenye masoko yao na pale walipo.
عربی تفاسیر:
وَنُفِخَ فِي ٱلصُّورِ فَإِذَا هُم مِّنَ ٱلۡأَجۡدَاثِ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ يَنسِلُونَ
Na kutavuviwa kwenye barugumu mvuvio wa pili, hapo roho zao zirudishwe kwenye miili yao, wakitahamaki wanatoka makaburini mwao wakielekea kwa Mola wao kwa haraka.
عربی تفاسیر:
قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَا مَنۢ بَعَثَنَا مِن مَّرۡقَدِنَاۜۗ هَٰذَا مَا وَعَدَ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَصَدَقَ ٱلۡمُرۡسَلُونَ
Hapo watasema wenye kukanusha Ufufuzi hali ya kujua, «Ewe maangamivu yetu! Ni nani aliyetutoa makaburini mwetu?» Hapo wajibiwe na waambiwe, «Hili ndilo lile Aliloahidi Mwingi wa rehema na wakalitolea habari Mitume walio wakweli.»
عربی تفاسیر:
إِن كَانَتۡ إِلَّا صَيۡحَةٗ وَٰحِدَةٗ فَإِذَا هُمۡ جَمِيعٞ لَّدَيۡنَا مُحۡضَرُونَ
Hakutakuwa kufufuliwa huku isipokuwa ni matokeo ya mvuvio mmoja katika barugumu, punde si punde viumbe wote watasimama watakuwa wamesimama mbele yetu wapate kuhesabiwa na kulipwa.
عربی تفاسیر:
فَٱلۡيَوۡمَ لَا تُظۡلَمُ نَفۡسٞ شَيۡـٔٗا وَلَا تُجۡزَوۡنَ إِلَّا مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Katika Siku hiyo hesabu itakamilishwa kwa uadilifu. Hakuna nafsi itakayodhulumiwa kitu chochote, kwa kupunguzwa mema yake au kuongezwa maovu yake. Na hamtalipwa isipokuwa kwa yale mliokuwa mkiyafanya ulimwenguni.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ سورت: یٰس
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ محمد اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے ترجمہ کیا ہے۔

بند کریں