قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس * - ترجمے کی لسٹ


معانی کا ترجمہ آیت: (10) سورت: سورۂ احقاف
قُلۡ أَرَءَيۡتُمۡ إِن كَانَ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِ وَكَفَرۡتُم بِهِۦ وَشَهِدَ شَاهِدٞ مِّنۢ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ عَلَىٰ مِثۡلِهِۦ فَـَٔامَنَ وَٱسۡتَكۡبَرۡتُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Sema , ewe Mtume, uwaambie washirikina wa watu wako, “Nipasheni habari: ikiwa hii Qur’ani inatoka kwa Mwenyezi Mungu na mkaikanusha, na hali ameshuhudia shahidi kati ya Wana wa Isrāīl, kama ‘Abdullāh bin Salām, kwa mfano wa hii Qur’ani, nayo ni yaliyomo ndani ya Taurati ya kusadikisha unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, akaiamini na akayafuata kivitendo yaliyokuja ndani ya Qur’ani, na nyinyi mkakanusha hilo kwa njia ya kiburi. Basi ni upi huu isipokuwa ni udhalimu mkubwa na ukafiri mwingi?” Hakika Mwenyezi Mungu Hawaongozi kwenye Uislamu na kuifikia haki wale watu waliojidhulumu kwa kumkanusha Mwenyezi Mungu.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ آیت: (10) سورت: سورۂ احقاف
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ صامت اور ناصر خمیس - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ ڈاکٹر عبد اللہ محمد ابو بکر اور شیخ ناصر خمیس نے کیا ہے۔

بند کریں