قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ * - ترجمے کی لسٹ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

معانی کا ترجمہ آیت: (81) سورت: سورۂ نحل
وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُم مِّمَّا خَلَقَ ظِلَٰلٗا وَجَعَلَ لَكُم مِّنَ ٱلۡجِبَالِ أَكۡنَٰنٗا وَجَعَلَ لَكُمۡ سَرَٰبِيلَ تَقِيكُمُ ٱلۡحَرَّ وَسَرَٰبِيلَ تَقِيكُم بَأۡسَكُمۡۚ كَذَٰلِكَ يُتِمُّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تُسۡلِمُونَ
Na Mwenyezi Mungu amekufanyieni vivuli katika vitu alivyo viumba,na amekufanyieni maskani milimani, na amekufanyieni nguo za kukingeni na joto, na nguo za kukingeni katika vita vyenu. Ndio hivyo anakutimizieni neema zake ili mpate kut'ii.
Na Mwenyezi Mungu amekuumbieni miti na vitu vyenginevyo vya kukupeni vivuli kukulindeni na taabu ya joto, na amekufanyieni mapango milimani, nanyi mkafanya humo maskani kama nyumba. Pia amekuumbieni nguo za sufi na pamba na kitani na vyenginevyo, ili kukuhifadhini na joto la jua, na nguo za chuma za kukulindeni katika vita na adui zenu. Kama alivyo kujaalieni hayo, basi kadhaalika amekutimizieni neema zake kwa kukupeni Dini iliyo simama sawa, ili mpate kuifuata amri yake, na mumsafie ibada Yeye tu si na mwenginewe.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ آیت: (81) سورت: سورۂ نحل
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ- ترجمہ علی محسن بروانی نے کیا ہے۔

بند کریں