قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ * - ترجمے کی لسٹ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

معانی کا ترجمہ آیت: (8) سورت: سورۂ فاطر
أَفَمَن زُيِّنَ لَهُۥ سُوٓءُ عَمَلِهِۦ فَرَءَاهُ حَسَنٗاۖ فَإِنَّ ٱللَّهَ يُضِلُّ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۖ فَلَا تَذۡهَبۡ نَفۡسُكَ عَلَيۡهِمۡ حَسَرَٰتٍۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمُۢ بِمَا يَصۡنَعُونَ
Je! Yule aliye pambiwa a'mali zake mbaya na akaziona ni njema - basi hakika Mwenyezi Mungu humwacha akapotea amtakaye, na humwongoa amtakaye. Basi nafsi yako isijihiliki kwa kuwasikitikia. Hakika Mwenyezi Mungu anajua wanayo yafanya.
Wamekuwa hawatambui? Je! Yule ambaye Shetani kampambia vitendo vyake viovu na mwenyewe akaona ni vizuri, ni kama aliye hidika kwa uwongofu wa Mwenyezi Mungu na akaliona jema kuwa ni jema, na uovu akauona kuwa ni uovu? Kwani hakika Mwenyezi Mungu humwacha akapotea amtakaye katika wanao khiari njia ya upotovu, wakaiona ndiyo njia ya kuifuata. Na humhidi amtakaye miongoni mwa walio ikhiari njia ya hidaya kuwa ndiyo njia ya kuifuata. Basi usiihiliki nafsi yako kwa kuwasikitikia wapotovu na kuwaonea huruma. Hakika Mwenyezi Mungu anajua uovu wautendao, naye atawalipa kwa hayo.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ آیت: (8) سورت: سورۂ فاطر
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ- ترجمہ علی محسن بروانی نے کیا ہے۔

بند کریں