قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ * - ترجمے کی لسٹ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

معانی کا ترجمہ آیت: (15) سورت: سورۂ شوریٰ
فَلِذَٰلِكَ فَٱدۡعُۖ وَٱسۡتَقِمۡ كَمَآ أُمِرۡتَۖ وَلَا تَتَّبِعۡ أَهۡوَآءَهُمۡۖ وَقُلۡ ءَامَنتُ بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ مِن كِتَٰبٖۖ وَأُمِرۡتُ لِأَعۡدِلَ بَيۡنَكُمُۖ ٱللَّهُ رَبُّنَا وَرَبُّكُمۡۖ لَنَآ أَعۡمَٰلُنَا وَلَكُمۡ أَعۡمَٰلُكُمۡۖ لَا حُجَّةَ بَيۡنَنَا وَبَيۡنَكُمُۖ ٱللَّهُ يَجۡمَعُ بَيۡنَنَاۖ وَإِلَيۡهِ ٱلۡمَصِيرُ
Basi kwa haya waite! Nawe simama sawa sawa kama ulivyo amrishwa, wala usiyafuate matamanio yao. Na sema: Naamini aliyo teremsha Mwenyezi Mungu katika Vitabu. Na nimeamrishwa nifanye uadilifu baina yenu. Mwenyezi Mungu ni Mola wetu Mlezi, na Mola wenu Mlezi. Sisi tuna jukumu kwa vitendo vyetu, na nyinyi mna jukumu kwa vitendo vyenu. Hapana kuhojiana baina yetu na nyinyi. Na Mwenyezi Mungu atatukusanya pamoja, na marejeo ni kwake.
Basi kwa ajili ya umoja wa Dini, na kuondoa mtafaruku ndani yake, waite waishike Dini, na shikilia Wito huo kama alivyo kuamrisha Mwenyezi Mungu, wala usitafute kuyaridhi matamanio ya washirikina. Na sema: Mimi naamini Vitabu vyote alivyo wateremshia Mwenyezi Mungu Mitume wake, na Mwenyezi Mungu ameniamrisha nisimamishe uadilifu baina yenu. Na waambie: Mwenyezi Mungu ndiye Muumba wetu, na ndiye Muumba wenu. Vitendo vyetu ni vyetu sisi, si vyenu. Na vitendo vyenu ni vyenu nyinyi, si vyetu. Hapana la kubishana baina yetu na nyinyi, kwani haki iwazi. Mwenyezi Mungu atatukusanya kwa kutuhukumu kwa uadilifu. Na kwake Yeye peke yake ndio marejeo ya kurejea.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ آیت: (15) سورت: سورۂ شوریٰ
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ- ترجمہ علی محسن بروانی نے کیا ہے۔

بند کریں