قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ * - ترجمے کی لسٹ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

معانی کا ترجمہ آیت: (42) سورت: سورۂ انفال
إِذۡ أَنتُم بِٱلۡعُدۡوَةِ ٱلدُّنۡيَا وَهُم بِٱلۡعُدۡوَةِ ٱلۡقُصۡوَىٰ وَٱلرَّكۡبُ أَسۡفَلَ مِنكُمۡۚ وَلَوۡ تَوَاعَدتُّمۡ لَٱخۡتَلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡمِيعَٰدِ وَلَٰكِن لِّيَقۡضِيَ ٱللَّهُ أَمۡرٗا كَانَ مَفۡعُولٗا لِّيَهۡلِكَ مَنۡ هَلَكَ عَنۢ بَيِّنَةٖ وَيَحۡيَىٰ مَنۡ حَيَّ عَنۢ بَيِّنَةٖۗ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَسَمِيعٌ عَلِيمٌ
Kumbukeni pale mlipo kuwa nyinyi kwenye ng'ambo ya karibu ya bonde, na wao wakawa ng'ambo ya mbali, na msafara ulipo kuwa chini yenu. Na ingeli kuwa mmeagana mngeli khitalifiana katika miadi. Lakini (mkakutana) ili Mwenyezi Mungu atimize jambo lilio kuwa lazima litendeke, kwa sababu aangamie wa kuangamia kwa dalili zilizo dhaahiri, na asalimike wa kusalimika kwa dalili zilizo dhaahiri. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
Na kumbukeni mlipo kuwa bondeni ng'ambo hii ya karibu na Madina, na wao makafiri wako ng'ambo ile ya mbali, na msafara wenye bidhaa mlio kuwa mnautaka uko karibu zaidi nanyi upande wa baharini. Na lau kuwa mmepeana miadi ya kukutana kwa kupigana basi msinge wafikiana hivyo. Lakini Mwenyezi Mungu kapanga mkutane bila ya miadi, na bila ya kutaka wao, ili apate kutekeleza jambo ambalo katika ujuzi wake limekwisha thibiti litokee tu, wala hapana jenginelo. Jambo lenyewe ni kuwa vitokee vita vitavyo pelekea nyinyi mshinde na wao washindwe. Ipate kuondoka shaka - wateketee wa kuteketea kwa hoja wazi ya kuonekana, nako ni kushindwa makafiri juu ya wingi wao; na wahuike Waumini kwa hoja iliyo wazi, nako ni kushinda kulio toka kwa Mwenyezi Mungu kuwapa Waumini wachache. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia na kujua. Haimfichikii kauli wala niya yoyote ya pande zote mbili.
عربی تفاسیر:
 
معانی کا ترجمہ آیت: (42) سورت: سورۂ انفال
سورتوں کی لسٹ صفحہ نمبر
 
قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - علی محسن بروانی نے کیا ہے۔ - ترجمے کی لسٹ

قرآن کریم کے معانی کا سواحلی ترجمہ- ترجمہ علی محسن بروانی نے کیا ہے۔

بند کریں