Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима, таржимонлар: Абдуллоҳ Муҳаммад ва Носир Хумайс * - Таржималар мундарижаси


Маънолар таржимаси Оят: (25) Сура: Нисо сураси
وَمَن لَّمۡ يَسۡتَطِعۡ مِنكُمۡ طَوۡلًا أَن يَنكِحَ ٱلۡمُحۡصَنَٰتِ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ فَمِن مَّا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُم مِّن فَتَيَٰتِكُمُ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِۚ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِإِيمَٰنِكُمۚ بَعۡضُكُم مِّنۢ بَعۡضٖۚ فَٱنكِحُوهُنَّ بِإِذۡنِ أَهۡلِهِنَّ وَءَاتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِ مُحۡصَنَٰتٍ غَيۡرَ مُسَٰفِحَٰتٖ وَلَا مُتَّخِذَٰتِ أَخۡدَانٖۚ فَإِذَآ أُحۡصِنَّ فَإِنۡ أَتَيۡنَ بِفَٰحِشَةٖ فَعَلَيۡهِنَّ نِصۡفُ مَا عَلَى ٱلۡمُحۡصَنَٰتِ مِنَ ٱلۡعَذَابِۚ ذَٰلِكَ لِمَنۡ خَشِيَ ٱلۡعَنَتَ مِنكُمۡۚ وَأَن تَصۡبِرُواْ خَيۡرٞ لَّكُمۡۗ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Na asiyeweza kujimudu mahari ya Waumini waungwana, basi ni hiyari yake aoe wengineo miongoni mwa wanawake wenu waumini waliomilikiwa. Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Ndiye Mjuzi wa ukweli wa Imani yenu. Baadhi yenu mnatokana na wengine katika nyinyi. Basi waoeni kwa ruhusa ya watu wao, na wapeni mahari yao mliokubaliana nayo kwa moyo wenu safi, na wawe ni wenye kujiepusha na haramu, si wenye kudhihirisha zina, wala si wenye kuzini kwa siri kwa kufanya urafiki na wanaume. Wakiolewa na wakafanya kitendo kichafu cha kuzini, adhabu yao ni kadiri ya nusu ya adhabu ya walio huru. Huyo aliyeruhusiwa kuoa wajakazi wenye sifa zilizotajwa, ameruhusiwa iwapo anachelea kuingia kwenye uzinifu na ikawa ni uzito kwake kuvumilia kutoundama. Na kuvumilia kutooa wajakazi pamoja na kujihifadhi ni aula na bora zaidi. Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, ni Mwingi wa msamaha kwenu, ni Mwenye kuwahurumia sana kwa kuwaruhusu muwaoe wao(hao wajakazi) mkishindwa kuwaoa waungwana.
Арабча тафсирлар:
 
Маънолар таржимаси Оят: (25) Сура: Нисо сураси
Суралар мундарижаси Бет рақами
 
Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима, таржимонлар: Абдуллоҳ Муҳаммад ва Носир Хумайс - Таржималар мундарижаси

Қуръон Карим маъноларининг савоҳилийча таржимаси, мутаржимлар: д. Абдуллоҳ Муҳаммад Абу Бакр, Шайх Носир Хумайс

Ёпиш