Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима, таржимонлар: Абдуллоҳ Муҳаммад ва Носир Хумайс * - Таржималар мундарижаси


Маънолар таржимаси Оят: (77) Сура: Нисо сураси
أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ قِيلَ لَهُمۡ كُفُّوٓاْ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَ فَلَمَّا كُتِبَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقِتَالُ إِذَا فَرِيقٞ مِّنۡهُمۡ يَخۡشَوۡنَ ٱلنَّاسَ كَخَشۡيَةِ ٱللَّهِ أَوۡ أَشَدَّ خَشۡيَةٗۚ وَقَالُواْ رَبَّنَا لِمَ كَتَبۡتَ عَلَيۡنَا ٱلۡقِتَالَ لَوۡلَآ أَخَّرۡتَنَآ إِلَىٰٓ أَجَلٖ قَرِيبٖۗ قُلۡ مَتَٰعُ ٱلدُّنۡيَا قَلِيلٞ وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لِّمَنِ ٱتَّقَىٰ وَلَا تُظۡلَمُونَ فَتِيلًا
Kwani hukujua, ewe Mtume, mambo ya wale walioambiwa, kabla ya kuruhusiwa kupigana jihadi, «Izuieni mikono yenu kupigana na maadui wenu washirikina. Na jilazimisheni kutekeleza yale mliyofaradhiwa ya Swala na Zaka»? Na Mwenyezi Mungu Alipowafaradhia kupigana, kulitokea kundi la watu katika wao iliobadilika hali yao wakawa wana kicho cha kuwaogopa watu kama vile wanavyomuogopa Mwenyezi Mungu au zaidi na wakawa wanaidhihirisha hofu kubwa iliyowaingia na kusema, «Ewe Mola wetu, kwa nini ulitufaradhia kupigana? Lau wewe ulitupa muhula mpaka muda mchache.» Wakitumai kupata starehe ya maisha ya ulimwengu. Waambie, ewe Mtume, Starehe ya ulimwengu ni chache, na Akhera na yaliyomo ndani ni makubwa zaidi na ni yenye kusalia zaidi kwa mwenye kuwa na uchamungu, akafanya aliyoamrishwa na akajiepusha na aliyokatazwa. Na Mola wako Hatamdhulumu yoyote, hata kama ni kadiri ya uzi unoakuwako kwenye mwanya wa koko ya tende.
Арабча тафсирлар:
 
Маънолар таржимаси Оят: (77) Сура: Нисо сураси
Суралар мундарижаси Бет рақами
 
Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима, таржимонлар: Абдуллоҳ Муҳаммад ва Носир Хумайс - Таржималар мундарижаси

Қуръон Карим маъноларининг савоҳилийча таржимаси, мутаржимлар: д. Абдуллоҳ Муҳаммад Абу Бакр, Шайх Носир Хумайс

Ёпиш