Check out the new design

Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима * - Таржималар мундарижаси


Маънолар таржимаси Сура: Қамар   Оят:

Qamar

ٱقۡتَرَبَتِ ٱلسَّاعَةُ وَٱنشَقَّ ٱلۡقَمَرُ
Kimekaribia Kiyama na mwezi umepasuka pande mbili, pale makafiri wa Makkah walipomtaka Nabii, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshikie, awaoneshe alama, na yeye akamuomba Mwenyezi Mungu na akawaonesha hiyo alama.
Арабча тафсирлар:
وَإِن يَرَوۡاْ ءَايَةٗ يُعۡرِضُواْ وَيَقُولُواْ سِحۡرٞ مُّسۡتَمِرّٞ
Na washirikina wakiiona dalili na ushahidi juu ya ukweli wa Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, wanakataa kuziamini na kuzisadiki hali ya kukanusha na kupinga, na wanasema baada ya dalili kujitokeza, «Huu ni uchawi wenye ubatilifu na wenye kuondoka na kupotea usiokuwa na sifa ya kudumu.
Арабча тафсирлар:
وَكَذَّبُواْ وَٱتَّبَعُوٓاْ أَهۡوَآءَهُمۡۚ وَكُلُّ أَمۡرٖ مُّسۡتَقِرّٞ
Na walimkanusha Nabii, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, wakafuata upotevu wao na kile cha ukanushaji ambacho matamanio yao yaliwavuta kwacho. Na kila jambo, la kheri au la shari, litawashukia wanaostahili Siku ya Kiyama yatakapodhihiri malipo na mateso.
Арабча тафсирлар:
وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّنَ ٱلۡأَنۢبَآءِ مَا فِيهِ مُزۡدَجَرٌ
Na hakika ziliwajia makafiri wa Kikureshi habari za ummah waliokanusha mitume wao na adhabu iliyowashukia zinazotosha kuwakemea na kuwafanya warudi nyuma waache ukafiri wao na upotevu wao.
Арабча тафсирлар:
حِكۡمَةُۢ بَٰلِغَةٞۖ فَمَا تُغۡنِ ٱلنُّذُرُ
Hii Qur’ani iliowajia ni hekima kubwa iliyofikia upeo. Basi yatawafalia nini maonyo wale watu waliyoipa mgongo na kuikanusha?
Арабча тафсирлар:
فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡۘ يَوۡمَ يَدۡعُ ٱلدَّاعِ إِلَىٰ شَيۡءٖ نُّكُرٍ
Kwa hivyo, wapuuze, ewe Mtume, na uingojee Siku kubwa, Siku Malaika Atakapoita, kwa kuvuvia kwenye baragumu, kwenye jambo linalotisha linalochukiza, nalo ni Kisimamo cha Hesabu.
Арабча тафсирлар:
 
Маънолар таржимаси Сура: Қамар
Суралар мундарижаси Бет рақами
 
Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима - Таржималар мундарижаси

Таржимаси доктор Абдуллоҳ Муҳаммад Абу Бакр ва шайх Носир Хамис.

Ёпиш