Check out the new design

Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима * - Таржималар мундарижаси


Маънолар таржимаси Сура: Тавба   Оят:
قَٰتِلُوهُمۡ يُعَذِّبۡهُمُ ٱللَّهُ بِأَيۡدِيكُمۡ وَيُخۡزِهِمۡ وَيَنصُرۡكُمۡ عَلَيۡهِمۡ وَيَشۡفِ صُدُورَ قَوۡمٖ مُّؤۡمِنِينَ
Enyi mkusanyiko wa Waumini,piganeni vita na maadui wa Mwenyezi Mungu, kwani Aliyetukuka na kushinda Atawaadhibu wao kwa mikono yenu na Atawafanya wanyonge kwa kushindwa na kutwezwa, Atawanusuru juu yao, Ataliinua neno Lake, Atavipoza, kwa kushindwa kwao, vifua vyenu ambavyo kwa muda mrefu viliingiwa na sikitiko na kero kutokana na vitimbi vya washirikina hawa.
Арабча тафсирлар:
وَيُذۡهِبۡ غَيۡظَ قُلُوبِهِمۡۗ وَيَتُوبُ ٱللَّهُ عَلَىٰ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ
Na Ataziondoa hasira kwenye nyoyo za Waumini. Na yoyote mwenye kutubia, miongoni mwa wajeuri hawa, basi Mwenyezi mungu Humkubalia toba amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa ujuzi wa ukweli wa toba ya mwenye kutubia, ni Mwingi wa hekima katika uendeshaji Wake mambo, utengenezaji Wake na sheria Zake Alizowaekea waja Wake.
Арабча тафсирлар:
أَمۡ حَسِبۡتُمۡ أَن تُتۡرَكُواْ وَلَمَّا يَعۡلَمِ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ جَٰهَدُواْ مِنكُمۡ وَلَمۡ يَتَّخِذُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ وَلَا رَسُولِهِۦ وَلَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَلِيجَةٗۚ وَٱللَّهُ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ
Ni katika mipango ya Mwenyezi Mungu kuwajaribu waja Wake. Basi msidhani, enyi mkusanyiko wa Waumini, kwamba MwenyeziMungu Atawaacha bila ya mtihani ili Apate kuwajua, ujuzi uliyofunuka wazi kwa viumbe, waja Wake ambao wamemtakasia Mola wao katika jihadi yao na hawakuwafanya wasiokuwa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na Waumini kuwa ni washauri na marafiki. Na Mwenyezi Mungu ni Mtambuzi wa vitendo vyenu vyote na Atawalipa kwa vitendo hivyo.
Арабча тафсирлар:
مَا كَانَ لِلۡمُشۡرِكِينَ أَن يَعۡمُرُواْ مَسَٰجِدَ ٱللَّهِ شَٰهِدِينَ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِم بِٱلۡكُفۡرِۚ أُوْلَٰٓئِكَ حَبِطَتۡ أَعۡمَٰلُهُمۡ وَفِي ٱلنَّارِ هُمۡ خَٰلِدُونَ
Si katika mambo ya washirikina kuziamirisha Nyumba za Mwenyezi Mungu huku wao wanautangaza ukafiri wao wa kumkanusha Mwenyezi Mungu na wanamfanya kuwa Ana washirika. Washirikina hawa, Siku ya Kiyama, vitendo vyao vyote vitaharibika na mwisho wao ni kukaa milele Motoni.
Арабча тафсирлар:
إِنَّمَا يَعۡمُرُ مَسَٰجِدَ ٱللَّهِ مَنۡ ءَامَنَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَأَقَامَ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتَى ٱلزَّكَوٰةَ وَلَمۡ يَخۡشَ إِلَّا ٱللَّهَۖ فَعَسَىٰٓ أُوْلَٰٓئِكَ أَن يَكُونُواْ مِنَ ٱلۡمُهۡتَدِينَ
Hawawi na hamu ya kujishughulisha na Nyumba za Mwenyezi Mungu na kuziamirisha. isipokuwa wale ambao wanamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, wanasimamisha Swala, wanatoa Zaka na hawaogopi, kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, lawama ya yoyote mwenye kulaumu. Hawa waamirishaji ndio waongofu wa njia ya haki.
Арабча тафсирлар:
۞ أَجَعَلۡتُمۡ سِقَايَةَ ٱلۡحَآجِّ وَعِمَارَةَ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ كَمَنۡ ءَامَنَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَجَٰهَدَ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۚ لَا يَسۡتَوُۥنَ عِندَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Mnayafanya, enyi watu, yale mnayoyasimamia ya kuwanwyesha mahujaji na kuuamirisha msikiti wa Ḥarām ni kama Imani ya aliyemuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na akapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu? Haziwi sawa hali za Waumini na hali za makafiri mbele ya Mwenyezi Mungu, kwani Mwenyezi Mungu halikubali tendo lolote bila ya Imani. Na Mwenyezi Mungu hawaelekezi watu wanaozidhulumu nafsi zao kwa ukafiri kwenye mambo mema.
Арабча тафсирлар:
ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَهَاجَرُواْ وَجَٰهَدُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡ أَعۡظَمُ دَرَجَةً عِندَ ٱللَّهِۚ وَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡفَآئِزُونَ
Wale waliomuamini Mwenyezi Mungu, wakaiacha Nyumba ya ukafiri wakielekea kwenye Nyumba ya Uislamu na wakatoa mali zao na nafsi zao katika jihadi ili kulikuza neno la Mwenyezi Mungu. Hawa wana daraja kubwa mno kwa Mwenyezi Mungu, na wao ndio wenye kufaulu kuzipata radhi Zake.
Арабча тафсирлар:
 
Маънолар таржимаси Сура: Тавба
Суралар мундарижаси Бет рақами
 
Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима - Таржималар мундарижаси

Таржимаси доктор Абдуллоҳ Муҳаммад Абу Бакр ва шайх Носир Хамис.

Ёпиш