Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилийча таржима - Али Муҳсин ал-Бервааний * - Таржималар мундарижаси

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Маънолар таржимаси Оят: (110) Сура: Ҳуд сураси
وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا مُوسَى ٱلۡكِتَٰبَ فَٱخۡتُلِفَ فِيهِۚ وَلَوۡلَا كَلِمَةٞ سَبَقَتۡ مِن رَّبِّكَ لَقُضِيَ بَيۡنَهُمۡۚ وَإِنَّهُمۡ لَفِي شَكّٖ مِّنۡهُ مُرِيبٖ
Na kwa yakini tulimpa Musa Kitabu; zikazuka khitilafu ndani yake. Na lau kuwa si neno lilio kwisha tangulia kutoka kwa Mola wako Mlezi, bila ya shaka ingeli hukumiwa baina yao. Na hakika wao wamo katika shaka juu yake inayo wahangaisha.
Na Sisi tunakuhakikishia, ewe Nabii, kwamba tulimpa Musa Taurati. Na watu wake baada yake wakakhitalifiana katika tafsiri yake na maana yake, kwa kufuata pumbao lao na matamanio yao. Kila mmoja wao anataka kuielekeza ifuate matamanio yake. Wakafarikiana makundi mbali mbali. Wengi wao wakajitenga na Haki iliyo wajia. Na lau kuwa ahadi ya Mwenyezi Mungu haikutangulia kuwa itaakhirishwa adhabu yao mpaka Siku ya Kiyama, ingeli wateremkia katika hii dunia yao hukumu ya Mwenyezi Mungu wakateketezwa wapotovu na wakaokoka walio na haki, kama yalivyo washukia wengineo, walio jiwa na ujumbe wakakhitalifiana katika kuufahamu baadae, na wakaugeuza, hata ikawa ni uzito kuifahamu kweli. Na hawa walio irithi Taurati wanababaika hawaijui kweli iko wapi!
Арабча тафсирлар:
 
Маънолар таржимаси Оят: (110) Сура: Ҳуд сураси
Суралар мундарижаси Бет рақами
 
Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилийча таржима - Али Муҳсин ал-Бервааний - Таржималар мундарижаси

Қуръон Карим маъноларининг савоҳилийча таржимаси, мутаржим: Али Муҳсин ал-Бервааний

Ёпиш