Check out the new design

የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የስዋሂሊ ትርጉም - በዐብደላህ ሙሐመድ ናስር ኸሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ዩሱፍ   አንቀጽ:
قَالَ يَٰبُنَيَّ لَا تَقۡصُصۡ رُءۡيَاكَ عَلَىٰٓ إِخۡوَتِكَ فَيَكِيدُواْ لَكَ كَيۡدًاۖ إِنَّ ٱلشَّيۡطَٰنَ لِلۡإِنسَٰنِ عَدُوّٞ مُّبِينٞ
Ya’qūb, amani imshukiye, alisema kumwambia mwanawe Yūsuf, «Ewe Mwanangu, usiwatajie ndugu zako ndoto hii, watakuhusudu, watakufanyia uadui na watafanya hila za kukuua, hakika Shetani kwa binadamu ni adui ambaye uadui wake uko waziwazi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَكَذَٰلِكَ يَجۡتَبِيكَ رَبُّكَ وَيُعَلِّمُكَ مِن تَأۡوِيلِ ٱلۡأَحَادِيثِ وَيُتِمُّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكَ وَعَلَىٰٓ ءَالِ يَعۡقُوبَ كَمَآ أَتَمَّهَا عَلَىٰٓ أَبَوَيۡكَ مِن قَبۡلُ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡحَٰقَۚ إِنَّ رَبَّكَ عَلِيمٌ حَكِيمٞ
«Na kama kama Alivyokuonesha Mola wako ndoto hii, pia Atakuteua na Atakufundisha uaguzi wa ndoto ambazo watu huziona usingizini, ujue matokeo yake ya uhakika, na atazitimiza neema zake kwako na kwa kizazi cha Ya’qūb, kama alivyozitimiza hapo nyuma kwa wazazi wako wawili, Ibrāhīm na Is’ḥāq, kwa kuwapa unabii na utume. Hakika Mola wako Anamjua yule Anayemteua miongoni mwa waja Wake, ni Mwingi wa hekima katika kuendesha mambo ya viumbe vyake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
۞ لَّقَدۡ كَانَ فِي يُوسُفَ وَإِخۡوَتِهِۦٓ ءَايَٰتٞ لِّلسَّآئِلِينَ
Hakika katika kisa cha Yūsuf na ndugu zake kuna mazingatio na dalili za uweza wa Mwenyezi Mungu na hekima Yake kwa anyeuliza habari zao na akataka kuzijua.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِذۡ قَالُواْ لَيُوسُفُ وَأَخُوهُ أَحَبُّ إِلَىٰٓ أَبِينَا مِنَّا وَنَحۡنُ عُصۡبَةٌ إِنَّ أَبَانَا لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ
Waliposema ndugu zake Yūsuf wa kwa baba kuambiana wao kwa wao, «Hakika Yūsuf na ndugu yake wa kwa baba na mama wanapendwa zaidi na baba yetu kuliko sisi. Anawafanya wao bora juu yetu, na sisi ni kundi lenye idadi kubwa. Hakika baba yetu yuko makosani waziwazi, kwa kuwa amewafanya wao ni bora juu yetu bila ya sababu tunayoiyona yenye kupelekea kufanya hivyo.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ٱقۡتُلُواْ يُوسُفَ أَوِ ٱطۡرَحُوهُ أَرۡضٗا يَخۡلُ لَكُمۡ وَجۡهُ أَبِيكُمۡ وَتَكُونُواْ مِنۢ بَعۡدِهِۦ قَوۡمٗا صَٰلِحِينَ
«Muueni Yūsuf! Au mtupeni kwenye ardhi isiyojulikana iliyo mbali na mji, hapo yatasafika kwenu mapenzi ya baba yenu na muelekeo wake kwenu, na hatageuka kwa wengine na kuacha kushughulika na nyinyi, na mtakuwa, baada ya kumuua Yūsuf au kumuepusha, ni wenye kutubia kwa Mwenyezi Mungu na kumuomba msamaha baada ya kosa lenu.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
قَالَ قَآئِلٞ مِّنۡهُمۡ لَا تَقۡتُلُواْ يُوسُفَ وَأَلۡقُوهُ فِي غَيَٰبَتِ ٱلۡجُبِّ يَلۡتَقِطۡهُ بَعۡضُ ٱلسَّيَّارَةِ إِن كُنتُمۡ فَٰعِلِينَ
Akasema mwenye kusema, miongoni mwa ndugu za Yūsuf, «Msimuue Yūsuf, na mtupeni ndani ya kisima ataokotwa na wapita njia miongoni mwa wasafiri, na hapo mtapumzika na yeye; na hakuna haja ya nyinyi kumuua, iwapo muna azma ya kulifanya hilo mnalolisema.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
قَالُواْ يَٰٓأَبَانَا مَا لَكَ لَا تَأۡمَ۬نَّا عَلَىٰ يُوسُفَ وَإِنَّا لَهُۥ لَنَٰصِحُونَ
wakasema ndugu zake Yūsuf, baada ya kuafikiana kumuepusha, «Ewe baba yetu, unani wewe hutufanyi sisi ni waaminifu juu ya Yūsufu pamoja na kuwa yeye ni ndugu yetu, na sisi tunamtakia wema na kumhurumia, tutamtunza na tutampa ushauri mzuri wa kidhati?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَرۡسِلۡهُ مَعَنَا غَدٗا يَرۡتَعۡ وَيَلۡعَبۡ وَإِنَّا لَهُۥ لَحَٰفِظُونَ
«Tuachie awe na sisi kesho tutakapotoka kwenda kwenye malisho ya wanyama wetu, apate kutembea, apumbae, afurahike na acheze kwa kushindana na mfano wake miongoni mwa machezo yanayofaa. Na sisi ni wenye kumtunza na kila unalomuogopea.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
قَالَ إِنِّي لَيَحۡزُنُنِيٓ أَن تَذۡهَبُواْ بِهِۦ وَأَخَافُ أَن يَأۡكُلَهُ ٱلذِّئۡبُ وَأَنتُمۡ عَنۡهُ غَٰفِلُونَ
Ya’qūb alisema, «Hakika nafsi yangu itaniuma akiepukana na mimi na mkaenda na yeye malishoni. Na mimi nachelea asije akaliwa na mbwamwitu, hali mkiwa kwenye shughuli zenu mumeghafilika na yeye.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
قَالُواْ لَئِنۡ أَكَلَهُ ٱلذِّئۡبُ وَنَحۡنُ عُصۡبَةٌ إِنَّآ إِذٗا لَّخَٰسِرُونَ
Wakasema ndugu zake Yūsuf kumwambia baba yao, «Ikiwa mbwamwitu atamla na hali sisi ni kikundi chenye nguvu, sisi wakati huo tutakuwa ni wenye kupata hasara, hatuna wema wowote, na hakuna manufaa yoyote yanayotarajiwa kutoka kwetu.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ዩሱፍ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የስዋሂሊ ትርጉም - በዐብደላህ ሙሐመድ ናስር ኸሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

ተተርጉሞ በዶ/ር ዐብደሏህ ሙሐመድ አቡበክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ።

መዝጋት