የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም አንቀጽ: (75) ምዕራፍ: ሱረቱ አን-ነሕል
۞ ضَرَبَ ٱللَّهُ مَثَلًا عَبۡدٗا مَّمۡلُوكٗا لَّا يَقۡدِرُ عَلَىٰ شَيۡءٖ وَمَن رَّزَقۡنَٰهُ مِنَّا رِزۡقًا حَسَنٗا فَهُوَ يُنفِقُ مِنۡهُ سِرّٗا وَجَهۡرًاۖ هَلۡ يَسۡتَوُۥنَۚ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِۚ بَلۡ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Na Mwenyezi Mungu Amepiga mfano, Akafafanua kwa mfano huo ubatilifu wa itikadi ya washirikina. Mfano wenyewe ni wa mtu aliyemilikiwa asiyeweza kujipitishia jambo asiyemiliki chochote, na mtu mwingine aliye huru, mwenye mali ya halali ambayo Mwenyezi Mungu Amemruzuku, anayemiliki kupitisha atakalo katika mali hayo, akawa anapeana kwa siri na kwa dhahiri. Je, kuna yoyote mwenye akili atakayesema kwamba watu wawili hawa wako sawa? Hivyo ndivyo Alivyo Mwenyezi Mungu Anayemiliki na Anayepitisha. Yeye Hafanani na viumbe Vyake na watumwa wake. Basi vipi mtasawazisha baina yao? Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Peke Yake. Yeye Ndiye Anayestahiki kushukuriwa na kusifiwa. Lakini wengi wa washirikina hawajui kwamba sifa njema na neema ni za Mwenyezi mungu na kwamba Yeye, Peke Yake, Ndiye Anayestahiki kuabudiwa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም አንቀጽ: (75) ምዕራፍ: ሱረቱ አን-ነሕል
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዶ/ር ሙሐመድ ዓብደሏህ አቡ በክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ

መዝጋት