Check out the new design

የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የስዋሂሊ ትርጉም - በዐብደላህ ሙሐመድ ናስር ኸሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: አስ ሰጅደህ   አንቀጽ:
وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذِ ٱلۡمُجۡرِمُونَ نَاكِسُواْ رُءُوسِهِمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ رَبَّنَآ أَبۡصَرۡنَا وَسَمِعۡنَا فَٱرۡجِعۡنَا نَعۡمَلۡ صَٰلِحًا إِنَّا مُوقِنُونَ
Na lau ungaliona, ewe mhutubiwa, pindi wahalifu waliokanusha kufufuliwa wakiwa wameviinamisha vichwa vyao mbele ya Mola wao kutokana na hizaya na aibu huku wanasema, «Mola wetu! Tumeyaona machafu yetu na tumesikia kutoka kwako ukweli wa yale waliokuwa Mitume wako wakituamrisha duniani, na tumeshatubia kwako, basi turudishe duniani ili tufanye matendo ya utiifu kwako. Sisi tushayaamini sasa yale tuliokuwa tukiyakanusha ya kuwa wewe ni mmoja na kwamba wewe utawafufua walio makaburini. Na lau ungaliyaona, ewe mhutubiwa, haya yote ungaliona jambo kubwa na janga zito.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَلَوۡ شِئۡنَا لَأٓتَيۡنَا كُلَّ نَفۡسٍ هُدَىٰهَا وَلَٰكِنۡ حَقَّ ٱلۡقَوۡلُ مِنِّي لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ أَجۡمَعِينَ
Na lau tungalitaka tungaliwapa washirikina hawa uongofu wao na Angaliwaonyesha njia ya Imani, lakini limethibiti neno linalotoka kwangu na limepasa kwamba nitaujaza, moto wa jahanamu, watu wote wa aina mbili, ya kijini na kibanadamu, wenye kukufuru na kuasi, kwa kuwa walichagua upotevu na kuacha uungofu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَذُوقُواْ بِمَا نَسِيتُمۡ لِقَآءَ يَوۡمِكُمۡ هَٰذَآ إِنَّا نَسِينَٰكُمۡۖ وَذُوقُواْ عَذَابَ ٱلۡخُلۡدِ بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Wataambiwa washirikina hawa kwa njia ya kulaumiwa, watakapoingia Motoni, «Basi onjeni adhabu kwa sababu ya kughafilika kwenu na Akhera na kujiingiza kwenu kwenye ladha za dunia, sisi tutawaacha kwenye adhabu leo, na onjeni adhabu ya moto wa Jahanamu isiyomalizika kwa yale mliokuwa mkiyafanya duniani ya kumkanusha Mwenyezi Mungu na kumuasi.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّمَا يُؤۡمِنُ بِـَٔايَٰتِنَا ٱلَّذِينَ إِذَا ذُكِّرُواْ بِهَا خَرُّواْۤ سُجَّدٗاۤ وَسَبَّحُواْ بِحَمۡدِ رَبِّهِمۡ وَهُمۡ لَا يَسۡتَكۡبِرُونَ۩
Kwa kweli, wanaoziamini aya za Qur’ani na kuzifuata kivitendo ni wale ambao wanapowaidhiwa nazo au wanaposomewa, wanamsujudia Mola wao kwa kumnyenyekea na kumtii na wanamtakasa Mwenyezi Mungu kwa kumsifu katika kusujudu kwao, na hali wao hawaoni kiburi wakaacha kumsujudia na kumtakasa na kumuabudu Yeye Peke Yake Asiyekuwa na mshirika.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
تَتَجَافَىٰ جُنُوبُهُمۡ عَنِ ٱلۡمَضَاجِعِ يَدۡعُونَ رَبَّهُمۡ خَوۡفٗا وَطَمَعٗا وَمِمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡ يُنفِقُونَ
Mbavu za hawa wanaoziamini aya za Mwenyezi Mungu zinajiepusha na magodoro ya kulalia, wakiswali kwa Mola wao swala ya usiku, wakimuomba kwa kuogopa adhabu na kutarajia malipo mema, na katika kile tulichowaruzuku wanatumia katika kumtii Mwenyezi Mungu na katika njia Yake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَلَا تَعۡلَمُ نَفۡسٞ مَّآ أُخۡفِيَ لَهُم مِّن قُرَّةِ أَعۡيُنٖ جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Hakuna nafsi yoyote inayoyajua yale aliyowawekea Mwenyezi Mungu hawa Waumini ya kutuliza macho na kufurahisha moyo, yakiwa ni malipo yao kwa matendo yao mema.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَفَمَن كَانَ مُؤۡمِنٗا كَمَن كَانَ فَاسِقٗاۚ لَّا يَسۡتَوُۥنَ
Je, Yule Aliyekuwa mtiifu kwa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, mwenye kuamini agizo lake la kuwalipa mema wema wenye kufanya mema na kuwalipa ubaya wenye kufanya mabaya, ni kama yule aliyemkanusha Mwenyezi Mungu na Mitume Yake na akaikanusha Siku ya Kiyama? Hawalingani mbele ya Mwenyezi Mungu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَمَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَلَهُمۡ جَنَّٰتُ ٱلۡمَأۡوَىٰ نُزُلَۢا بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Ama wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na wakayafanya yale waliyoamrishwa kwayo, basi malipo yao ni mabustani ya Pepo watashukia huko na watakaa kwenye starehe zake wakiandaliwa, yakiwa malipo yao kwa yale waliokuwa wakiyafanya ulimwenguni ya utiifu Kwake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَأَمَّا ٱلَّذِينَ فَسَقُواْ فَمَأۡوَىٰهُمُ ٱلنَّارُۖ كُلَّمَآ أَرَادُوٓاْ أَن يَخۡرُجُواْ مِنۡهَآ أُعِيدُواْ فِيهَا وَقِيلَ لَهُمۡ ذُوقُواْ عَذَابَ ٱلنَّارِ ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Na ama wale waliotoka nje ya utiifu kwa Mwenyezi Mungu na wakafanya matendo ya kumuasi, basi mahali pao pa kutulia ni moto wa Jahanamu, kila wakitaka kutoka wanarudishwa ndani. Na wataambiwa, kwa kulaumiwa na kukaripiwa, «Onjeni adhabu ya Moto ambayo mlikuwa mkiikanusha ulimwenguni.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: አስ ሰጅደህ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የስዋሂሊ ትርጉም - በዐብደላህ ሙሐመድ ናስር ኸሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

ተተርጉሞ በዶ/ር ዐብደሏህ ሙሐመድ አቡበክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ።

መዝጋት