Check out the new design

የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የስዋሂሊ ትርጉም - በዐብደላህ ሙሐመድ ናስር ኸሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም አንቀጽ: (46) ምዕራፍ: አን-ኒሳዕ
مِّنَ ٱلَّذِينَ هَادُواْ يُحَرِّفُونَ ٱلۡكَلِمَ عَن مَّوَاضِعِهِۦ وَيَقُولُونَ سَمِعۡنَا وَعَصَيۡنَا وَٱسۡمَعۡ غَيۡرَ مُسۡمَعٖ وَرَٰعِنَا لَيَّۢا بِأَلۡسِنَتِهِمۡ وَطَعۡنٗا فِي ٱلدِّينِۚ وَلَوۡ أَنَّهُمۡ قَالُواْ سَمِعۡنَا وَأَطَعۡنَا وَٱسۡمَعۡ وَٱنظُرۡنَا لَكَانَ خَيۡرٗا لَّهُمۡ وَأَقۡوَمَ وَلَٰكِن لَّعَنَهُمُ ٱللَّهُ بِكُفۡرِهِمۡ فَلَا يُؤۡمِنُونَ إِلَّا قَلِيلٗا
Miongoni mwa Mayahudi kuna kundi lililozoea kuyabadilisha maneno ya Mwenyezi Mungu na kuyageuza kinyume cha vile yalivyo kwa kumzulia Mwenyezi Mungu urongo na kusema kumwambia Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, «Tumesikia neno lako na tumeasi amri yako, na sikia kutoka kwetu mwana kutosikia,» na wanasema, «tupe masikizi yako,» yaani, tuelewe na utufahamishe, huku wakizipotoa ndimi zao kwa hilo wakikusudia kumnasibisha na upumbavu, kulingana na lugha yao, na kuitukana dini ya Uislamu. Na lau wao walisema, «Sami'nā wa ata'nā (tumesikia na tumetii),» badala ya kusema «'Aṣaynā» (tumeasi), na walisema «Isma'» (sikia) bila kuongeza «Ghayra musma'» (mwana kutosikia) na walisema, «Unzumā» (tuangalie na utuchunge) badala ya kusema,»Rā'inā», ingalikuwa ni bora kwao mbele ya Mwenyezi Mungu na lingalikuwa ni neno la uadilifu zaidi. Lakini Mwenyezi Mungu Aliwatoa kwenye rehema Yake kwa sababu ya ukafiri wao na kukanusha kwao unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, kwa kuwa hawaamini isipokuwa Imani chache isiyowanufaisha.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም አንቀጽ: (46) ምዕራፍ: አን-ኒሳዕ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የስዋሂሊ ትርጉም - በዐብደላህ ሙሐመድ ናስር ኸሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

ተተርጉሞ በዶ/ር ዐብደሏህ ሙሐመድ አቡበክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ።

መዝጋት