የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - ስዋሂሊኛ ትርጉም - በዓሊይ ሙሕሲን አል-በርዋሊይ * - የትርጉሞች ማዉጫ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አት ተካሱር   አንቀጽ:

Surat At-Takathur

أَلۡهَىٰكُمُ ٱلتَّكَاثُرُ
Kumekushughulisheni kutafuta wingi,
Yamekushughulisheni mkaacha kutimiza yaliyo waajibu na ya ut'iifu kule kujitapa kwenu kwa wana na wafwasi, na kujifakhiri kwa mali, na hisabu, na nasaba, mpaka yakusibuni mauti!
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
حَتَّىٰ زُرۡتُمُ ٱلۡمَقَابِرَ
Mpaka mje makaburini!
Mpaka yakusibuni mauti!
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّا سَوۡفَ تَعۡلَمُونَ
Sivyo hivyo! Mtakuja jua!
Hakika mtakuja jua matokeo ya upumbavu wenu na mapuuza yenu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ كَلَّا سَوۡفَ تَعۡلَمُونَ
Tena sivyo hivyo! Mtakuja jua!
Na hakika bila ya shaka mtakuja jua natija ya hayo!
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّا لَوۡ تَعۡلَمُونَ عِلۡمَ ٱلۡيَقِينِ
Sivyo hivyo! Lau mngeli jua kwa ujuzi wa yakini,
Ama kwa hakika lau mngeli jua kwa yakini uovu wa mwisho wenu bila ya shaka mngeli ogopa huko kushindania kurindika mali, na mngeli jitengenezea Akhera yenu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لَتَرَوُنَّ ٱلۡجَحِيمَ
Basi bila ya shaka mtaiona Jahannamu!
Nakuapieni na nakutilieni mkazo, enyi watu, kwamba hakika nyinyi mtakuja ushuhudia Moto unao waka.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ لَتَرَوُنَّهَا عَيۡنَ ٱلۡيَقِينِ
Tena, bila ya shaka, mtaiona kwa jicho la yakini.
Kisha ninaapa na natilia mkazo kwamba mtauona wazi na kwa yakini.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ لَتُسۡـَٔلُنَّ يَوۡمَئِذٍ عَنِ ٱلنَّعِيمِ
Tena bila ya shaka mtaulizwa siku hiyo juu ya neema.
Tena naapa na natilia mkazo kwamba hakika nyinyi mtahisabiwa kwa neema mlizo deka nazo na mkazistarehea.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አት ተካሱር
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - ስዋሂሊኛ ትርጉም - በዓሊይ ሙሕሲን አል-በርዋሊይ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዓሊይ ሙሕሲን አል-በርዋሊይ

መዝጋት