ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني سورة: التكاثر   آية:

سورة التكاثر - Surat At-Takathur

أَلۡهَىٰكُمُ ٱلتَّكَاثُرُ
Kumekushughulisheni kutafuta wingi,
Yamekushughulisheni mkaacha kutimiza yaliyo waajibu na ya ut'iifu kule kujitapa kwenu kwa wana na wafwasi, na kujifakhiri kwa mali, na hisabu, na nasaba, mpaka yakusibuni mauti!
التفاسير العربية:
حَتَّىٰ زُرۡتُمُ ٱلۡمَقَابِرَ
Mpaka mje makaburini!
Mpaka yakusibuni mauti!
التفاسير العربية:
كَلَّا سَوۡفَ تَعۡلَمُونَ
Sivyo hivyo! Mtakuja jua!
Hakika mtakuja jua matokeo ya upumbavu wenu na mapuuza yenu.
التفاسير العربية:
ثُمَّ كَلَّا سَوۡفَ تَعۡلَمُونَ
Tena sivyo hivyo! Mtakuja jua!
Na hakika bila ya shaka mtakuja jua natija ya hayo!
التفاسير العربية:
كَلَّا لَوۡ تَعۡلَمُونَ عِلۡمَ ٱلۡيَقِينِ
Sivyo hivyo! Lau mngeli jua kwa ujuzi wa yakini,
Ama kwa hakika lau mngeli jua kwa yakini uovu wa mwisho wenu bila ya shaka mngeli ogopa huko kushindania kurindika mali, na mngeli jitengenezea Akhera yenu.
التفاسير العربية:
لَتَرَوُنَّ ٱلۡجَحِيمَ
Basi bila ya shaka mtaiona Jahannamu!
Nakuapieni na nakutilieni mkazo, enyi watu, kwamba hakika nyinyi mtakuja ushuhudia Moto unao waka.
التفاسير العربية:
ثُمَّ لَتَرَوُنَّهَا عَيۡنَ ٱلۡيَقِينِ
Tena, bila ya shaka, mtaiona kwa jicho la yakini.
Kisha ninaapa na natilia mkazo kwamba mtauona wazi na kwa yakini.
التفاسير العربية:
ثُمَّ لَتُسۡـَٔلُنَّ يَوۡمَئِذٍ عَنِ ٱلنَّعِيمِ
Tena bila ya shaka mtaulizwa siku hiyo juu ya neema.
Tena naapa na natilia mkazo kwamba hakika nyinyi mtahisabiwa kwa neema mlizo deka nazo na mkazistarehea.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني سورة: التكاثر
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق