Check out the new design

আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - শ্বাহিলি অনুবাদ- আলী মুহছিন আল-বাৰওৱানী * - অনুবাদসমূহৰ সূচীপত্ৰ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

অৰ্থানুবাদ ছুৰা: আল-ইছৰা   আয়াত:
إِلَّا رَحۡمَةٗ مِّن رَّبِّكَۚ إِنَّ فَضۡلَهُۥ كَانَ عَلَيۡكَ كَبِيرٗا
Isipo kuwa iwe rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika fadhila yake kwako ni kubwa.
Lakini tumeiacha Qur'ani ibaki vile vile kifuani mwako kwa rehema kutoka kwa Mola wako Mlezi, kwani fadhila zake kwako wewe ni kubwa mno katika muujiza huu.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
قُل لَّئِنِ ٱجۡتَمَعَتِ ٱلۡإِنسُ وَٱلۡجِنُّ عَلَىٰٓ أَن يَأۡتُواْ بِمِثۡلِ هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانِ لَا يَأۡتُونَ بِمِثۡلِهِۦ وَلَوۡ كَانَ بَعۡضُهُمۡ لِبَعۡضٖ ظَهِيرٗا
Sema: Wangeli kusanyika watu na majini ili walete mfano wa hii Qur'ani basi hawaleti mfano wake, hata wakisaidiana wao kwa wao.
Waambie, kwa kushindana nao, kama wanaweza walete mfano wake. Nao hawawezi! Hata wakikusanyika watu na majini wakasaidiana kuleta mfano wa hii Qur'ani kwa mpango wake na maana yake, hawawezi; na wanga saidiana wao kwa wao.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَلَقَدۡ صَرَّفۡنَا لِلنَّاسِ فِي هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانِ مِن كُلِّ مَثَلٖ فَأَبَىٰٓ أَكۡثَرُ ٱلنَّاسِ إِلَّا كُفُورٗا
Na hakika tumewaeleza watu katika hii Qur'ani kwa kila mfano. Lakini watu wengi wanakataa isipo kuwa kukanusha tu.
Na katika Qur'ani hii tumewaeleza watu kwa namna mbali mbali kila maana kama ni mifano katika maajabu yake. Lakini watu wengi walikataa ila kupinga na kuchukia.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَقَالُواْ لَن نُّؤۡمِنَ لَكَ حَتَّىٰ تَفۡجُرَ لَنَا مِنَ ٱلۡأَرۡضِ يَنۢبُوعًا
Na walisema: Hatutakuamini mpaka ututimbulie chemchem katika ardhi hii.
Ilipo dhihiri kushindwa kwao na Qur'ani, na wakabanwa kwa hoja, wakataka waletewe ishara nyingine na miujiza mingine. Hicho ni kitendo cha mwenye kushindwa hoja, aliye emewa na kutahayari. Ndio wakasema: Hatutokuamini mpaka ututimbulie katika ardhi ya Makka chemchem ambayo maji yake hayakatiki.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَوۡ تَكُونَ لَكَ جَنَّةٞ مِّن نَّخِيلٖ وَعِنَبٖ فَتُفَجِّرَ ٱلۡأَنۡهَٰرَ خِلَٰلَهَا تَفۡجِيرًا
Au uwe na kitalu cha mitende na mizabibu, na utupitishie mito kati yake ikimiminika.
Au uwe nacho kitalu Makka cha mitende na mizabibu chenye kupita mito kati yake! (Kwa kujua kuwa ardhi ya Makka ni kavu haioti kitu.)
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَوۡ تُسۡقِطَ ٱلسَّمَآءَ كَمَا زَعَمۡتَ عَلَيۡنَا كِسَفًا أَوۡ تَأۡتِيَ بِٱللَّهِ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ قَبِيلًا
Au utuangushie mbingu vipande vipande kama ulivyo dai; au utuletee Mwenyezi Mungu na Malaika uso kwa uso.
Au mbingu ituangukie vichwani mwetu kwa mapande kama ulivyo dai kuwa Mwenyezi Mungu anatuahidi hayo. Au utuletee Mwenyezi Mungu na Malaika tukabiliane nao macho kwa macho!
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَوۡ يَكُونَ لَكَ بَيۡتٞ مِّن زُخۡرُفٍ أَوۡ تَرۡقَىٰ فِي ٱلسَّمَآءِ وَلَن نُّؤۡمِنَ لِرُقِيِّكَ حَتَّىٰ تُنَزِّلَ عَلَيۡنَا كِتَٰبٗا نَّقۡرَؤُهُۥۗ قُلۡ سُبۡحَانَ رَبِّي هَلۡ كُنتُ إِلَّا بَشَرٗا رَّسُولٗا
Au uwe na nyumba ya dhahabu, au upae mbinguni. Wala hatutaamini kupaa kwako mpaka ututeremshie kitabu tukisome. Sema: Subhana Rabbi, Ametakasika Mola wangu Mlezi! Kwani mimi ni nani isipo kuwa ni mwanaadamu na Mtume?
Au uwe na nyumba iliyo pambwa kwa dhahabu, au upae mbinguni. Na hata hivyo hatukusadiki mpaka ukituletea kitabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kinacho thibitisha ukweli wako tukisome! Waambie: Mola wangu Mlezi ametakasika kabisa na kuhukumiwa na yeyote, au yeyote kushirikiana naye katika kudra yake! Mimi si chochote ila ni mwanaadamu kama Mitume wote wengineo. Na wala wao hawakuwaletea watu wao muujiza ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَمَا مَنَعَ ٱلنَّاسَ أَن يُؤۡمِنُوٓاْ إِذۡ جَآءَهُمُ ٱلۡهُدَىٰٓ إِلَّآ أَن قَالُوٓاْ أَبَعَثَ ٱللَّهُ بَشَرٗا رَّسُولٗا
Na nini kilicho wazuilia watu kuamini ulipo wajia uwongofu isipo kuwa walisema: Je! Mwenyezi Mungu humtuma mwanaadamu kuwa ni Mtume?
Na nini kilicho wazuilia washirikina wa Makka kuifuata Haki ulipo wajia wahyi (ufunuo) pamoja na miujiza isipo kuwa madai yao kwa ujinga wao ya kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu hatumi Mitume wanaadamu, ila huwa ni Malaika!
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
قُل لَّوۡ كَانَ فِي ٱلۡأَرۡضِ مَلَٰٓئِكَةٞ يَمۡشُونَ مُطۡمَئِنِّينَ لَنَزَّلۡنَا عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ مَلَكٗا رَّسُولٗا
Sema: Ingeli kuwa duniani wapo Malaika wanatembea kwa utulivu wao, basi bila ya shaka tungeli wateremshia Malaika kuwa ni Mtume wao.
Sema kwa kuwarudi: Lau kuwa duniani badala ya wanaadamu wapo Malaika wanatembea kama wanaadamu na wamekaa humo, basi tungeli wateremshia kutoka mbinguni Malaika kuwa ni Mitume wao katika jinsi yao. Lakini Malaika si kama binaadamu; na wangeli kuja basi wange kuja kwa sura za watu.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
قُلۡ كَفَىٰ بِٱللَّهِ شَهِيدَۢا بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۚ إِنَّهُۥ كَانَ بِعِبَادِهِۦ خَبِيرَۢا بَصِيرٗا
Sema: Mwenyezi Mungu anatosha kuwa Shahidi baina yangu na nyinyi. Hakika Yeye anawajua vyema waja wake na anawaona.
Sema: Kama mnaukataa Utume wangu, basi Mwenyezi Mungu anatosha kuwa ni wa kutuhukumu baina yangu na nyinyi, akathibitisha ukweli wa Ujumbe wangu kwenu. Hakika Yeye kwa waja wake ni Mwenye kujua hali zenu, na Mwenye kuviona vitendo vyenu. Naye ni Mwenye kukulipeni kwa hivyo.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
 
অৰ্থানুবাদ ছুৰা: আল-ইছৰা
ছুৰাৰ তালিকা পৃষ্ঠা নং
 
আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - শ্বাহিলি অনুবাদ- আলী মুহছিন আল-বাৰওৱানী - অনুবাদসমূহৰ সূচীপত্ৰ

অনুবাদ কৰিছে আলী মুহছিন আল-বিৰৱানী চাহাবে।

বন্ধ