Check out the new design

Prijevod značenja časnog Kur'ana - Prijevod na svahili jezik - Abdullah Muhammed i Nasir Hamis * - Sadržaj prijevodā


Prijevod značenja Sura: Hud   Ajet:
قَالَتۡ يَٰوَيۡلَتَىٰٓ ءَأَلِدُ وَأَنَا۠ عَجُوزٞ وَهَٰذَا بَعۡلِي شَيۡخًاۖ إِنَّ هَٰذَا لَشَيۡءٌ عَجِيبٞ
Alipopewa bishara ya Isḥāq, Sārah alisema kwa kustaajabu, «Ee mimi ee! Vipi nitakuwa na mtoto na mimi ni mkongwe na huyu mume wangu yuko katika hali ya uzee na utu uzima? Kuzaa kwa mtu mfano wangu mimi na mfano wa mume wangu pamoja na ukuu wa myaka ni jambo la ajabu.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قَالُوٓاْ أَتَعۡجَبِينَ مِنۡ أَمۡرِ ٱللَّهِۖ رَحۡمَتُ ٱللَّهِ وَبَرَكَٰتُهُۥ عَلَيۡكُمۡ أَهۡلَ ٱلۡبَيۡتِۚ إِنَّهُۥ حَمِيدٞ مَّجِيدٞ
Wajumbe walisema kumwambia , «Hivi wewe unaionea ajabu amri ya Mwenyezi Mungu na hukumu Yake? Rehema ya Mwenyezi Mungu na baraka Zake ziwashukie nyinyi, enyi watu wa nyumba ya unabii. Hakika Yeye, kutakata na kutukuka ni Kwake, ni mhimidiwa wa sifa na vitendo, ni Mwenye utukufu na ukubwa katika hizo.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَلَمَّا ذَهَبَ عَنۡ إِبۡرَٰهِيمَ ٱلرَّوۡعُ وَجَآءَتۡهُ ٱلۡبُشۡرَىٰ يُجَٰدِلُنَا فِي قَوۡمِ لُوطٍ
Ulipomuondokea Ibrāhīm uoga uliompata kwa wale wageni kutokula chakula, na ikamjia bishara njema ya Isḥāq na Ya’qūb, aliendelea kuwajadili Wajumbe wetu juu ya kile tulichowatuma cha kuwaadhibu watu wa Lūṭ na kuwaangamiza.
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنَّ إِبۡرَٰهِيمَ لَحَلِيمٌ أَوَّٰهٞ مُّنِيبٞ
Hakika Ibrāhīm ni mwingi wa uhalimu, hapendi uharakishaji wa adhabu, ni mwingi wa kunyenyekea kwa Mwenyezi Mungu na kumuomba, ni mwenye kutubia, anarejea kwa Mwenyezi Mungu katika mambo yake yote.
Tefsiri na arapskom jeziku:
يَٰٓإِبۡرَٰهِيمُ أَعۡرِضۡ عَنۡ هَٰذَآۖ إِنَّهُۥ قَدۡ جَآءَ أَمۡرُ رَبِّكَۖ وَإِنَّهُمۡ ءَاتِيهِمۡ عَذَابٌ غَيۡرُ مَرۡدُودٖ
Wajumbe wa Mwenyezi Mungu wakasema, «Ewe Ibrāhīm, uacha mjadala huu kuhusu mambo ya watu wa Lūṭ na kuwaombea huruma, kwani hakika ya mambo ni kwamba imithibiti juu yao adhabu na amri ya Mola wako aliyowapangia. Na wao, adhabu inayotoka Mwenyezi Mungu ni yenye kuwashukia, si yenye kuepushwa na wao wala kuzuiliwa..»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَمَّا جَآءَتۡ رُسُلُنَا لُوطٗا سِيٓءَ بِهِمۡ وَضَاقَ بِهِمۡ ذَرۡعٗا وَقَالَ هَٰذَا يَوۡمٌ عَصِيبٞ
Na Malaika wetu walipomjia Lūṭ, aliudhika kwa kuja kwao na akaingiwa na hamu kwa hilo. Hivyo ni kwa kuwa yeye hakuwa anajua kwamba wao ni wajumbe wa Mwenyezi Mungu, akawachelea wasidhuriwe na watu wake na akasema, «Hii ni siku ya mtihani na shida.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَجَآءَهُۥ قَوۡمُهُۥ يُهۡرَعُونَ إِلَيۡهِ وَمِن قَبۡلُ كَانُواْ يَعۡمَلُونَ ٱلسَّيِّـَٔاتِۚ قَالَ يَٰقَوۡمِ هَٰٓؤُلَآءِ بَنَاتِي هُنَّ أَطۡهَرُ لَكُمۡۖ فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلَا تُخۡزُونِ فِي ضَيۡفِيٓۖ أَلَيۡسَ مِنكُمۡ رَجُلٞ رَّشِيدٞ
Watu wa Lūṭ wakamjia kwa haraka kutaka kufanya uchafu, na kabla ya kuja kwao walikuwa wanawendea wanaume kwa njia ya matamanio badala ya wanawake. Lūṭ akasema kuwaambia watu wake, «Hawa ni watoto wangu wa kike, waoeni. Wao niwasafi zaidi kwenu kuliko hayo mnayoyataka.» Aliwaita kuwa ni watoto wake wa kike sababu Nabii wa umma ana daraja ya baba kwao. «Basi muogopeni Mwenyezi Mungu na mjihadhari na mateso Yake, wala msinifedhehi kwa kuwakosea wageni wangu. Kwani hakuna mtu yoyote katika nyinyi aliye mzuri wa kupima mambo apate kuwakataza wanaotaka kufanya machafu akawzuia wao na hayo? Kumdhalilisha mgeni ni jambo la kutukanisha hakuna alifanyalo isipokuwa ni watu wa utwevu.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قَالُواْ لَقَدۡ عَلِمۡتَ مَا لَنَا فِي بَنَاتِكَ مِنۡ حَقّٖ وَإِنَّكَ لَتَعۡلَمُ مَا نُرِيدُ
Wakasema watu wa Lūṭ kumwambia yeye, «Umeshajua tangu mbeleni kwamba sisi hatuna haja ya wanawake wala matamanio. Na wewe unajua tulitakalo. Yaani, sisi hatutaki isipokuwa wanaume na hatuna hamu ya kuoa wanawake.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قَالَ لَوۡ أَنَّ لِي بِكُمۡ قُوَّةً أَوۡ ءَاوِيٓ إِلَىٰ رُكۡنٖ شَدِيدٖ
Walipokataa isipokuwa ni kufanaya machafu, aliwaambia, «Lau mimi nina nguvu kwenu na nina wasaidizi pamoja na mimi, au niutemegee ukoo utakaonihami na nyinyi, ningaliwazuia nyinyi na hayo mnayoyataka.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قَالُواْ يَٰلُوطُ إِنَّا رُسُلُ رَبِّكَ لَن يَصِلُوٓاْ إِلَيۡكَۖ فَأَسۡرِ بِأَهۡلِكَ بِقِطۡعٖ مِّنَ ٱلَّيۡلِ وَلَا يَلۡتَفِتۡ مِنكُمۡ أَحَدٌ إِلَّا ٱمۡرَأَتَكَۖ إِنَّهُۥ مُصِيبُهَا مَآ أَصَابَهُمۡۚ إِنَّ مَوۡعِدَهُمُ ٱلصُّبۡحُۚ أَلَيۡسَ ٱلصُّبۡحُ بِقَرِيبٖ
Malaika wakasema, Ewe Lūṭ, sisi ni wajumbe wa Mola wako, Ametutuma kuwaangamiza watu wako, na wao hawatakufikia. Basi toka kwenye kijiji hiki, wewe na watu wako (waliokuamini), katika kipindi kilichosalia cha usiku, na asizunguke nyuma yoyote katika nyinyi, ili asiione adhabu ikampata. Lakini mke wako aliyeenda kinyume chako kwa kukanusha na kufanya unafiki, kitampata yeye kile kitakachowapata watu wako cha maangamivu. Hakika maagano ya kuangamia kwao ni wakati wa asubuhi, nao ni wakati ambao ni karibu kufika.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Sura: Hud
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - Prijevod na svahili jezik - Abdullah Muhammed i Nasir Hamis - Sadržaj prijevodā

Prevodili su je dr. Abdullah Muhammed Ebu Bekr i šejh Nasir Hamis.

Zatvaranje