Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Sadržaj prijevodā


Prijevod značenja Ajet: (61) Sura: Sura el-Bekara
وَإِذۡ قُلۡتُمۡ يَٰمُوسَىٰ لَن نَّصۡبِرَ عَلَىٰ طَعَامٖ وَٰحِدٖ فَٱدۡعُ لَنَا رَبَّكَ يُخۡرِجۡ لَنَا مِمَّا تُنۢبِتُ ٱلۡأَرۡضُ مِنۢ بَقۡلِهَا وَقِثَّآئِهَا وَفُومِهَا وَعَدَسِهَا وَبَصَلِهَاۖ قَالَ أَتَسۡتَبۡدِلُونَ ٱلَّذِي هُوَ أَدۡنَىٰ بِٱلَّذِي هُوَ خَيۡرٌۚ ٱهۡبِطُواْ مِصۡرٗا فَإِنَّ لَكُم مَّا سَأَلۡتُمۡۗ وَضُرِبَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلذِّلَّةُ وَٱلۡمَسۡكَنَةُ وَبَآءُو بِغَضَبٖ مِّنَ ٱللَّهِۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ كَانُواْ يَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَيَقۡتُلُونَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ بِغَيۡرِ ٱلۡحَقِّۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَواْ وَّكَانُواْ يَعۡتَدُونَ
Na Kumbukeni, tulipowateremshia chakula tamu na ndege wa kuvutia, mkawa hamjali, kama ilivyo desturi yenu, ikawapata dhiki na machovu na mkasema, “Ewe Mūsā! Sisi hatutavumilia chakula hicho kwa hicho kisichobadilika siku zote. Basi tuombee Mola wako Atutolee chakula katika mimea ya ardhini kama mboga, matango, mbegu zinazoliwa, adasi na vitunguu.” Musa akawaambia, kwa kuwapinga vikali, “Vipi mnataka hivyi ambavyo ni duni zaidi na mnaacha riziki yenye manufaa ambayo Mwenyezi Mungu amewachagulia? Ondokeni jangwani na mshuke mjini. Huko mtavipata mnavyovitamani sana kwenye mashamba na masoko.” Waliposhuka, iliwabainikia kuwa wao wanatanguliza chaguo lao,kila mahali, juu ya chaguo la Mwenyezi Mungu na wanayafadhilisha matamanio yao juu ya vitu ambavyo Mwenyezi Mungu Alilowachagulia. Kwa hivyo, sifa ya unyonge na umasikini wa moyo iliwaambata, na wakaondoka na kurudi wakiwa wamo kwenye ghadhabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu, kwa kuipa mgongo dini ya Mwenyezi Mungu, na kwa kuwa wao walikuwa wakikanusha aya za Mwenyezi Mungu na kuua Manabii kwa udhalimu na uadui. Yote hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao na kuivuka mipaka ya Mola wao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Ajet: (61) Sura: Sura el-Bekara
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Zatvaranje