Check out the new design

Prijevod značenja časnog Kur'ana - Prijevod na svahili jezik - Abdullah Muhammed i Nasir Hamis * - Sadržaj prijevodā


Prijevod značenja Sura: El-Enbija   Ajet:
وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِيٓ إِلَيۡهِ أَنَّهُۥ لَآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنَا۠ فَٱعۡبُدُونِ
Na hatukutumiliza kabla yako, ewe Mtume, mjumbe yoyote isipokuwa tunampatia wahyi kwamba hapana mwenye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu. Basi mtakasieni ibada Yeye Peke Yake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَقَالُواْ ٱتَّخَذَ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَلَدٗاۗ سُبۡحَٰنَهُۥۚ بَلۡ عِبَادٞ مُّكۡرَمُونَ
Na washirikina walisema, «Mwenyezi Mungu Amejifanyia mtoto» kwa madai yao kwamba Malaika ni watoto wa kike wa Mwenyezi Mungu. Ametakasika Mwenyezi Mungu na hilo! Malaika ni waja wa Mwenyezi Mungu waliokurubishwa waliohusishwa kwa kupewa matukufu,
Tefsiri na arapskom jeziku:
لَا يَسۡبِقُونَهُۥ بِٱلۡقَوۡلِ وَهُم بِأَمۡرِهِۦ يَعۡمَلُونَ
na wao kwa utiifu wao mzuri hawasemi isipokuwa lile ambalo Mola wao Amewaamrisha kwalo, na hawafanyi tendo lolote mpaka Awaruhusu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
يَعۡلَمُ مَا بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَمَا خَلۡفَهُمۡ وَلَا يَشۡفَعُونَ إِلَّا لِمَنِ ٱرۡتَضَىٰ وَهُم مِّنۡ خَشۡيَتِهِۦ مُشۡفِقُونَ
Na hakuna tendo lolote miongoni mwa matendo ya Malaika, lililopita au linalofuatia, isipokuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Analijua na anawahesabia kwalo. Na hawatangulii kumuombea yoyote isipokuwa yule ambaye Mwenyezi Mungu Ameridhika wamuombee. Na wao kwa kumuogopa Mwenyezi Mungu wana hadhari ya kuenda kinyume na maamrisho Yake na makatazo Yake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ وَمَن يَقُلۡ مِنۡهُمۡ إِنِّيٓ إِلَٰهٞ مِّن دُونِهِۦ فَذَٰلِكَ نَجۡزِيهِ جَهَنَّمَۚ كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلظَّٰلِمِينَ
Na yoyote miongoni mwa Malaika atakayedai kwamba yeye ni mungu pamoja na Mwenyezi Mungu, kwa kukadiria, basi malipo yake ni moto wa Jahanamu. Na mfano wa malipo hayo ndivyo tunavyomlipa kila dhalimu mshirikina.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَوَلَمۡ يَرَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَنَّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ كَانَتَا رَتۡقٗا فَفَتَقۡنَٰهُمَاۖ وَجَعَلۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ كُلَّ شَيۡءٍ حَيٍّۚ أَفَلَا يُؤۡمِنُونَ
Kwani hawakujua hawa ambao wamekufuru kwamba mbingu na ardhi zilikuwa zimeshikana, hakuna kipambanuzi baina yao, hakuna mvua kutoka juu wala mimea kutoka kwenye ardhi, kisha tukazipambanua kwa uweza wetu, tukateremsha mvua kutoka juu na tukatoa mimea kutoka kwenye ardhi na tukajaalia kutokana na maji kila kitu chenye uhai. Basi je hawaamini hawa wakanushaji, wakayasadiki wanayoyaona na wakamuhusuMwenyezi Mungu tu kwa ibada?.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَجَعَلۡنَا فِي ٱلۡأَرۡضِ رَوَٰسِيَ أَن تَمِيدَ بِهِمۡ وَجَعَلۡنَا فِيهَا فِجَاجٗا سُبُلٗا لَّعَلَّهُمۡ يَهۡتَدُونَ
Na tumeumba kwenye ardhi majabali yenye kuituliza isitikisike na tumetoa, kwenye hayo majabali, njia kunjufu, ili viumbe waongoke kwenye njia za kujitafutia maisha yao na kumpwekesha Muumba wao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَجَعَلۡنَا ٱلسَّمَآءَ سَقۡفٗا مَّحۡفُوظٗاۖ وَهُمۡ عَنۡ ءَايَٰتِهَا مُعۡرِضُونَ
Na tumeifanya mbingu ni sakafu ya ardhi, haiinuliwi na nguzo, nayo imetunzwa, haianguki wala haipenywi na mashetani. Na makafiri wameghafilika na kupumbaa kutozizingatia alama za mbnguni (Jua, mwezi na nyota) na kutozifikiria.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلَّيۡلَ وَٱلنَّهَارَ وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَۖ كُلّٞ فِي فَلَكٖ يَسۡبَحُونَ
Na mwenyezi Mungu , Aliyetukuka, Ndiye Aliyeumba usiku ili watu wapate kutulia, na mchana ili wapate kutafuta maisha. Na Ameumba jua, likiwa ni alama ya mchana, na mwezi, ukiwa ni alama ya usiku. Na kila kimojawapo ya hivyo viwili kina njia ya kupitia na kuogelea hakiendi kando nayo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا جَعَلۡنَا لِبَشَرٖ مِّن قَبۡلِكَ ٱلۡخُلۡدَۖ أَفَإِيْن مِّتَّ فَهُمُ ٱلۡخَٰلِدُونَ
Hatukumfanya mwadamu yoyote kabla yako, ewe Mtume, asalie duniani milele. Basi ufapo wewe, kwani wao wana matumaini ya kuishi daima baada yako? Hili haliwi. Katika aya hii pana dalili kwamba Al-Khadhir, amani imshukie, ameshakufa, kwa kuwa yeye ni mwanadamu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
كُلُّ نَفۡسٖ ذَآئِقَةُ ٱلۡمَوۡتِۗ وَنَبۡلُوكُم بِٱلشَّرِّ وَٱلۡخَيۡرِ فِتۡنَةٗۖ وَإِلَيۡنَا تُرۡجَعُونَ
Kila nafsi ni yenye kuonja kifo hapana budi namna utakavyorefuka umri wake duniani. Na kuweko kwake maishani hakukuwa isipokuwa ni mtihani wa majukumu ya maamrisho na makatazo na mabadiliko ya hali, mazuri na mabaya, kisha baada ya hapo kuna kurudi na kurejea kwa Mwenyezi Mungu, Peke Yake, ili kuhesabiwa na kulipwa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Sura: El-Enbija
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - Prijevod na svahili jezik - Abdullah Muhammed i Nasir Hamis - Sadržaj prijevodā

Prevodili su je dr. Abdullah Muhammed Ebu Bekr i šejh Nasir Hamis.

Zatvaranje