Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Sadržaj prijevodā


Prijevod značenja Sura: Sura el-Ankebut   Ajet:

Surat Al-Ankabut

الٓمٓ
«Alif, Lām, Mīm.» Yametangulia maelezo juu ya herufi zilizokatwa na kutengwa mwanzo wa sura ya Al-Baqarah.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَحَسِبَ ٱلنَّاسُ أَن يُتۡرَكُوٓاْ أَن يَقُولُوٓاْ ءَامَنَّا وَهُمۡ لَا يُفۡتَنُونَ
Je wanadhani watu kwamba wakisema «Tumeamini» Mwenyezi Mungu Atawaachilia bila ya kuwajaribu wala kuwatahini?
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَقَدۡ فَتَنَّا ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۖ فَلَيَعۡلَمَنَّ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ صَدَقُواْ وَلَيَعۡلَمَنَّ ٱلۡكَٰذِبِينَ
Kwa hakika, tuliwajaribu wale waliokuwa kabla yao miongoni mwa ummah mbalimbali na tukawatahini kwa Mitume wetu tuliowatumiliza kwao. Basi hakika ni kwamba Mwenyezi Mungu Atawajua, ujuzi wa kujitokeza nje kwa viumbe, ukweli wa wale wakweli katika Imani yao na urongo wa warongo, ili Alipambanue kila kundi na lingine.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَمۡ حَسِبَ ٱلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلسَّيِّـَٔاتِ أَن يَسۡبِقُونَاۚ سَآءَ مَا يَحۡكُمُونَ
Je, kwani wanadhani wale wanaofanya mambo ya uasi, ya ushirikina na mengineyo, kuwa watatushinda wajikwepeshe na sisi tusiwaweze? Ni uamuzi mbaya mno wanaouamua.
Tefsiri na arapskom jeziku:
مَن كَانَ يَرۡجُواْ لِقَآءَ ٱللَّهِ فَإِنَّ أَجَلَ ٱللَّهِ لَأٓتٖۚ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Yoyote mwenye kuwa na matumaini ya kukutana na Mwenyezi Mungu na akawa na matarajio ya kupata malipo Yake mema, basi muda Aliouweka Mwenyezi Mungu wa kuwafufua viumbe Wake ili wahesabiwe na walipwe ni wenye kuja hivi karibuni. Na Yeye Ndiye Msikizi wa maneno, Mjuzi wa vitendo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَن جَٰهَدَ فَإِنَّمَا يُجَٰهِدُ لِنَفۡسِهِۦٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَغَنِيٌّ عَنِ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na mwenye kupigana jihadi katika njia ya kuinua neno la Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na akapigana jihadi na nafsi yake kwa kuisukuma ifanye vitendo vya utiifu, basi anapigana jihadi kwa maslahi ya nafsi yake. Kwa kuwa yeye anafanya hilo kwa kutaka thawabu ya kupigana kwake jihadi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Hana haja ya matendo mema ya waja Wake, kwani mamlaka ni Yake, uumba na mapitisho.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَنُكَفِّرَنَّ عَنۡهُمۡ سَيِّـَٔاتِهِمۡ وَلَنَجۡزِيَنَّهُمۡ أَحۡسَنَ ٱلَّذِي كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Na wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya matendo mema, kwa hakika tutawafutia makosa yao na tutawalipa kwa matendo yao mema, mazuri zaidi ya yale waliokuwa wakiyafanya.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَوَصَّيۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ بِوَٰلِدَيۡهِ حُسۡنٗاۖ وَإِن جَٰهَدَاكَ لِتُشۡرِكَ بِي مَا لَيۡسَ لَكَ بِهِۦ عِلۡمٞ فَلَا تُطِعۡهُمَآۚ إِلَيَّ مَرۡجِعُكُمۡ فَأُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Na tumemsihi binadamu awatendee wema wazazi wake wawili na awe mwema kwao wa maneno na vitendo. Na wakikusukuma kwa bidii, ewe binadamu, umshirikishe mwingine na mimi katika ibada yangu, basi usifuate amri yao. Matakwa ya kuwa Mwenyezi Mungu ashirikishwe yanashikanishwa na matakwa ya kuwa vitendo vingine vya maasia vifanywe. Kwani hakuna kutiiwa kiumbe namna atakavyokuwa katika jambo la kumuasi Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kama lilivyothibiti hilo kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye. Kwangu mimi ndio mwisho wenu, Siku ya Kiyama, na huko niwape habari ya matendo mema na mabaya ambayo mlikuwa mkiyafanya duniani na niwalipe kwa hayo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَنُدۡخِلَنَّهُمۡ فِي ٱلصَّٰلِحِينَ
Na wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wakafanya matendo mema, tutawatia Peponi wakiwa ni katika jumla ya waja wa Mwenyezi Mungu wema.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمِنَ ٱلنَّاسِ مَن يَقُولُ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ فَإِذَآ أُوذِيَ فِي ٱللَّهِ جَعَلَ فِتۡنَةَ ٱلنَّاسِ كَعَذَابِ ٱللَّهِۖ وَلَئِن جَآءَ نَصۡرٞ مِّن رَّبِّكَ لَيَقُولُنَّ إِنَّا كُنَّا مَعَكُمۡۚ أَوَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَعۡلَمَ بِمَا فِي صُدُورِ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na miongoni mwa watu, kuna anayesema, «Tumemuamini Mwenyezi Mungu.» Na afanyiwapo udhia na washirikina huwa akipapatika kutokana na mateso yao na makero yao, kama anavyopapatika kutokana na adhabu ya Mwenyezi Mungu na asivumilie makero yake, akaritadi na akaiacha Imani yake. Na lau waja ushindi kutoka kwa Mola wako, ewe Mtume, kwa watu wenye kumuamini, watasema hawa wenye kuritadi kuiacha Imani yao, «Sisi tulikuwa pamoja na nyinyi, enyi Waumini, tukiwasaidia dhidi ya maadui wenu.» Je, si Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi kuliko yoyote wa kuyajua yaliyomo ndani ya vifua vya viumbe wake wote?
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَيَعۡلَمَنَّ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَلَيَعۡلَمَنَّ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ
Na Atawajua Mwenyezi Mungu, tena atawajua, ujuzi wenye kujitokeza kwa viumbe, wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakazifuata Sheria Zake kivitendo, na Atawajua, tena Atawajua, wanafiki, ili Alipambanue kila kundi na lingine.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لِلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّبِعُواْ سَبِيلَنَا وَلۡنَحۡمِلۡ خَطَٰيَٰكُمۡ وَمَا هُم بِحَٰمِلِينَ مِنۡ خَطَٰيَٰهُم مِّن شَيۡءٍۖ إِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ
Na wanasema wale waliokataa upweke wa Mwenyezi Mungu miongoni mwa Makureshi, na wasiliamini onyo la Mwenyezi Mungu na ahadi Yake, kuwaambia wale waliomuamini Mwenyezi Mungu miongoni mwao na wakafuata Sharia Zake kivitendo, «Iacheni Dini ya Muhammad, na fuateni dini yetu, kwani sisi tutayabeba makosa yenu,» na wao si wenye kubeba chochote katika dhambi zao. Kwa kweli, wao ni warongo kwa yale waliyoyanena.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَيَحۡمِلُنَّ أَثۡقَالَهُمۡ وَأَثۡقَالٗا مَّعَ أَثۡقَالِهِمۡۖ وَلَيُسۡـَٔلُنَّ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ عَمَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ
Na wataibeba, tena wataibeba, washirikina hawa mizigo ya nafsi zao na madhambi yake na mizigo ya wale waliowapoteza na wakawazuia wasiifuate njia ya Mwenyezi Mungu pamoja na mizigo yao wenyewe, bila ya wale waliowafuata nyinyi kupunguziwa mizigo yao kitu chochote. Na wataulizwa, tena wataulizwa, Siku ya Kiyama, kuhusu yale ya urongo waliokuwa wakiyazua.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوۡمِهِۦ فَلَبِثَ فِيهِمۡ أَلۡفَ سَنَةٍ إِلَّا خَمۡسِينَ عَامٗا فَأَخَذَهُمُ ٱلطُّوفَانُ وَهُمۡ ظَٰلِمُونَ
Na hakika tulimtumiliza Nūḥ kwa watu wake, akakaa kwao miaka elfu moja kasoro miaka hamsini, akiwaita kwenye upwekeshaji wa Mwenyezi Mungu na akiwakataza ushirikina, na wao wasimuitikie. Mwenyezi Mungu Akawaangamiza kwa mafuriko, na wao wako katika hali ya kujidhulumu wenyewe kwa ukafiri wao na kupita kiasi kwao katika uasi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَأَنجَيۡنَٰهُ وَأَصۡحَٰبَ ٱلسَّفِينَةِ وَجَعَلۡنَٰهَآ ءَايَةٗ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Hivyo basi tukamuokoa Nūḥ na waliomfuata miongoni mwa wale waliokuwa naye jahazini. Na tukalifanya hilo kuwa ni mazingatio na mawaidha kwa viumbe wote.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِبۡرَٰهِيمَ إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَٱتَّقُوهُۖ ذَٰلِكُمۡ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Mkumbuke na umtaje, ewe Mtume, Ibrāhīm, amani imshukie, alipowalingania watu wake kwamba: mtakasieni Ibada Mwenyezi Mungu Peke Yake, na muogope hasira Zake kwa kutekeleza faradhi Zake na kujiepusha na vitendo vya kumuasi. Hilo ni bora kwenu ikiwa mnakijua kilicho chema kwenu kutokana na kilicho kibaya kwenu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنَّمَا تَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ أَوۡثَٰنٗا وَتَخۡلُقُونَ إِفۡكًاۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ تَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ لَا يَمۡلِكُونَ لَكُمۡ رِزۡقٗا فَٱبۡتَغُواْ عِندَ ٱللَّهِ ٱلرِّزۡقَ وَٱعۡبُدُوهُ وَٱشۡكُرُواْ لَهُۥٓۖ إِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ
Hamuabudu, enyi watu, badala ya Mwenyezi Mungu isipokuwa masanamu na mnazua urongo kwa kuwaita wao waungu. Kwa hakika, hawa masanamu wenu mnaoaowaabudu badala ya Mwenyezi Mungu, hawawezi kuwaruzuku nyinyi kitu chochote, basi tafuteni riziki kwa Mwenyezi Mungu na sio kwa masanamu wenu na mumtakasie ibada na shukrani kwa kuwaruzuku. Ni kwa Mwenyezi Mungu mtarudishwa baada ya kufa kwenu, na hapo awalipe kwa yale ambayo mlifanya.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِن تُكَذِّبُواْ فَقَدۡ كَذَّبَ أُمَمٞ مِّن قَبۡلِكُمۡۖ وَمَا عَلَى ٱلرَّسُولِ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ
Na mkimkanusha, enyi watu, Mtume wetu Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, katika kile alichowalingania mkifuate cha kumuabudu Mwenyezi Mungu Peke Yake, basi kuna makundi ya watu kabla yenu waliowakanusha Mitume wao katika kile walichowaitia, na kwa hivyo zikawashukia hasira za Mwenyezi Mungu. Na Mtume Muhammad hana jukumu lingine isipokuwa ni kuwafikishia nyinyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu ujumbe Wake ufikishaji wenye uwazi, na ashafanya hilo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ كَيۡفَ يُبۡدِئُ ٱللَّهُ ٱلۡخَلۡقَ ثُمَّ يُعِيدُهُۥٓۚ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى ٱللَّهِ يَسِيرٞ
Kwani hawa hawajui ni vipi Mwenyezi Mungu Anaanzisha uumbaji viumbe kutoka katika hali ya kutokuwako, kisha Atawarudisha baada ya kutoweka kwao, kama alivyoanzisha mara ya kwanza uumbaji mpya na kwamba kulifanya hili si jambo lisilowezekana na Yeye? Hakika hilo kwa Mwenyezi Mungu ni lepesi kama lilivyokuwa lepesi lile la kuanzisha uumbaji wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ سِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱنظُرُواْ كَيۡفَ بَدَأَ ٱلۡخَلۡقَۚ ثُمَّ ٱللَّهُ يُنشِئُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأٓخِرَةَۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia wenye kukanusha kufufuliwa baada ya kufa, «Endeni katika ardhi, muangalie namna Mwenyezi Mungu Alivyoanzisha uumbaji na Asielemewe kuuanzisha hapo mwanzo?» Hivyo basi Hataelemewa na kule kuuanzilisha upya uanzilishaji mwingine. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu, hakuna jambo lolote Alitakalo linalomshinda.
Tefsiri na arapskom jeziku:
يُعَذِّبُ مَن يَشَآءُ وَيَرۡحَمُ مَن يَشَآءُۖ وَإِلَيۡهِ تُقۡلَبُونَ
Anamuadhibu Anayemtaka kati ya viumbe Vyake kwa makosa waliyoyafanya siku za uhai wao, na Anawarehemu Anaowataka miongoni mwao, kati ya wale waliotubia, wakaamini na wakafanya matendo mema. Na Kwake Yeye mtarejeshwa muhesabiwe na mulipwe kwa mliyoyafanya.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَآ أَنتُم بِمُعۡجِزِينَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا فِي ٱلسَّمَآءِۖ وَمَا لَكُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ مِن وَلِيّٖ وَلَا نَصِيرٖ
Na hamkuwa nyinyi, enyi watu, ni wenye kumshinda Mwenyezi Mungu katika ardhi wala katika mbingu iwapo mtamuasi. Na nyinyi hamuna badala ya Mwenyezi Mungu mtegemewa yoyote wa kuyasimamia mambo yenu, wala msaidizi wa kuwaokoa nyinyi na Mwenyezi Mungu iwapo Anawatakia mabaya.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَلِقَآئِهِۦٓ أُوْلَٰٓئِكَ يَئِسُواْ مِن رَّحۡمَتِي وَأُوْلَٰٓئِكَ لَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ
Na wenye kukanusha hoja za Mwenyezi Mungu na kupinga dalili Zake, hao hawatakuwa na matarajio ya rehema yangu huko Akhera watakapoishuhudia adhabu iliyoandaliwa kwao, na wao watakuwa na adhabu yenye uchungu na iumizayo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَمَا كَانَ جَوَابَ قَوۡمِهِۦٓ إِلَّآ أَن قَالُواْ ٱقۡتُلُوهُ أَوۡ حَرِّقُوهُ فَأَنجَىٰهُ ٱللَّهُ مِنَ ٱلنَّارِۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Basi jawabu ya watu wa Ibrāhīm haikuwa isipokuwa ni kuambiana wao kwa wao, «Muueni au mchomeni kwa moto!» Wakamtupa motoni, na Mwenyezi Mungu Akamuokoa nao, na akaufanya kuwa ni baridi na salama kwake. Hakika katika kumuokoa kwetu Ibrāhīm kutokana na moto pana dalili na hoja kwa watu wanaomuamini Mwenyezi Mungu na kufanya matendo yanayoambatana na Sheria Yake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَقَالَ إِنَّمَا ٱتَّخَذۡتُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ أَوۡثَٰنٗا مَّوَدَّةَ بَيۡنِكُمۡ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ ثُمَّ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ يَكۡفُرُ بَعۡضُكُم بِبَعۡضٖ وَيَلۡعَنُ بَعۡضُكُم بَعۡضٗا وَمَأۡوَىٰكُمُ ٱلنَّارُ وَمَا لَكُم مِّن نَّٰصِرِينَ
Na Akasema Ibrāhīm kuwaambia watu wake, «Enyi watu wangu! Kwa hakika, nyinyi mumewaabudu waungu wa ubatilifu, mumewafanya wao ni waabudiwa badala ya Mwenyezi Mungu, mnapendana juu ya kuwaabudu na mnajipendekeza kwa kuwatumikia. Kisha, Siku ya Kiyama, baadhi yenu watajiepusha na wengine na mtalaaniana nyinyi kwa nyinyi, na mwisho wenu ni Moto, na hamtakuwa na msaidizi wa kuwazuia kuuingia.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ فَـَٔامَنَ لَهُۥ لُوطٞۘ وَقَالَ إِنِّي مُهَاجِرٌ إِلَىٰ رَبِّيٓۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ
Lūṭ akamuamini Ibrāhīm na akaufuata mwenendo wake. Na Ibrāhīm akasema, «Mimi nitaiwacha nchi ya watu wangu na nitaenda kwenye ardhi iliyobarikiwa, nayo ni Shām, kwani Mwenyezi Mungu ni Mshindi Asiyeshindwa ni Mwingi wa hekima katika uendeshaji mambo Wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَوَهَبۡنَا لَهُۥٓ إِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ وَجَعَلۡنَا فِي ذُرِّيَّتِهِ ٱلنُّبُوَّةَ وَٱلۡكِتَٰبَ وَءَاتَيۡنَٰهُ أَجۡرَهُۥ فِي ٱلدُّنۡيَاۖ وَإِنَّهُۥ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ لَمِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Na tukamtunukia yeye Isḥāq, mtoto wake, na Y'qub, mtoto wa mtoto wake. Na tukawafanya, katika kizazi chake, Mitume na tukawaletea Vitabu. Na tukampa yeye malipo mema ya mitihani aliyoipata kwa ajili yetu, nayo ni kutajwa vizuri na kuwa na wana wema duniani. Na kwa hakika, yeye huko Akhera ni miongoni mwa watu wema.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلُوطًا إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِۦٓ إِنَّكُمۡ لَتَأۡتُونَ ٱلۡفَٰحِشَةَ مَا سَبَقَكُم بِهَا مِنۡ أَحَدٖ مِّنَ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Mkumbuke na umtaje Lūṭ, ewe Mtume, alipowaambia watu wake, «Kwa hakika, nyinyi mnaleta kitendo kichafu, hakuna yoyote katika viumbe aliyetangulia kukifanya.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَئِنَّكُمۡ لَتَأۡتُونَ ٱلرِّجَالَ وَتَقۡطَعُونَ ٱلسَّبِيلَ وَتَأۡتُونَ فِي نَادِيكُمُ ٱلۡمُنكَرَۖ فَمَا كَانَ جَوَابَ قَوۡمِهِۦٓ إِلَّآ أَن قَالُواْ ٱئۡتِنَا بِعَذَابِ ٱللَّهِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Je, ni vipi nyinyi mnawajilia wanaume kupitia sehemu zao za nyuma, mnavamia njia za wasafiri kwa kitendo chenu kiovu na mnafanya vitendo vibaya kwenye mabaraza yenu, kama vile kuwacheza shere watu, kuwarushia mawe wapita njia na kuwakera kwa maneno na vitendo kwa namna isiyofaa?» Katika haya kuna tangazo kwamba haifai watu kukusanyika juu ya jambo baya ambalo Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wamelikataza. Watu wa Lūṭ hawakuwa na jawabu la kumpa isipokuwa ni kusema, «tuletee adhabu ya Mwenyezi Mungu ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli katika hayo unayoyasema na ni miongoni mwa watekelezaji katika ahadi unayoitoa.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قَالَ رَبِّ ٱنصُرۡنِي عَلَى ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡمُفۡسِدِينَ
Akasema, «Mola wangu! Nipe ushindi juu ya watu waharibifu kwa kuwateremshia adhabu, kwa kuwa wameuzua uchafu huu na wameendelea nao» Na Mwenyezi Mungu Akaikubali dua yake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَمَّا جَآءَتۡ رُسُلُنَآ إِبۡرَٰهِيمَ بِٱلۡبُشۡرَىٰ قَالُوٓاْ إِنَّا مُهۡلِكُوٓاْ أَهۡلِ هَٰذِهِ ٱلۡقَرۡيَةِۖ إِنَّ أَهۡلَهَا كَانُواْ ظَٰلِمِينَ
Na Malaika walipomjia Ibrāhīm na habari ya furaha itokayo kwa Mwenyezi Mungu ya (kuzaliwa) Isḥāq, na nyuma ya Isḥāq ni mwanawe, Ya’qūb, walisema wale Malaika, «Sisi ni wenye kuwaangamiza watu wa kijiji cha watu wa Lūṭ, nacho ni Sadūm, kwa kuwa watu wake wamekuwa ni wenye kujidhulumu wenyewe kwa kumuasi Mwenyezi Mungu.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قَالَ إِنَّ فِيهَا لُوطٗاۚ قَالُواْ نَحۡنُ أَعۡلَمُ بِمَن فِيهَاۖ لَنُنَجِّيَنَّهُۥ وَأَهۡلَهُۥٓ إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ كَانَتۡ مِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ
Akasema Ibrāhīm kuwaambia Malaika, «Huko kuna Lūṭ, na yeye si miongoni mwa madhalimu.» Malaika wakasema, «Sisi tunamjua zaidi aliye huko. Tutamuokoa, yeye na watu wa nyumbani kwake, na maangamivu yatakayowashukia watu wa kijiji chake, isipokuwa mke wake atakayesalia kwenye maangamivu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَمَّآ أَن جَآءَتۡ رُسُلُنَا لُوطٗا سِيٓءَ بِهِمۡ وَضَاقَ بِهِمۡ ذَرۡعٗاۖ وَقَالُواْ لَا تَخَفۡ وَلَا تَحۡزَنۡ إِنَّا مُنَجُّوكَ وَأَهۡلَكَ إِلَّا ٱمۡرَأَتَكَ كَانَتۡ مِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ
Na Malaika walipomjia Lūṭ, hilo lilimkera, kwa kuwa yeye aliwadhania ni wageni wanadamu na akaingiwa na masikitiko kwa kuwako kwao kwa kuwa ajua ubaya wa kitendo cha watu wake, na wao wakamwambia, «Usituogopee, kwani watu wako hawatatufikia. Na wala usiwe na masikitiko kwa kuwa tunakupasha habari kuwa sisi ni wenye kuwaangamiza wao. Sisi ni wenye kukuokoa wewe na hiyo adhabu itakayowashukia watu wako na ni wenye kuwaokoa watu wa nyumbani kwako pamoja nawe isipokuwa mke wako, kwani yeye ni mwenye kuangamia akiwa na wale wenye kuangamia katika watu wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنَّا مُنزِلُونَ عَلَىٰٓ أَهۡلِ هَٰذِهِ ٱلۡقَرۡيَةِ رِجۡزٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ بِمَا كَانُواْ يَفۡسُقُونَ
«Sisi ni wenye kuwateremshia watu wa kijiji hiki adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya kumuasi kwao Mwenyezi Mungu na kufanya kwao machafu.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَقَد تَّرَكۡنَا مِنۡهَآ ءَايَةَۢ بَيِّنَةٗ لِّقَوۡمٖ يَعۡقِلُونَ
Na tulizibakisha, katika nyumba za watu wa Lūṭ, athari zilizo wazi kwa watu wanaoelewa mambo ya kuwapa mazingatio na kunufaika kwayo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِلَىٰ مَدۡيَنَ أَخَاهُمۡ شُعَيۡبٗا فَقَالَ يَٰقَوۡمِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَٱرۡجُواْ ٱلۡيَوۡمَ ٱلۡأٓخِرَ وَلَا تَعۡثَوۡاْ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُفۡسِدِينَ
Na tulimtumiliza, kwa watu wa Madyan, ndugu yao, Shu'ayb. Akawaambia, «Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu Peke Yake, na mumtakasie Ibada, kwani nyinyi hamuna Mola isipokuwa Yeye. Na kuweni na matarajio mema, kwa ibada mnazofanya, kupata malipo mazuri ya Siku ya Akhera, na msifanye uharibifu na maasia kwa wingi, na msijikite juu ya hayo. Lakini tubieni kwa Mwenyezi Mungu kwa makosa hayo na mrudi Kwake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلرَّجۡفَةُ فَأَصۡبَحُواْ فِي دَارِهِمۡ جَٰثِمِينَ
Wakamkanusha Shu'ayb watu wa Madyan kwa yale aliyokuja nayo ya utume kutoka kwa Mweyezi Mungu, basi wakapatikana na msukosuko mkali, wakawa wamelala chini kwenye nyumba zao hali ya kuwa wameangamia.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَعَادٗا وَثَمُودَاْ وَقَد تَّبَيَّنَ لَكُم مِّن مَّسَٰكِنِهِمۡۖ وَزَيَّنَ لَهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ أَعۡمَٰلَهُمۡ فَصَدَّهُمۡ عَنِ ٱلسَّبِيلِ وَكَانُواْ مُسۡتَبۡصِرِينَ
Na tukawaangamiza kina 'Ād na Thamūd, na yameshaonekana na nyinyi magofu ya nyumba zao, vile yalivyokuwa matupu, hayana mtu yoyote katika wakazi wake, na vile mateso yetu yalivyowashukia wao wote. Na Shetani aliwapambia wao matendo yao maovu, na kwa hivyo akawazuia wasiifuate njia ya Mwenyezi Mungu na njia ya kumuamini Yeye na Mitume Wake, na walikuwa wakijiongoza kuona njia katika ukafiri wao na upotevu wao wakijifurahisha nayo, wakidhani kwamba wao wako kwenye uongofu na usawa, ilhali wao wamezama kwenye upotevu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَقَٰرُونَ وَفِرۡعَوۡنَ وَهَٰمَٰنَۖ وَلَقَدۡ جَآءَهُم مُّوسَىٰ بِٱلۡبَيِّنَٰتِ فَٱسۡتَكۡبَرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا كَانُواْ سَٰبِقِينَ
Na tulimuangamiza Qārūn, Fir'awn na Hāmān. Na wote hao Mūsā aliwajia na dalili waziwazi, wakajifanya wakubwa katika ardhi na wakafanya kiburi humo. Na hawakuwa wao ni wenye kutuponyoka, bali sisi tulikuwa tuna uweza juu yao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَكُلًّا أَخَذۡنَا بِذَنۢبِهِۦۖ فَمِنۡهُم مَّنۡ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِ حَاصِبٗا وَمِنۡهُم مَّنۡ أَخَذَتۡهُ ٱلصَّيۡحَةُ وَمِنۡهُم مَّنۡ خَسَفۡنَا بِهِ ٱلۡأَرۡضَ وَمِنۡهُم مَّنۡ أَغۡرَقۡنَاۚ وَمَا كَانَ ٱللَّهُ لِيَظۡلِمَهُمۡ وَلَٰكِن كَانُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ
Kila mmoja, kati ya hao waliotajwa, tulimkamata kwa dhambi zake: kati yao kuna wale tuliyowatumia mawe ya udongo ulioshikana, nao ni watu wa Lūṭ, na kati yao kuna waliopatwa na ukelele, nao ni watu wa Ṣāliḥ na watu wa Shu'ayb , na kati yao kuna tuliowadidimiza ardhini kama vile Qārūn, na katika wao kuna tuliowazamisha majini, nao ni watu wa Nūḥ na Fir'awn na jamaa zake. Na Mwenyezi Mungu hakuwa ni Mwenye kuwaangamiza hawa kwa dhambi wengine akawa ni mwenye kuwadhulumu kwa kuwaangamiza wao bila kustahili, lakini wao walikuwa wakijidhulumu wenyewe kwa kujistarehesha kwa neema za Mola wao na kumuabudu asiyekuwa Yeye.
Tefsiri na arapskom jeziku:
مَثَلُ ٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ أَوۡلِيَآءَ كَمَثَلِ ٱلۡعَنكَبُوتِ ٱتَّخَذَتۡ بَيۡتٗاۖ وَإِنَّ أَوۡهَنَ ٱلۡبُيُوتِ لَبَيۡتُ ٱلۡعَنكَبُوتِۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ
Mfano wa wale waliowafanya masanamu ni wategemewa badala ya Mwenyezi Mungu, wakawa wanatarajia msaada wao, ni kama mfano wa buibui aliyejitengenezea nyumba ili imuhifadhi, isimfalie kitu alipokuwa na haja nayo. Hivyo basi ndivyo walivyo hawa washirikina, hawakuwafalia kitu wale waliowachukuwa kuwa ni wasaidizi wao badala ya Mwenyezi Mungu. Na kwa hakika, nyumba iliyo dhaifu zaidi ni nyumba ya buibui, na lau wao wangalikuwa wakilijua hilo hawangaliwafanya wao ni wasaidizi wenye kutegemewa badala ya Mwenyezi Mungu, kwani wao hawawanufaishi wala hawawadhuru.
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا يَدۡعُونَ مِن دُونِهِۦ مِن شَيۡءٖۚ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ
Hakika Mwenyezi Mungu Anavijua vile wanavyomfananisha navyo washirikina na kumshirikisha navyo, na kwamba hivyo , kwa hakika, si kitu chochote, bali ni majina tu waliyoyaita, havinufaishi wala havidhuru. Na Yeye Ndiye Mshindi Mwenye uweza wa kuwatesa waliomkufuru, Ndiye Mwenye hekima katika uendeshaji mambo Wake na utengenezaji Wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَتِلۡكَ ٱلۡأَمۡثَٰلُ نَضۡرِبُهَا لِلنَّاسِۖ وَمَا يَعۡقِلُهَآ إِلَّا ٱلۡعَٰلِمُونَ
Na mifano hii tunawapigia watu , ili wanufaike nayo na wajifunze kwayo. Na hawaielewi isipokuwa wale wanaomjua Mwenyezi Mungu na kuzijua aya Zake na Sheria Zake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
خَلَقَ ٱللَّهُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّلۡمُؤۡمِنِينَ
Mwenyezi Mungu Ameumba mbingu na ardhi kwa uadilifu na usawa. Hakika katika uumbaji Wake huo kuna ushahidi mkubwa, kwa wanaoamini, wa uweza Wake na kupwekeka kwake kwa uungu. Na Amewahusu Waumini kwa kuwataja kwa kuwa wao ndio wanaonufaika na huo ushahidi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
ٱتۡلُ مَآ أُوحِيَ إِلَيۡكَ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَأَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَۖ إِنَّ ٱلصَّلَوٰةَ تَنۡهَىٰ عَنِ ٱلۡفَحۡشَآءِ وَٱلۡمُنكَرِۗ وَلَذِكۡرُ ٱللَّهِ أَكۡبَرُۗ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ مَا تَصۡنَعُونَ
Isome hii Qur’ani iliyoteremshwa kwako, na uifuate kivitendo, na utekeleze Swala kwa mipaka yake, kwani utunzaji wa Swala unamkataza mtu kuingia kwenye vitendo vya uasi na makatazo. Hivyo ni kwamba mwenye kuzitimiza nguzo zake na masharti yake, moyo wake unang’ara, Imani yake inazidi, hima yake ya kufanya mema inapata nguvu na matamanio yake ya kufanya mabaya yanapungua au yanaondoka. Na kwa hakika, kumtaja Mwenyezi Mungu katika Swala na isiyokuwa Swala ni jambo kubwa na bora kuliko kitu chochote. Na Mwenyezi Mungu Anayajua mnayoyatenda ya uzuri na ubaya, hivyo basi Atawalipa kwa hayo malipo makamilifu zaidi na yanayotosha zaidi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ وَلَا تُجَٰدِلُوٓاْ أَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ إِلَّا بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ إِلَّا ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ مِنۡهُمۡۖ وَقُولُوٓاْ ءَامَنَّا بِٱلَّذِيٓ أُنزِلَ إِلَيۡنَا وَأُنزِلَ إِلَيۡكُمۡ وَإِلَٰهُنَا وَإِلَٰهُكُمۡ وَٰحِدٞ وَنَحۡنُ لَهُۥ مُسۡلِمُونَ
Na wala msijadiliane, enyi Waumini, na Mayahudi na Wanaswara isipokuwa kwa njia nzuri na maneno mazuri na kulingania kwenye haki kwa njia sahali yenye kupelekea kwenye lengo hilo, isipokuwa wale ambao wamekaa kando na haki wakafanya ushindani na kiburi na wakatangaza vita juu yenu, basi hao piganeni nao kwa upanga mpaka waamini au watoe jizia (kodi maalumu) kwa mkono na wao wakiwa katika hali ya unyonge. Na semeni, «Tumeiamini Qur’ani iliyoteremshwa kwetu, na tumeiamini Taurati na Injili ambazo mliteremshiwa, na Mola wetu na Mola wenu ni Mmoja Hana mshirika Wake katika uungu Wake, wala katika sifa Yake ya kuwa ni Mola, wala majina Yake na sifa Zake. Na sisi ni wenye kunyenyekea na kujifanya wanyonge Kwake kwa kumtii katika yale Aliyotuamrisha na Aliyotukataza.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَذَٰلِكَ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَۚ فَٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ يُؤۡمِنُونَ بِهِۦۖ وَمِنۡ هَٰٓؤُلَآءِ مَن يُؤۡمِنُ بِهِۦۚ وَمَا يَجۡحَدُ بِـَٔايَٰتِنَآ إِلَّا ٱلۡكَٰفِرُونَ
Na kama tulivyowateremshia Kitabu, ewe Mtume, wale Mitume waliokuwa kabla yako, vilevile tumekuteremshia Kitabu hiki chenye kusadikisha Vitabu vilivyotangulia. Basi wale tuliyowapa Kitabu miongoni mwa Wana wa Isrāīl wakamjua vile inavyotakikana wamjue, wanaiamini Qur’ani. Na kati ya hawa Warabu wa Kikureshi kuna wanaomuamini. Na hawaikanushi Qur’ani au kuzifanyia shaka dalili zake na hoja zake zenye ushahidi uliyo wazi isipokuwa makafiri ambao mienendo yao ni kukataa na kufanya ushindani.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا كُنتَ تَتۡلُواْ مِن قَبۡلِهِۦ مِن كِتَٰبٖ وَلَا تَخُطُّهُۥ بِيَمِينِكَۖ إِذٗا لَّٱرۡتَابَ ٱلۡمُبۡطِلُونَ
Na miongoni mwa miujiza yako iliyo wazi, ewe Mtume, ni kuwa wewe hukusoma kitabu wala hukuandika herufi zozote kwa mkono wako wa kulia kabla ya hii Qur’ani kukuteremkia, na hali wao wanalijua hilo. Na lau ungalikuwa ni mwenye kusoma au kuandika kabla hujaletewa wahyi wangalilifanyia shaka hilo hao wapotofu na wangalisema, «Amejifunza hiyo (Qur’ani) au ameinakili kutoka kwenye vitabu vilivyotangulia.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
بَلۡ هُوَ ءَايَٰتُۢ بَيِّنَٰتٞ فِي صُدُورِ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَۚ وَمَا يَجۡحَدُ بِـَٔايَٰتِنَآ إِلَّا ٱلظَّٰلِمُونَ
Lakini Qur’ani ni aya zilizofunuka zilizo wazi katika kuutolea ushahidi ukweli, wanavyuoni wanaihifadhi. Na hawazikanushi aya zetu na kuzikataa isipokuwa washindani wanaoijua haki na kuiepuka.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَقَالُواْ لَوۡلَآ أُنزِلَ عَلَيۡهِ ءَايَٰتٞ مِّن رَّبِّهِۦۚ قُلۡ إِنَّمَا ٱلۡأٓيَٰتُ عِندَ ٱللَّهِ وَإِنَّمَآ أَنَا۠ نَذِيرٞ مُّبِينٌ
Na washirikina walisema, «Si ateremshiwe Muammad dalili na hoja kutoka kwa Mola wake, kama vile ngamia wa Ṣāliḥ na fimbo ya Mūsā!» Waambie, «Jambo la miujiza hii liko kwa Mwenyezi Mungu, Akitaka Ataiteremsha na Akitaka Ataizuia. Na hakika ni kwamba mimi ni muonyaji, ninawatahadharisha na ukali wa adhabu Yake na mateso Yake, na ni mwenye kuwaonyesha njia ya haki na batili.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَوَلَمۡ يَكۡفِهِمۡ أَنَّآ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ يُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَرَحۡمَةٗ وَذِكۡرَىٰ لِقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Kwani haikuwatosha washirikina hawa ili wajue ukweli wako, ewe Mtume, kuwa sisi tumekuteremshia Qur’ani inayosomwa kwao? Hakika katika hii Qur’ani kuna rehema kwa Waumini, ulimwenguni na Akhera, na kuna ukumbusho wa kujikumbusha nao wa mazingatio na mawaidha.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ كَفَىٰ بِٱللَّهِ بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡ شَهِيدٗاۖ يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۗ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِٱلۡبَٰطِلِ وَكَفَرُواْ بِٱللَّهِ أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ
Sema, «Inatosha kuwa Mwenyezi Mungu ni Shahidi baina yangu mimi na nyinyi juu ya ukweli wangu wa kuwa mimi ni Mtume Wake, na juu ya kunikanusha kwenu mimi na kuirudisha kwenu haki niliyokuja nayo kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Anavijuwa vilivyomo mbinguni na ardhini», hakuna kinachofichamana na Yeye chochote kile kilichoko ndani ya hivyo viwili. Na wale waliouamini urongo na wakamkanusha Mwenyezi Mungu, pamoja na kuwepo dalili hizi zilizo wazi, hao ndiyo wenye hasara ulimwenguni na Akhera.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَيَسۡتَعۡجِلُونَكَ بِٱلۡعَذَابِ وَلَوۡلَآ أَجَلٞ مُّسَمّٗى لَّجَآءَهُمُ ٱلۡعَذَابُۚ وَلَيَأۡتِيَنَّهُم بَغۡتَةٗ وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ
Na wanakuharakisha, ewe Mtume, hawa washirikina wa watu wako uwaletee adhabu kwa kukufanyia shere. Na lau si Mwenyezi Mungu kuwa Amewawekea wakati wa kuadhibiwa wao duniani usiotangulia wala kuchelewa, ingaliwajia wao adhabu pale walipoitaka. Na kwa hakika itawajia ghafula na hali wao hawaitambui wala kuihisi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
يَسۡتَعۡجِلُونَكَ بِٱلۡعَذَابِ وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمُحِيطَةُۢ بِٱلۡكَٰفِرِينَ
Wanakuharakisha uwaletee adhabu ulimwenguni, na hali hiyo ni yenye kuwajia hapana budi, ima hapa ulimwenguni au huko Akhera. Na kwa hakika adhabu ya Jahanamu huko Akhera ni yenye kuwazunguka, hawana makimbilio nayo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
يَوۡمَ يَغۡشَىٰهُمُ ٱلۡعَذَابُ مِن فَوۡقِهِمۡ وَمِن تَحۡتِ أَرۡجُلِهِمۡ وَيَقُولُ ذُوقُواْ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Hiyo Siku ya Kiyama, adhabu ya Jahanamu itawafinika makafiri upande wa juu ya vichwa vyao na upande wa chini ya nyayo zao. Hivyo basi Moto utawazunguka pande zao zote, na Mwenyezi Mungu Atasema kuwaambia wakati huo, «Onjeni malipo ya yale mliokuwa mkiyafanya ulimwenguni, ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kufanya uhalifu na madhambi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
يَٰعِبَادِيَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِنَّ أَرۡضِي وَٰسِعَةٞ فَإِيَّٰيَ فَٱعۡبُدُونِ
«Enyi waja wangu mlioamini! Iwapo muna shida ya kudhihirisha Imani na ibada ya Mwenyezi Mungu Peke Yake, basi hamieni kwenye ardhi ya Mwenyezi Mungu iliyo kunjufu na munitakasie ibada mimi peke yangu.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
كُلُّ نَفۡسٖ ذَآئِقَةُ ٱلۡمَوۡتِۖ ثُمَّ إِلَيۡنَا تُرۡجَعُونَ
Kila nafsi iliyo hai ni yenye kuonja kifo, kisha kwetu sisi mtarejea muhesabiwe na mulipwe.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَنُبَوِّئَنَّهُم مِّنَ ٱلۡجَنَّةِ غُرَفٗا تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ نِعۡمَ أَجۡرُ ٱلۡعَٰمِلِينَ
Na wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya matendo mema waliyoamrishwa kwayo, tutawatayarishia katika Pepo vyumba vilivyo juu, ambavyo chini yake inapita mito, hali ya kukaa humo milele.Neema ya malipo ya wenye kufanya utiifu kwa Mwenyezi Mungu ni Vyumba hivi vilivyoko ndani ya Mabustani ya starehe.
Tefsiri na arapskom jeziku:
ٱلَّذِينَ صَبَرُواْ وَعَلَىٰ رَبِّهِمۡ يَتَوَكَّلُونَ
Mabustani hayo yaliyotajwa ni ya Waumini waliovumilia katika kumuabudu Mwenyezi Mungu, wakashikamana na dini yao na wakawa wanamtegemea Mwenyezi Mungu katika riziki zao na kupigana jihadi na maadui wao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَأَيِّن مِّن دَآبَّةٖ لَّا تَحۡمِلُ رِزۡقَهَا ٱللَّهُ يَرۡزُقُهَا وَإِيَّاكُمۡۚ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Ni viumbe vingapi vitambaavyo visivyojiwekea akiba ya chakula chao cha kesho, kama vile mwanadamu anavyofanya. Basi Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kuwa juu, Anaviruzuku kama Anavyowaruzuku nyinyi. Na Yeye ni Msikizi wa maneno yenu, ni Mjuzi wa vitendo vyenu na mawazo ya nyoyo zenu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَئِن سَأَلۡتَهُم مَّنۡ خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَسَخَّرَ ٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ لَيَقُولُنَّ ٱللَّهُۖ فَأَنَّىٰ يُؤۡفَكُونَ
Na ukiwauliza, ewe Mtume, hao washirikina,»Ni nani aliyeumba mbingu na ardhi kwa mpango huu mzuri na akalidhalilisha jua na mwezi?» Watasema, «Aliyeviumba hivyo ni Mwenyezi Mungu Peke Yake.» Basi vipi wao watapotoshwa waache kumuamini Mwenyezi Mungu, Muumba na Muendeshaji wa kila kitu, na wakawa wanamuabudu asiyekuwa Yeye? Basi uonee ajabu uzushi wao na urongo wao!
Tefsiri na arapskom jeziku:
ٱللَّهُ يَبۡسُطُ ٱلرِّزۡقَ لِمَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦ وَيَقۡدِرُ لَهُۥٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ
Mwenyezi Mungu, aliyetakasika na kuwa juu, Anampanulia riziki Anayemtaka na Anawabania wengine katika wao, kwa kuwa Anayajua yanayowafaa waja Wake. Hakika Mwenyezi Mungu kwa kila jambo, katika hali zenu na mambo yenu, ni Mjuzi, hakuna chochote kinachofichamana Kwake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَئِن سَأَلۡتَهُم مَّن نَّزَّلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَحۡيَا بِهِ ٱلۡأَرۡضَ مِنۢ بَعۡدِ مَوۡتِهَا لَيَقُولُنَّ ٱللَّهُۚ قُلِ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِۚ بَلۡ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يَعۡقِلُونَ
Na ukiwauliza, ewe Mtume, hao washirikina, «Ni nani anayeteremsha maji kutoka mawinguni, yakaotesha mimea juu ya ardhi baada ya kuwa imekauka?» watakwambia huku wakikubali, «Mwenyezi Mungu Peke Yake Ndiye Anayeyateremsha hayo.» Sema, «Shukrani ni za Mwenyezi Mungu Aliyedhihirisha hoja yako kwao. Lakini wengi wao hawafahamu yanayowafaa wala yanayowadhuru, na lau waelewa hawangalimshirikisha Mwenyezi Mungu na Mwengine.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا هَٰذِهِ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَآ إِلَّا لَهۡوٞ وَلَعِبٞۚ وَإِنَّ ٱلدَّارَ ٱلۡأٓخِرَةَ لَهِيَ ٱلۡحَيَوَانُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ
Na haukuwa uhai huu wa ulimwengu isipokuwa ni pumbao na mchezo wa kuzifanya nyoyo zipumbae na miili icheza, kwa sababu ya pambo na matamanio, kisha yanaondoka haraka. Na kwa hakika, nyumba ya Akhera ndiyo uhai wa kikweli na wa daima usikokuwa na kifo ndani yake. Lau watu wanalijua hilo hawangalifadhilisha nyumba ya kutoweka juu ya Nyumba ya kusalia.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَإِذَا رَكِبُواْ فِي ٱلۡفُلۡكِ دَعَوُاْ ٱللَّهَ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَ فَلَمَّا نَجَّىٰهُمۡ إِلَى ٱلۡبَرِّ إِذَا هُمۡ يُشۡرِكُونَ
Na wanapopanda makafiri kwenye majahazi baharini, na wakaogopa kuzama, wanampwekesha Mwenyezi Mungu na kumtakasia dua wakati wa shida yao. Na Anapowaokoa akawafikisha kwenye nchi kavu, na shida ikawaondokea, wanarudi kwenye ushirikina wao. Hakika yao wao, kwa kufanya hivi, wanagongana, wanampwekesha Mwenyezi Mungu kipindi cha shida na wanamshirikisha kipindi cha raha.
Tefsiri na arapskom jeziku:
لِيَكۡفُرُواْ بِمَآ ءَاتَيۡنَٰهُمۡ وَلِيَتَمَتَّعُواْۚ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ
Na kushirikisha kwao baada ya sisi kuwaneemesha kwa kuwaokoa na bahari, ni ili iwe mwisho wake ni kuzikanusha zile tulizowaneemesha katika nafsi zao na mali zao na ili wakamilishe kujistarehesha kwao katika hii dunia. Basi wataujua uharibikaji wa matendo yao na kile Alichowaandalia wao Mwenyezi Mungu cha adhabu kali Siku ya Kiyama. Na katika hilo pana onyo na tahadharisho kwao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّا جَعَلۡنَا حَرَمًا ءَامِنٗا وَيُتَخَطَّفُ ٱلنَّاسُ مِنۡ حَوۡلِهِمۡۚ أَفَبِٱلۡبَٰطِلِ يُؤۡمِنُونَ وَبِنِعۡمَةِ ٱللَّهِ يَكۡفُرُونَ
Kwani hawakushuhudia makafiri wa Makkah kwamba Mwenyezi Mungu Amewawekea Makkah kuwa ni mahali patakatifu penye amani, watu wake wanapata amani humo ya nafsi zao na mali zao, hali watu walio pambizoni mwake, nje ya eneo takatifu, wananyakuliwa hawana amani? Je, ni ushirikina wanaouamini na ni neema ya Mwenyezi Mungu Aliyowahusu wao nayo, wanayoikanusha, wakawa hawamuabudu Yeye, Peke Yake, bila mwingine?
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَوۡ كَذَّبَ بِٱلۡحَقِّ لَمَّا جَآءَهُۥٓۚ أَلَيۡسَ فِي جَهَنَّمَ مَثۡوٗى لِّلۡكَٰفِرِينَ
Hakuna yoyote aliye na udhalimu mkubwa kuliko yule aliyemkanusha Mwenyezi Mungu na akamnasibishia Mwenyezi Mungu upotevu alio nao na ubatilifu, au akaikanusha haki ambayo Mwenyezi Mungu Amemleta nayo Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie. Hakika ndani ya Moto ni makao ya aliyemkanusha Mwenyezi Mungu na akaukataa upweke Wake na akamkanusha Mtume Wake Muhammad,rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَٱلَّذِينَ جَٰهَدُواْ فِينَا لَنَهۡدِيَنَّهُمۡ سُبُلَنَاۚ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَمَعَ ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Na Waumini waliopigana jihadi na maadui wa Mwenyezi Mungu, nafsi na Shetani na wakavumilia kwenye misukosuko na makero katika njia ya Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu Atawaongoa kwenye wema na kuwasimamisha imara juu ya njia iliyolingana sawa. Na yoyote ambaye sifa yake ni hii, basi yeye amejifanyia wema nafsi yake na amewafanyia wema wengine. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kuwa juu, Yupo pamoja na wale viumbe wake waliofanya wema, kwa kuwapa ushindi, kuwatilia nguvu, kuwahifadhi na kuwaongoza.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Sura: Sura el-Ankebut
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Zatvaranje