Check out the new design

Prijevod značenja časnog Kur'ana - Prijevod na svahili jezik - Abdullah Muhammed i Nasir Hamis * - Sadržaj prijevodā


Prijevod značenja Sura: En-Nisa   Ajet:
وَٱللَّهُ يُرِيدُ أَن يَتُوبَ عَلَيۡكُمۡ وَيُرِيدُ ٱلَّذِينَ يَتَّبِعُونَ ٱلشَّهَوَٰتِ أَن تَمِيلُواْ مَيۡلًا عَظِيمٗا
Na Mwenyezi Mungu Anataka kuwakubalia toba zenu na kuyasamehe makosa yenu; na wale wanaofuata matamanio yao na starehe zao, wanataka mupotoke muwe kando na Dini kabisa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
يُرِيدُ ٱللَّهُ أَن يُخَفِّفَ عَنكُمۡۚ وَخُلِقَ ٱلۡإِنسَٰنُ ضَعِيفٗا
Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kwa sheria Zake Alizowaekea, Anataka kuwafanyia sahali na kutowafanyia mkazo, kwa kuwa nyinyi mumeumbwa mkiwa madhaifu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَأۡكُلُوٓاْ أَمۡوَٰلَكُم بَيۡنَكُم بِٱلۡبَٰطِلِ إِلَّآ أَن تَكُونَ تِجَٰرَةً عَن تَرَاضٖ مِّنكُمۡۚ وَلَا تَقۡتُلُوٓاْ أَنفُسَكُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِكُمۡ رَحِيمٗا
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata sheria Yake kivitendo! Si halali kwa baadhi yenu kula mali ya wengine kati yenu pasi na haki, isipokuwa ikiwa itaambatana na Sheria na chumo la halali litokanalo na kuridhiana baina yenu. Na wala msiuane nyinyi kwa nyinyi mkaziangamiza nafsi zenu kwa kufanya maasia yaliyoharamishwa na Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye huruma sana katika kila Alilowaamrisha kwalo na kuwakataza nalo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٰلِكَ عُدۡوَٰنٗا وَظُلۡمٗا فَسَوۡفَ نُصۡلِيهِ نَارٗاۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عَلَى ٱللَّهِ يَسِيرًا
Na Mwenye kutenda Aliyoyakataza Mwenyezi Mungu ya kuchukua mali ya haramu, kama kuiba, kunyang’anya na kudanganya, kwa dhuluma na kukiuka mipaka ya Sheria, Mwenyezi Mungu Atamuingiza kwenye Moto alionje joto lake. Na hilo kwa Mwenyezi Mungu ni jepesi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِن تَجۡتَنِبُواْ كَبَآئِرَ مَا تُنۡهَوۡنَ عَنۡهُ نُكَفِّرۡ عَنكُمۡ سَيِّـَٔاتِكُمۡ وَنُدۡخِلۡكُم مُّدۡخَلٗا كَرِيمٗا
Mkijiepusha, enyi Waumini, na madhambi makubwa, kama kumshrikisha Mwenyezi Mungu, kuwaasi wazazi wawili, kumuua mtu bila ya haki na mengineyo, tutawasamehe madhambi yenu madogo yaliyo chini ya hayo na tutawaingiza mahali pema pa kuingia, napo ni Pepo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَا تَتَمَنَّوۡاْ مَا فَضَّلَ ٱللَّهُ بِهِۦ بَعۡضَكُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖۚ لِّلرِّجَالِ نَصِيبٞ مِّمَّا ٱكۡتَسَبُواْۖ وَلِلنِّسَآءِ نَصِيبٞ مِّمَّا ٱكۡتَسَبۡنَۚ وَسۡـَٔلُواْ ٱللَّهَ مِن فَضۡلِهِۦٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٗا
Wala msiyatamani mambo ambayo Mwenyezi Mungu Amewafadhilisha kwayo, baadhi yenu juu ya wengine, ya vipewa na riziki na mengineyo. Kwani Mwenyezi Mungu Amewapa wanaume malipo kulingana na matendo yao na Amewapa wanawake malipo kulingana na matendo yao. Na muombeni Mwenyezi Mungu Aliye Mkarimu na Mpaji Awape nyongeza za ukarimu Wake, badala ya kutamani tu. Hakika Mwenyezi Mungu kwa kila kitu ni Mjuzi, na Yeye Anayajua zaidi yanayowafaa waja Wake miongoni mwa kheri Aliyowagawia,
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلِكُلّٖ جَعَلۡنَا مَوَٰلِيَ مِمَّا تَرَكَ ٱلۡوَٰلِدَانِ وَٱلۡأَقۡرَبُونَۚ وَٱلَّذِينَ عَقَدَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡ فَـَٔاتُوهُمۡ نَصِيبَهُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدًا
Kila mmoja katika nyinyi tumemwekea warithi wenye kukirithi kilichoachwa na wazazi wawili na jamaa wa karibu. Na wale mliofungamana nao kwa mayamini yaliyotiliwa mkazo kuwa mtanusuriana na mtawapa kitu katika urithi, basi wapeni walichokadiriwa. Kurithiana kwa mikataba ya kunusuriana kulikuwako mwanzo wa Uislamu , kisha hukumu yake ikaondolewa kwa kuteremka aya za mirathi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuona kila kitu katika vitendo vyenu na Atawalipa kulingana navyo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Sura: En-Nisa
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - Prijevod na svahili jezik - Abdullah Muhammed i Nasir Hamis - Sadržaj prijevodā

Prevodili su je dr. Abdullah Muhammed Ebu Bekr i šejh Nasir Hamis.

Zatvaranje