Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Sadržaj prijevodā


Prijevod značenja Ajet: (17) Sura: Sura el-Maida
لَّقَدۡ كَفَرَ ٱلَّذِينَ قَالُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلۡمَسِيحُ ٱبۡنُ مَرۡيَمَۚ قُلۡ فَمَن يَمۡلِكُ مِنَ ٱللَّهِ شَيۡـًٔا إِنۡ أَرَادَ أَن يُهۡلِكَ ٱلۡمَسِيحَ ٱبۡنَ مَرۡيَمَ وَأُمَّهُۥ وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗاۗ وَلِلَّهِ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَاۚ يَخۡلُقُ مَا يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Kwa hakika wamekufuru Wanaswara wanaosema kwamba Mwenyezi Mungu ni Al-Masīh mwana wa Maryam. Sema, ewe Mtume, kuwaambia Wanaswara hawa wajinga, «Lau Al-Masīh angalikuwa Mungu, kama wanavyodai, angaliweza kuuzuia uamuzi wa Mwenyezi Mungu ukimjia wa kumwangamiza yeye na mama yake na watu wote wa ardhini. Na mama yake ‘Īsā alikufa, hakuweza kumkinga na kifo. Vilevile hawezi kujitetea nafsi yake. Kwani wote wawili ni waja miongoni mwa waja wa Mwenyezi Mungu, hawawezi kujiepusha na maangamivu. Hii ni dalili kuwa yeye ni mwanadamu kama wanadamu wengine. Na vitu vyote vilivyoko mbinguni na ardhini ni milki ya Mwenyezi Mungu, Anaumba na kupatisha anachotaka na yeye ni muweza wa kila kitu. Hakika ya tawhīd (kumpwekesha Mwenyezi Mungu) inawajibisha kupwekeka Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kwa sifa za uola na uungu; hakuna yoyote anayeshirikiana naye, katika viumbe Wake, kwa hilo. Na mara nyingi sana watu huingia kwenye ushirikina na upotevu kwa kuwatukuza Mitume na watu wema kupita kiasi, kama walivyopita kiasi Wanaswara katika kumtukuza Al-Masīh. Ulimwengu wote ni wa Mwenyezi Mungu, na viumbe viko kwenye mkono Wake Peke Yake. Na miujiza na alama kubwa zinazodhihiri, marejeo yake ni Mwenyezi Mungu.Anaumba, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, na Anafanya Anachotaka.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Ajet: (17) Sura: Sura el-Maida
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Zatvaranje