Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Sadržaj prijevodā

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Prijevod značenja Ajet: (32) Sura: Sura el-Kasas
ٱسۡلُكۡ يَدَكَ فِي جَيۡبِكَ تَخۡرُجۡ بَيۡضَآءَ مِنۡ غَيۡرِ سُوٓءٖ وَٱضۡمُمۡ إِلَيۡكَ جَنَاحَكَ مِنَ ٱلرَّهۡبِۖ فَذَٰنِكَ بُرۡهَٰنَانِ مِن رَّبِّكَ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦٓۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَوۡمٗا فَٰسِقِينَ
Ingiza mkono wako kwenye mfuko wako, utatoka mweupe pasipo na ubaya. Na jiambatishe mkono wako ukihisi khofu. Basi hizi ni dalili mbili zitokazo kwa Mola wako Mlezi kumpelekea Firauni na wakuu wa umma wake. Hakika hao walikuwa watu mafaasiki.
Na uingize mkono wako kwenye uwazi wa nguo yako utatoka mweupe, bila ya ila wala maradhi. Na jiambatishe mkono wako ubavuni mwako katika nguo ukiwa una khofu. Wala usishituke kwa kuona fimbo imekuwa nyoka, na kuona mkono wako umekuwa mweupe. Kwani miujiza hii miwili inatokana na Mwenyezi Mungu ya kumkabili nayo Firauni na kaumu yake watapo ukabili Ujumbe wako kwa kuukadhibisha na hali wametoka kwenye ut'iifu wa Mwenyezi Mungu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Ajet: (32) Sura: Sura el-Kasas
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Zatvaranje