Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Sadržaj prijevodā

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Prijevod značenja Ajet: (8) Sura: Sura el-Ahkaf
أَمۡ يَقُولُونَ ٱفۡتَرَىٰهُۖ قُلۡ إِنِ ٱفۡتَرَيۡتُهُۥ فَلَا تَمۡلِكُونَ لِي مِنَ ٱللَّهِ شَيۡـًٔاۖ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَا تُفِيضُونَ فِيهِۚ كَفَىٰ بِهِۦ شَهِيدَۢا بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۖ وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ
Au wanasema: Ameizua mwenyewe! Sema: Ikiwa nimeizua mimi, basi nyinyi hamwezi kunifaa chochote mbele ya Mwenyezi Mungu. Yeye anajua zaidi hayo mnayo ropokwa; anatosha kuwa shahidi baina yangu na nyinyi. Na Yeye ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
Bali wanasema hawa makafiri: Muhammad ameizua hii na akamsingizia Mwenyezi Mungu! Sema kuwajibu: Ikiwa mimi nimeizua hii Mwenyezi Mungu atanipatiliza upesi upesi, wala nyinyi hamwezi kunilinda hata kwa chembe ya adhabu. Yeye peke yake ndiye Mwenye kujua kabisa hayo mnayo ropokwa katika kuzitia kombo Aya zake. Na Yeye anatosha kunishuhudia ukweli wangu, na kukushuhudilieni nyinyi kuwa mnanikadhibisha. Na Yeye pekee, ndiye Mkunjufu wa msamaha kwa mwenye kutubu, Mkubwa wa rehema, kwa kuwapa muhula wenye kuasi ili wadiriki kurejea.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Ajet: (8) Sura: Sura el-Ahkaf
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Zatvaranje