Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Sadržaj prijevodā

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Prijevod značenja Ajet: (8) Sura: Sura el-Maida
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُونُواْ قَوَّٰمِينَ لِلَّهِ شُهَدَآءَ بِٱلۡقِسۡطِۖ وَلَا يَجۡرِمَنَّكُمۡ شَنَـَٔانُ قَوۡمٍ عَلَىٰٓ أَلَّا تَعۡدِلُواْۚ ٱعۡدِلُواْ هُوَ أَقۡرَبُ لِلتَّقۡوَىٰۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ
Enyi mlio amini! Kuweni wasimamizi madhubuti kwa ajili ya Mwenyezi Mungu mkitoa ushahidi kwa haki. Wala kuchukiana na watu kusikupelekeeni kutofanya uadilifu. Fanyeni uadilifu. Hivyo ndio kuwa karibu mno na uchamngu. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari za mnayo yatenda.
Enyi Waumini! Jitahidini kutimiza haki za Mwenyezi Mungu, na shuhudieni kwa haki baina ya watu. Chuki zenu kubwa kwa watu fulani zisikupelekeeni mkaacha kuwafanyia uadilifu. Bali jilazimisheni uadilifu, kwani hiyo ndiyo njia ya kupelekea kumcha Mwenyezi Mungu, na kuepukana na ghadhabu yake. Na mcheni Mwenyezi Mungu katika mambo yenu yote; kwani Yeye, Sub hanahu, anayajua vilivyo yote mnayo yafanya, naye atakulipeni kwayo. Uislamu unalingania uadilifu moja kwa moja, sawa kwa rafiki na adui.Haifai chuki ikakupelekea kudhulumu. Na hayo unapo amiliana na watu, na kuamiliana baina ya dola ya Kiislamu na dola nyenginezo. Na kumfanyia uadilifu adui kunaambiwa na Qur'ani kuwa ni karibu zaidi na uchamngu na usafi wa kidini. Lau kuwa wasia huu ungeli tumiwa katika sharia za baina ya madola basi pasingeli kuwapo vita. Kama kila dini ina kitambulisho chake na alama, basi kitambulisho cha Uislamu ni Dini ya Mungu Mmoja na Uadilifu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Ajet: (8) Sura: Sura el-Maida
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Zatvaranje