Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis * - Translations’ Index


Translation of the meanings Surah: Ibrāhīm   Ayah:
وَءَاتَىٰكُم مِّن كُلِّ مَا سَأَلۡتُمُوهُۚ وَإِن تَعُدُّواْ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ لَا تُحۡصُوهَآۗ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَظَلُومٞ كَفَّارٞ
Na Akawapa nyinyi kila mlichomuomba. Na mkihesabu ili kujua idadi ya neema za Mwenyezi Mungu juu yenu, hamtaweza kuzihesabu na kudhibiti idadi yake wala kusimama itakikanavyo kushukuru kwa hizo kwa wingi wake na aina zake. Hakika Binadamu ni mwingi wa kujidhulumu nafsi yake, ni mwingi wa kukanusha neema za Mola wake.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِيمُ رَبِّ ٱجۡعَلۡ هَٰذَا ٱلۡبَلَدَ ءَامِنٗا وَٱجۡنُبۡنِي وَبَنِيَّ أَن نَّعۡبُدَ ٱلۡأَصۡنَامَ
Na kumbuka, ewe Mtume, pindi Ibrāhīm aliposema akimuomba Mola Wake, baada ya kumfanyia makao mwanawe wa kiume, Isma'il, pamojaa na mamake, Hajar, kwenye bonde la Makkah, «Ewe Mola ijaalie Makkah ni mji wa amani, awe kila aliye humo yuko kwenye amani, na uniepushe mimi na wanangu na kuabudu masanamu.
Arabic explanations of the Qur’an:
رَبِّ إِنَّهُنَّ أَضۡلَلۡنَ كَثِيرٗا مِّنَ ٱلنَّاسِۖ فَمَن تَبِعَنِي فَإِنَّهُۥ مِنِّيۖ وَمَنۡ عَصَانِي فَإِنَّكَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
«Ewe Mola wangu! Masanamu wamesababisha kuwaepusha watu wengi na njia ya ukweli. Basi mwenye kunifuata mimi katika kumpwekesha Mwenyezi Mungu, yeye atakuwa kwenye Dini yangu na mwendo wangu, na mwenye kwenda kinyume na mimi, katika mambo ambayo si ya ushirikina, basi wewe ni Mwingi wa kusamehe dhambi za wenye kufanya madhambi, kwa fadhila zako, ni Mwingi wa huruma kwao, unamsamehe unayemtaka miongoni mwao.
Arabic explanations of the Qur’an:
رَّبَّنَآ إِنِّيٓ أَسۡكَنتُ مِن ذُرِّيَّتِي بِوَادٍ غَيۡرِ ذِي زَرۡعٍ عِندَ بَيۡتِكَ ٱلۡمُحَرَّمِ رَبَّنَا لِيُقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ فَٱجۡعَلۡ أَفۡـِٔدَةٗ مِّنَ ٱلنَّاسِ تَهۡوِيٓ إِلَيۡهِمۡ وَٱرۡزُقۡهُم مِّنَ ٱلثَّمَرَٰتِ لَعَلَّهُمۡ يَشۡكُرُونَ
«Ewe Mola wetu! Mimi nimewafanya watoto wangu wakae kwenye bonde lisilo na mimea wala maji, penye ujirani na mji wako mtakatifu. Mola wetu! Mimi nimefanya hilo kwa amri Yako, ili wasimamishe Swala kwa namna yake itakikanayo, basi ifanye myoyo ya baadhi ya viumbe vyako ilemee kwao na ipendelee, na uwape riziki ya kila aina ya matunda wakiwa mahali hapa, ili wakushukuru kwa neema zako.» Mwenyezi Mungu Akakubali maombe yake.
Arabic explanations of the Qur’an:
رَبَّنَآ إِنَّكَ تَعۡلَمُ مَا نُخۡفِي وَمَا نُعۡلِنُۗ وَمَا يَخۡفَىٰ عَلَى ٱللَّهِ مِن شَيۡءٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا فِي ٱلسَّمَآءِ
«Ewe Mola wetu! Hakika wewe unajua kila tunachokificha na tunachokionyesha. Na hakuna chochote chenye kupotea na kuwa nje ya ujuzi wa Mwenyezi Mungu miongoni mwa vilivyoko ardhini na mbinguini.»
Arabic explanations of the Qur’an:
ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ ٱلَّذِي وَهَبَ لِي عَلَى ٱلۡكِبَرِ إِسۡمَٰعِيلَ وَإِسۡحَٰقَۚ إِنَّ رَبِّي لَسَمِيعُ ٱلدُّعَآءِ
Ibrāhīm anamsifu Mola wake na anasema, «Shukrani zote ni za Mwenyezi Mungu Aliyeniruzuku, pamoja na uzee wangu, wanangu wawili, Ismā'īl na Isḥāq, baada ya maombi yangu Anitunuku miongoni mwa wema, kwani Mola wangu ni mwenye kusikia maombi ya mwenye kumuomba; na mimemuomba na Hakuyapitisha patupu matarajio yangu.
Arabic explanations of the Qur’an:
رَبِّ ٱجۡعَلۡنِي مُقِيمَ ٱلصَّلَوٰةِ وَمِن ذُرِّيَّتِيۚ رَبَّنَا وَتَقَبَّلۡ دُعَآءِ
«Ewe Mola wangi! Nijaalie ni mwenye kuendelea kutekeleza Swala kwa njia ya ukamilifu zaidi na ujaalie katika kizazi changu wenye kuendelea nayo. Ewe Mola wetu! Na uyakubali maombi yangu na uikubali ibada yangu.
Arabic explanations of the Qur’an:
رَبَّنَا ٱغۡفِرۡ لِي وَلِوَٰلِدَيَّ وَلِلۡمُؤۡمِنِينَ يَوۡمَ يَقُومُ ٱلۡحِسَابُ
«Ewe Mola wetu! Nisamehe iwapo yametukia kutoka kwangu mambo ambayo binadamu hawasalimiki nayo, na uwasamehe wazazi wangu wawili (Hapa ni kambla haijamfunukia kwamba baba yake ni adui wa Mwenyezi Mungu) na uwasamehe Waumini wote Siku ambayo watu watasimama kuhesabiwa na kulipwa..»
Arabic explanations of the Qur’an:
وَلَا تَحۡسَبَنَّ ٱللَّهَ غَٰفِلًا عَمَّا يَعۡمَلُ ٱلظَّٰلِمُونَۚ إِنَّمَا يُؤَخِّرُهُمۡ لِيَوۡمٖ تَشۡخَصُ فِيهِ ٱلۡأَبۡصَٰرُ
Na usidhani, ewe Mtume, kwamba Mwenezi Mungu ni mwenye kughafilika na yale wanayoyafanya madhalimu, ya kukukanusha wewe na Mitume wengine na kuwakera Waumini na maasia mengineyo. Kwa kweli, Anachelewsha kuwatesa mpaka Siku ngumu ambayo macho yao yatakodoka na hayatafumbika kwa kitisho cha yale yanayoyaona. Katika hii pana kumliwaza Mtume Muhammad, rehema na amani zimshukiye.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Ibrāhīm
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis - Translations’ Index

Translated by Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr & Sh. Naser Khamis

close