Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis * - Translations’ Index


Translation of the meanings Surah: Āl-‘Imrān   Ayah:
وَلَئِن مُّتُّمۡ أَوۡ قُتِلۡتُمۡ لَإِلَى ٱللَّهِ تُحۡشَرُونَ
Na iwapo ajali zenu zitakoma katika haya maisha ya dunia na mkafa juu ya matandiko yenu au mkauawa katika uwanja wa mapigano, ni kwa Mwenyezi Mungu, Peke Yake, Mtakusanywa; na huko Atawalipa kwa matendo yenu mliyoyatenda.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَبِمَا رَحۡمَةٖ مِّنَ ٱللَّهِ لِنتَ لَهُمۡۖ وَلَوۡ كُنتَ فَظًّا غَلِيظَ ٱلۡقَلۡبِ لَٱنفَضُّواْ مِنۡ حَوۡلِكَۖ فَٱعۡفُ عَنۡهُمۡ وَٱسۡتَغۡفِرۡ لَهُمۡ وَشَاوِرۡهُمۡ فِي ٱلۡأَمۡرِۖ فَإِذَا عَزَمۡتَ فَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلۡمُتَوَكِّلِينَ
Na kwa ajili ya rehema za Mwenyezi Mungu kwako na maswhaba wako, ewe Nabii, Mwenyezi Mungu Alikuneemesha ukawa laini kwao. Na lau ungalikuwa na tabia mbaya, mwenye moyo mgumu, maswahaba wako wangalijitenga na kuwa mbali na wewe. Kwa hivyo, usiwe na hasira nao kwa yaliyotokea kwao katika vita vya Uhud. Basi muombe Mwenyezi Mungu, ewe Nabii, Awasamehe na uwashauri katika mambo yanayohitajia ushauri. Na utakapoazimia kufanya jambo kati ya mambo yoyote, baada ya kushauri, litekeleze hali ya kumtegemea Mwenyezi Mungu, Peke Yake. Hakika Mwenyezi Mungu Anawapenda wenye kujitegemeza Kwake.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِن يَنصُرۡكُمُ ٱللَّهُ فَلَا غَالِبَ لَكُمۡۖ وَإِن يَخۡذُلۡكُمۡ فَمَن ذَا ٱلَّذِي يَنصُرُكُم مِّنۢ بَعۡدِهِۦۗ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ
Iwapo Mwenyezi Mungu Atawapa msaada na nusura Yake, hapana yoyota awezaye kuwashinda. Na iwapo Atawaacha kuwasaidia na kuwanusuru, basi ni nani awezaye kuwanusuru nyinyi baada ya Yeye kuacha kuwanusuru? Na kwa Mwenyezi Mungu, Peke Yake, nawajitegemeze Waumini.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَمَا كَانَ لِنَبِيٍّ أَن يَغُلَّۚ وَمَن يَغۡلُلۡ يَأۡتِ بِمَا غَلَّ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ ثُمَّ تُوَفَّىٰ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا كَسَبَتۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ
Haiwi kwa Mtume kuwafanyia hiana maswahaba wake kwa kutwaa kitu katika ngawira ambayo Mwenyezi Mungu Hakumtengea. Na yoyote mwenye kulifanya hilo, miongoni mwenu, atakuja Siku ya Kiyama akiwa amekibeba kile alichokitwaa, ili afedheheshwe nacho mbele ya kila mtu katika kisimamo kinachojumuisha watu wote. Kisha itapewa kila nafsi malipo kamili ya ilichokichuma pasi na kupunguzwa wala kufanyiwa dhuluma.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَفَمَنِ ٱتَّبَعَ رِضۡوَٰنَ ٱللَّهِ كَمَنۢ بَآءَ بِسَخَطٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَمَأۡوَىٰهُ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ
Yule ambaye lengo lake ni radhi za Mwenyezi Mungu, halingani na yule ambaye ametopea kwenye maasia na kumkasirisha Mola wake na akastahiki kwa hilo makazi ya Jahanamu ambayo mwisho mbaya wa mtu kuishilia ni hapo.
Arabic explanations of the Qur’an:
هُمۡ دَرَجَٰتٌ عِندَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ
Watu wa Peponi wenye kufuata yenye kumridhisha Mwenyezi Mungu wanatafautiana daraja. Na watu wa Motoni wanaofuata yenye kumkasirisha Mwenyezi Mungu wanatafautiana katika matobwe. Wao hawalingani. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuziona amali zao, hakifichiki chochote Kwake katika matendo yao.
Arabic explanations of the Qur’an:
لَقَدۡ مَنَّ ٱللَّهُ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ إِذۡ بَعَثَ فِيهِمۡ رَسُولٗا مِّنۡ أَنفُسِهِمۡ يَتۡلُواْ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتِهِۦ وَيُزَكِّيهِمۡ وَيُعَلِّمُهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَإِن كَانُواْ مِن قَبۡلُ لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ
Hakika Mwenyezi Mungu Amewapa neema Waumini, miongoni mwa Waarabu, Alipomtumiliza Mtume atokaye katika jinsi yao, akawa anawasomea wao aya za Qur’ani, anawatakasa na ushirikina na tabia mbaya na anawafundisha Qur’ani na Suna, pamoja na kwamba kabla ya Mtume huyu walikuwa kwenye upotevu na ujinga ulio wazi.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَوَلَمَّآ أَصَٰبَتۡكُم مُّصِيبَةٞ قَدۡ أَصَبۡتُم مِّثۡلَيۡهَا قُلۡتُمۡ أَنَّىٰ هَٰذَاۖ قُلۡ هُوَ مِنۡ عِندِ أَنفُسِكُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Kwa nini mlipopatwa na msiba uliowakumba siku ya Uhud, ingawa mumewapata washirikina mara mbili yake siku ya Badr, mlisema kwa kustaajabu, «Mambo haya yatakuwa vipi, na sisi ni Waislamu, Mtume wa Mwenyezi Mungu yuko na sisi, na hawa ni washirikina?» Sema uwaambie, ewe Nabii, «Haya yaliyowapata yamesababishwa na nyinyi wenyewe kwa kuenda kinyume kwenu na amri ya Mtume wenu na kuelekea kwenu kukusanya ngawira.» Kwa hakika, Mwenyezi Mungu Anafanya Atakalo na Anahukumu Atakavyo. Hakuna mwenye kuitangua hukumu Yake.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Āl-‘Imrān
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis - Translations’ Index

Translated by Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr & Sh. Naser Khamis

close