Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis * - Translations’ Index


Translation of the meanings Surah: Al-Mulk   Ayah:
فَلَمَّا رَأَوۡهُ زُلۡفَةٗ سِيٓـَٔتۡ وُجُوهُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَقِيلَ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تَدَّعُونَ
Watakapoiona makafiri adhabu ya Mwenyezi Mungu ikiwa iko karibu nao na wakaishuhudia, utajitokeza unyonge na unguliko kwenye nyuso zao na waambiwe, kwa njia ya kuwalaumu na kuwakaripia, «Hii ndiyo ile mliokuwa mkitaka iharakishwe ulimwenguni.»
Arabic explanations of the Qur’an:
قُلۡ أَرَءَيۡتُمۡ إِنۡ أَهۡلَكَنِيَ ٱللَّهُ وَمَن مَّعِيَ أَوۡ رَحِمَنَا فَمَن يُجِيرُ ٱلۡكَٰفِرِينَ مِنۡ عَذَابٍ أَلِيمٖ
Sema, ewe Mtume, uwaambie hawa makafiri, «Nipasheni habari, iwapo Mwenyezi Mungu Atanifisha pamoja na Waumini walio pamoja na mimi, kama mnavyotamani, au Ataturehemu avicheleweshe vipindi vyetu vya kufa na Atuepushie adhabu yake, basi ni nani huyo ambaye atawahami aizuie adhabu kali yenye kuumiza isiwafikie?»
Arabic explanations of the Qur’an:
قُلۡ هُوَ ٱلرَّحۡمَٰنُ ءَامَنَّا بِهِۦ وَعَلَيۡهِ تَوَكَّلۡنَاۖ فَسَتَعۡلَمُونَ مَنۡ هُوَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ
Sema, «Ni Mwenyezi Mungu! Yeye Ndiye Mwingi wa rehema. Tumemuamini na tumeifuata Sheria Yake kivitendo na tumemtii. Na Kwake yeye, Peke Yake, tumetegemea katika mambo yetu yote. Basi mtajua, enyi makafiri, itakapoteremka adhabu, ni yupi kati ya makundi mawili miongoni mwetu: sisi na nyinyi, yuko mbali waziwazi na njia ya Mwenyezi Mungu iliyonyoka.»
Arabic explanations of the Qur’an:
قُلۡ أَرَءَيۡتُمۡ إِنۡ أَصۡبَحَ مَآؤُكُمۡ غَوۡرٗا فَمَن يَأۡتِيكُم بِمَآءٖ مَّعِينِۭ
Sema, ewe Mtume, Uwaambie hawa washirikina, «Nipasheni habari iwapo maji yenu mnayokunywa ni yenye kupotea ndani ya ardhi, mkawa hmyafikii kwa namna yoyote, basi ni nani asiyekuwa Mwenyezi Mungu Atakayewaletea maji yenye kutembea ardhini na yenye kuonekana na macho»
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Al-Mulk
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis - Translations’ Index

Translated by Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr & Sh. Naser Khamis

close