Check out the new design

Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis * - Përmbajtja e përkthimeve


Përkthimi i kuptimeve Surja: El Mulk   Ajeti:
فَلَمَّا رَأَوۡهُ زُلۡفَةٗ سِيٓـَٔتۡ وُجُوهُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَقِيلَ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تَدَّعُونَ
Watakapoiona makafiri adhabu ya Mwenyezi Mungu ikiwa iko karibu nao na wakaishuhudia, utajitokeza unyonge na unguliko kwenye nyuso zao na waambiwe, kwa njia ya kuwalaumu na kuwakaripia, «Hii ndiyo ile mliokuwa mkitaka iharakishwe ulimwenguni.»
Tefsiret në gjuhën arabe:
قُلۡ أَرَءَيۡتُمۡ إِنۡ أَهۡلَكَنِيَ ٱللَّهُ وَمَن مَّعِيَ أَوۡ رَحِمَنَا فَمَن يُجِيرُ ٱلۡكَٰفِرِينَ مِنۡ عَذَابٍ أَلِيمٖ
Sema, ewe Mtume, uwaambie hawa makafiri, «Nipasheni habari, iwapo Mwenyezi Mungu Atanifisha pamoja na Waumini walio pamoja na mimi, kama mnavyotamani, au Ataturehemu avicheleweshe vipindi vyetu vya kufa na Atuepushie adhabu yake, basi ni nani huyo ambaye atawahami aizuie adhabu kali yenye kuumiza isiwafikie?»
Tefsiret në gjuhën arabe:
قُلۡ هُوَ ٱلرَّحۡمَٰنُ ءَامَنَّا بِهِۦ وَعَلَيۡهِ تَوَكَّلۡنَاۖ فَسَتَعۡلَمُونَ مَنۡ هُوَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ
Sema, «Ni Mwenyezi Mungu! Yeye Ndiye Mwingi wa rehema. Tumemuamini na tumeifuata Sheria Yake kivitendo na tumemtii. Na Kwake yeye, Peke Yake, tumetegemea katika mambo yetu yote. Basi mtajua, enyi makafiri, itakapoteremka adhabu, ni yupi kati ya makundi mawili miongoni mwetu: sisi na nyinyi, yuko mbali waziwazi na njia ya Mwenyezi Mungu iliyonyoka.»
Tefsiret në gjuhën arabe:
قُلۡ أَرَءَيۡتُمۡ إِنۡ أَصۡبَحَ مَآؤُكُمۡ غَوۡرٗا فَمَن يَأۡتِيكُم بِمَآءٖ مَّعِينِۭ
Sema, ewe Mtume, Uwaambie hawa washirikina, «Nipasheni habari iwapo maji yenu mnayokunywa ni yenye kupotea ndani ya ardhi, mkawa hmyafikii kwa namna yoyote, basi ni nani asiyekuwa Mwenyezi Mungu Atakayewaletea maji yenye kutembea ardhini na yenye kuonekana na macho»
Tefsiret në gjuhën arabe:
 
Përkthimi i kuptimeve Surja: El Mulk
Përmbajtja e sureve Numri i faqes
 
Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis - Përmbajtja e përkthimeve

Përkthyer nga Dr. Abdullah Muhammed Abu Bekr dhe Shejh Nasir Khamis.

Mbyll