Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany * - Translations’ Index

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Translation of the meanings Surah: Al-Qiyāmah   Ayah:

Surat Al-Qiyamah

لَآ أُقۡسِمُ بِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
Ninaapa na natilia mkazo kiapo hichi kwa Siku ya Kiyama, na hiyo ni kweli iliyo thibiti;
Arabic explanations of the Qur’an:
وَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلنَّفۡسِ ٱللَّوَّامَةِ
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
Na ninaapa na natilia mkazo kiapo hichi kwa nafsi inayo mlaumu mtu kwa dhambi zake na upungufu wake, ya kwamba bila ya shaka yoyote mtafufuliwa baada ya kukusanywa mafupa yenu yaliyo tawanyika.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجۡمَعَ عِظَامَهُۥ
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
Hivyo mtu anadhani baada ya kuwa Sisi tulimuumba naye hakuwa kitu chochote, tutakuja shindwa kuyakusanya mafupa yake yaliyooza na yakatapanyika?
Arabic explanations of the Qur’an:
بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُۥ
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
Hasha! Sisi tuna uweza wa kuviweka sawa hata vifupa vya vidole vyake vilivyo vurugika, wachilia mbali mafupa yake makubwa makubwa ya mwili wake.
Arabic explanations of the Qur’an:
بَلۡ يُرِيدُ ٱلۡإِنسَٰنُ لِيَفۡجُرَ أَمَامَهُۥ
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
Hivyo mtu anakanya kufufuliwa? Anataka abakie katika uasi wake katika siku zote zilizo mbakilia katika umri wake ulio salia?
Arabic explanations of the Qur’an:
يَسۡـَٔلُ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
Anauliza kwa kuona haiwezi kutokea saa ya Kiyama: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
Arabic explanations of the Qur’an:
فَإِذَا بَرِقَ ٱلۡبَصَرُ
Basi jicho litapo dawaa!
Jicho litapo tahayari kwa kufazaika na kushtuka,
Arabic explanations of the Qur’an:
وَخَسَفَ ٱلۡقَمَرُ
Na mwezi utapo patwa!
Na mwangaza wa mwezi ukapotea,
Arabic explanations of the Qur’an:
وَجُمِعَ ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ
Na likakusanywa jua na mwezi!
Na jua likakusanyika na mwezi kuchomoza magharibi,
Arabic explanations of the Qur’an:
يَقُولُ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذٍ أَيۡنَ ٱلۡمَفَرُّ
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
Mtu hapo atasema: Yako wapi makimbilio kuikimbia hii adhabu?
Arabic explanations of the Qur’an:
كَلَّا لَا وَزَرَ
La! Hapana pa kukimbilia!
Huachi, ewe mtu, kutafuta makimbilio? Leo huna pa kukimbilia wewe,
Arabic explanations of the Qur’an:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمُسۡتَقَرُّ
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
ila kwa Mola wako Mlezi peke yake, ndipo penye matulivu ya waja, Peponi au Motoni.
Arabic explanations of the Qur’an:
يُنَبَّؤُاْ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذِۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
Siku hiyo mtu ataambiwa vitendo vyake alivyo vitanguliza na alivyo viakhirisha.
Arabic explanations of the Qur’an:
بَلِ ٱلۡإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٞ
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
Bali mtu yeye mwenyewe ni hoja iliyo wazi juu ya nafsi yake inayo mkazania kwa anayo yatenda na anayo yaacha.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
Na ijapo kuwa atajitolea chungu nzima ya udhuru na akazieneza, hawezi kabisa kuepukana na hoja hizo.
Arabic explanations of the Qur’an:
لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
Usiuharikishe ulimi wako kwa kuisoma Qur'ani na kujaribu kuihifadhi kwa haraka pale unapo teremshiwa kwa Wahyi.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
Hakika ni juu yetu Sisi kuikusanya hiyo katika kifua chako, na kuithibitisha katika ulimi wako.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
Akikusomea Mjumbe wetu (Jibril) basi nawe ifuatilize kama unavyo isikia.
Arabic explanations of the Qur’an:
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
Kisha baada ya hayo ni juu yetu kuibainisha ikiingia tatizo lolote juu yako.
Arabic explanations of the Qur’an:
كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
Wacheni kukanya kufufuliwa, na hilo ni jambo la kweli. Lakini nyinyi mnaipenda dunia na starehe zake,
Arabic explanations of the Qur’an:
وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Na mnaacha maisha ya Akhera.
Na mnaiacha Akhera na neema zake.
Arabic explanations of the Qur’an:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
Siku hiyo zitakuwapo nyuso nzuri, zenye kumwangalia Mola wao Mlezi bila ya kusema kwa sifa gani, wajihi gani, au masafa gani.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
Siku hiyo zitakuwapo nyuso nzuri, zenye kumwangalia Mola wao Mlezi bila ya kusema kwa sifa gani, wajihi gani, au masafa gani.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
Na nyuso nyengine zitakuwapo zimenuna, zimekunjana mno, zinangojea zitendewe jambo ambalo kwa kitisho chake linavunja uti wa mgongo.
Arabic explanations of the Qur’an:
تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
Zinangojea zitendewe jambo ambalo kwa kitisho chake linavunja uti wa mgongo.
Arabic explanations of the Qur’an:
كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
Mna nini na kuipenda dunia ambayo mnaifariki roho inapo fika katika mafupa ya kooni,
Arabic explanations of the Qur’an:
وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
Na walio hudhuria wakasema: Yupo wa kumganga huyu kwa haya aliyo nayo?
Arabic explanations of the Qur’an:
وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
Akayakinisha yule yaliyo mfika mauti kama lililo mshukia ni kuiacha dunia inayo pendwa, na imekwisha mfika shida yake kikomo cha mwisho.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
Na muundi wa mguu umekwisha ambatana na wa pili wakati wa kutoka roho.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
Kwa Mola wako Mlezi tu siku hiyo ndio machungio ya waja, ama Peponi au Motoni.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
Kwa sababu hakusadiki, wala hakuswali.
Binaadamu amekanya kufufuliwa, na kwa hivyo hakumsadiki Mtume wala Qur'ani. Wala hakumtimizia Mwenyezi Mungu faridha za Swala.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Bali alikanusha, na akageuka.
Lakini aliikadhibisha Qur'ani, akaipuuza Imani,
Arabic explanations of the Qur’an:
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
Na akatoka kwenda kwa watu wake wa nyumbani kwa maringo na kujitapa.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ
Ole wako, ole wako!
Ewe unaye kadhibisha, utaangamia!
Arabic explanations of the Qur’an:
ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ
Kisha Ole wako, ole wako!
Tena utaangamia! Na tena utaangamia, na utaangamia!
Arabic explanations of the Qur’an:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
Hivyo anadhani huyu mtu anaye kanya kufufuliwa kuwa ataachwa hivi hivi akiringa tu katika maisha yake, na akisha kufa iwe basi, wala asifufuliwe akahisabiwa kwa vitendo vyake?
Arabic explanations of the Qur’an:
أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
Kwani yeye mtu hakuwa ni tone tu ya manii, ilio jaaliwa kuwemo katika tumbo la uzazi?
Arabic explanations of the Qur’an:
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
Kisha hiyo tone ikawa kipande cha damu iliyo ganda, na Mwenyezi Mungu akaiumba, akaisawazisha mpaka ikawa na umbo zuri?
Arabic explanations of the Qur’an:
فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
Akajaalia namna mbili, mwanamume na mwanamke?
Arabic explanations of the Qur’an:
أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
Je! Huyo Muumba wa mwanzo aliye fanya yote haya, basi si muweza wa kuwahuisha maiti baada ya kuyakusanya mafupa yao?
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Al-Qiyāmah
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Ali Muhsen Alberwany

close