Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani * - Daftar isi terjemahan

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Terjemahan makna Surah: Surah Al-Qiyāmah   Ayah:

Surat Al-Qiyamah

لَآ أُقۡسِمُ بِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
Ninaapa na natilia mkazo kiapo hichi kwa Siku ya Kiyama, na hiyo ni kweli iliyo thibiti;
Tafsir berbahasa Arab:
وَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلنَّفۡسِ ٱللَّوَّامَةِ
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
Na ninaapa na natilia mkazo kiapo hichi kwa nafsi inayo mlaumu mtu kwa dhambi zake na upungufu wake, ya kwamba bila ya shaka yoyote mtafufuliwa baada ya kukusanywa mafupa yenu yaliyo tawanyika.
Tafsir berbahasa Arab:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجۡمَعَ عِظَامَهُۥ
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
Hivyo mtu anadhani baada ya kuwa Sisi tulimuumba naye hakuwa kitu chochote, tutakuja shindwa kuyakusanya mafupa yake yaliyooza na yakatapanyika?
Tafsir berbahasa Arab:
بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُۥ
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
Hasha! Sisi tuna uweza wa kuviweka sawa hata vifupa vya vidole vyake vilivyo vurugika, wachilia mbali mafupa yake makubwa makubwa ya mwili wake.
Tafsir berbahasa Arab:
بَلۡ يُرِيدُ ٱلۡإِنسَٰنُ لِيَفۡجُرَ أَمَامَهُۥ
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
Hivyo mtu anakanya kufufuliwa? Anataka abakie katika uasi wake katika siku zote zilizo mbakilia katika umri wake ulio salia?
Tafsir berbahasa Arab:
يَسۡـَٔلُ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
Anauliza kwa kuona haiwezi kutokea saa ya Kiyama: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
Tafsir berbahasa Arab:
فَإِذَا بَرِقَ ٱلۡبَصَرُ
Basi jicho litapo dawaa!
Jicho litapo tahayari kwa kufazaika na kushtuka,
Tafsir berbahasa Arab:
وَخَسَفَ ٱلۡقَمَرُ
Na mwezi utapo patwa!
Na mwangaza wa mwezi ukapotea,
Tafsir berbahasa Arab:
وَجُمِعَ ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ
Na likakusanywa jua na mwezi!
Na jua likakusanyika na mwezi kuchomoza magharibi,
Tafsir berbahasa Arab:
يَقُولُ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذٍ أَيۡنَ ٱلۡمَفَرُّ
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
Mtu hapo atasema: Yako wapi makimbilio kuikimbia hii adhabu?
Tafsir berbahasa Arab:
كَلَّا لَا وَزَرَ
La! Hapana pa kukimbilia!
Huachi, ewe mtu, kutafuta makimbilio? Leo huna pa kukimbilia wewe,
Tafsir berbahasa Arab:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمُسۡتَقَرُّ
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
ila kwa Mola wako Mlezi peke yake, ndipo penye matulivu ya waja, Peponi au Motoni.
Tafsir berbahasa Arab:
يُنَبَّؤُاْ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذِۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
Siku hiyo mtu ataambiwa vitendo vyake alivyo vitanguliza na alivyo viakhirisha.
Tafsir berbahasa Arab:
بَلِ ٱلۡإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٞ
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
Bali mtu yeye mwenyewe ni hoja iliyo wazi juu ya nafsi yake inayo mkazania kwa anayo yatenda na anayo yaacha.
Tafsir berbahasa Arab:
وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
Na ijapo kuwa atajitolea chungu nzima ya udhuru na akazieneza, hawezi kabisa kuepukana na hoja hizo.
Tafsir berbahasa Arab:
لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
Usiuharikishe ulimi wako kwa kuisoma Qur'ani na kujaribu kuihifadhi kwa haraka pale unapo teremshiwa kwa Wahyi.
Tafsir berbahasa Arab:
إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
Hakika ni juu yetu Sisi kuikusanya hiyo katika kifua chako, na kuithibitisha katika ulimi wako.
Tafsir berbahasa Arab:
فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
Akikusomea Mjumbe wetu (Jibril) basi nawe ifuatilize kama unavyo isikia.
Tafsir berbahasa Arab:
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
Kisha baada ya hayo ni juu yetu kuibainisha ikiingia tatizo lolote juu yako.
Tafsir berbahasa Arab:
كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
Wacheni kukanya kufufuliwa, na hilo ni jambo la kweli. Lakini nyinyi mnaipenda dunia na starehe zake,
Tafsir berbahasa Arab:
وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Na mnaacha maisha ya Akhera.
Na mnaiacha Akhera na neema zake.
Tafsir berbahasa Arab:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
Siku hiyo zitakuwapo nyuso nzuri, zenye kumwangalia Mola wao Mlezi bila ya kusema kwa sifa gani, wajihi gani, au masafa gani.
Tafsir berbahasa Arab:
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
Siku hiyo zitakuwapo nyuso nzuri, zenye kumwangalia Mola wao Mlezi bila ya kusema kwa sifa gani, wajihi gani, au masafa gani.
Tafsir berbahasa Arab:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
Na nyuso nyengine zitakuwapo zimenuna, zimekunjana mno, zinangojea zitendewe jambo ambalo kwa kitisho chake linavunja uti wa mgongo.
Tafsir berbahasa Arab:
تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
Zinangojea zitendewe jambo ambalo kwa kitisho chake linavunja uti wa mgongo.
Tafsir berbahasa Arab:
كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
Mna nini na kuipenda dunia ambayo mnaifariki roho inapo fika katika mafupa ya kooni,
Tafsir berbahasa Arab:
وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
Na walio hudhuria wakasema: Yupo wa kumganga huyu kwa haya aliyo nayo?
Tafsir berbahasa Arab:
وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
Akayakinisha yule yaliyo mfika mauti kama lililo mshukia ni kuiacha dunia inayo pendwa, na imekwisha mfika shida yake kikomo cha mwisho.
Tafsir berbahasa Arab:
وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
Na muundi wa mguu umekwisha ambatana na wa pili wakati wa kutoka roho.
Tafsir berbahasa Arab:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
Kwa Mola wako Mlezi tu siku hiyo ndio machungio ya waja, ama Peponi au Motoni.
Tafsir berbahasa Arab:
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
Kwa sababu hakusadiki, wala hakuswali.
Binaadamu amekanya kufufuliwa, na kwa hivyo hakumsadiki Mtume wala Qur'ani. Wala hakumtimizia Mwenyezi Mungu faridha za Swala.
Tafsir berbahasa Arab:
وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Bali alikanusha, na akageuka.
Lakini aliikadhibisha Qur'ani, akaipuuza Imani,
Tafsir berbahasa Arab:
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
Na akatoka kwenda kwa watu wake wa nyumbani kwa maringo na kujitapa.
Tafsir berbahasa Arab:
أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ
Ole wako, ole wako!
Ewe unaye kadhibisha, utaangamia!
Tafsir berbahasa Arab:
ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ
Kisha Ole wako, ole wako!
Tena utaangamia! Na tena utaangamia, na utaangamia!
Tafsir berbahasa Arab:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
Hivyo anadhani huyu mtu anaye kanya kufufuliwa kuwa ataachwa hivi hivi akiringa tu katika maisha yake, na akisha kufa iwe basi, wala asifufuliwe akahisabiwa kwa vitendo vyake?
Tafsir berbahasa Arab:
أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
Kwani yeye mtu hakuwa ni tone tu ya manii, ilio jaaliwa kuwemo katika tumbo la uzazi?
Tafsir berbahasa Arab:
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
Kisha hiyo tone ikawa kipande cha damu iliyo ganda, na Mwenyezi Mungu akaiumba, akaisawazisha mpaka ikawa na umbo zuri?
Tafsir berbahasa Arab:
فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
Akajaalia namna mbili, mwanamume na mwanamke?
Tafsir berbahasa Arab:
أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
Je! Huyo Muumba wa mwanzo aliye fanya yote haya, basi si muweza wa kuwahuisha maiti baada ya kuyakusanya mafupa yao?
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Surah: Surah Al-Qiyāmah
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani - Daftar isi terjemahan

Terjemahan Makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke Bahasa Sawahili oleh Ali Muhsin Al-Barwani

Tutup