Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany * - Índice de traducciones

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traducción de significados Versículo: (38) Capítulo: Sura Ar-Ra'd
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا رُسُلٗا مِّن قَبۡلِكَ وَجَعَلۡنَا لَهُمۡ أَزۡوَٰجٗا وَذُرِّيَّةٗۚ وَمَا كَانَ لِرَسُولٍ أَن يَأۡتِيَ بِـَٔايَةٍ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۗ لِكُلِّ أَجَلٖ كِتَابٞ
Na hakika Sisi tulikwisha watuma Mitume kabla yako, na tukajaalia wawe na wake na dhuriya. Na haiwi kwa Mtume kuleta miujiza isipo kuwa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Kila kipindi kina hukumu yake.
Na ikiwa washirikina wanachochea watu wastaajabu kuwa wewe una wake na dhuriya, yaani wazao, na wanataka ulete muujiza mwengine usio kuwa Qur'ani, basi tulileta kabla yako Mitume wenye wake na wana vile vile. Kwani Mtume ni mwanaadamu, na ana sifa za kibinaadamu. Lakini yeye ni mbora kuliko wote. Wala Nabii hawezi kuleta muujiza kama apendavyo yeye au wapendavyo watu wake! Bali aletaye muujiza ni Mwenyezi Mungu, na Yeye ndiye anaye toa idhini. Kila kizazi katika vizazi kina amri yao aliyo waandikia Mwenyezi Mungu ya kuwasilihi. Na kila kizazi kina muujiza wake unao wanasibu. (Nabii Isa a.s. anasimuliwa katika Injili ya Yohana 5.30 kuwa alisema: Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe.)
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Versículo: (38) Capítulo: Sura Ar-Ra'd
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por Ali Muhsen Alberwany

Cerrar