د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - علی محسن البرواني * - د ژباړو فهرست (لړلیک)

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

د معناګانو ژباړه آیت: (38) سورت: الرعد
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا رُسُلٗا مِّن قَبۡلِكَ وَجَعَلۡنَا لَهُمۡ أَزۡوَٰجٗا وَذُرِّيَّةٗۚ وَمَا كَانَ لِرَسُولٍ أَن يَأۡتِيَ بِـَٔايَةٍ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۗ لِكُلِّ أَجَلٖ كِتَابٞ
Na hakika Sisi tulikwisha watuma Mitume kabla yako, na tukajaalia wawe na wake na dhuriya. Na haiwi kwa Mtume kuleta miujiza isipo kuwa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Kila kipindi kina hukumu yake.
Na ikiwa washirikina wanachochea watu wastaajabu kuwa wewe una wake na dhuriya, yaani wazao, na wanataka ulete muujiza mwengine usio kuwa Qur'ani, basi tulileta kabla yako Mitume wenye wake na wana vile vile. Kwani Mtume ni mwanaadamu, na ana sifa za kibinaadamu. Lakini yeye ni mbora kuliko wote. Wala Nabii hawezi kuleta muujiza kama apendavyo yeye au wapendavyo watu wake! Bali aletaye muujiza ni Mwenyezi Mungu, na Yeye ndiye anaye toa idhini. Kila kizazi katika vizazi kina amri yao aliyo waandikia Mwenyezi Mungu ya kuwasilihi. Na kila kizazi kina muujiza wake unao wanasibu. (Nabii Isa a.s. anasimuliwa katika Injili ya Yohana 5.30 kuwa alisema: Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe.)
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه آیت: (38) سورت: الرعد
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - علی محسن البرواني - د ژباړو فهرست (لړلیک)

سواحلې ژبې ته د قرآن کریم د معناګانو ژباړه، علی محسن البرواني ژباړلې ده

بندول