ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی * - لیست ترجمه ها

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

ترجمهٔ معانی آیه: (35) سوره: سوره يونس
قُلۡ هَلۡ مِن شُرَكَآئِكُم مَّن يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلۡحَقِّۚ قُلِ ٱللَّهُ يَهۡدِي لِلۡحَقِّۗ أَفَمَن يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلۡحَقِّ أَحَقُّ أَن يُتَّبَعَ أَمَّن لَّا يَهِدِّيٓ إِلَّآ أَن يُهۡدَىٰۖ فَمَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Sema: Je! Yupo katika miungu yenu ya ushirikina anaye ongoa kwendea Haki? Sema: Mwenyezi Mungu anaongoa kwendea Haki. Basi, je, anaye stahiki kufuatwa ni yule Mwenye kuongoa kwendea Haki au asiye ongoa ila aongozwe yeye? Basi nyinyi mna nini? Mnahukumu namna gani?
Ewe Mtume! Waambie hao washirikina: Yupo yeyote katika hao mlio wafanya washirika wa Mwenyezi Mungu mkawaabudu, awezaye kupambanua baina ya uwongofu na upotovu, akawaongoza watu kwenye Njia ya Haki? Wataemewa! Basi, je! Yupi bora kufuatwa - Mwenye kuweza kuongoa kwendea Haki au asiye weza hata kujiongoa nafsi yake? Naye huyo hawezi kumwongoa mtu, ila yeye anahitaji mtu wa kumwongoa. Hao ndio kama wakuu wa makafiri, mapadri na mamonaki ambao ndio mmewafanya ni waola mkamuacha Mwenyezi Mungu!! Nini basi kilicho kupelekeeni kukengeuka hata mkawashirikisha hawa na Mwenyezi Mungu? Na nini hali ya ajabu iliyo kusukumeni kwenye hizo hukumu na sharia za kigeni?
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی آیه: (35) سوره: سوره يونس
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی ـ ترجمهٔ علی محسن البروانی.

بستن