Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Ali Muchsen Al-Beruany * - Vertimų turinys

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (35) Sūra: Sūra Jūnus
قُلۡ هَلۡ مِن شُرَكَآئِكُم مَّن يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلۡحَقِّۚ قُلِ ٱللَّهُ يَهۡدِي لِلۡحَقِّۗ أَفَمَن يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلۡحَقِّ أَحَقُّ أَن يُتَّبَعَ أَمَّن لَّا يَهِدِّيٓ إِلَّآ أَن يُهۡدَىٰۖ فَمَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Sema: Je! Yupo katika miungu yenu ya ushirikina anaye ongoa kwendea Haki? Sema: Mwenyezi Mungu anaongoa kwendea Haki. Basi, je, anaye stahiki kufuatwa ni yule Mwenye kuongoa kwendea Haki au asiye ongoa ila aongozwe yeye? Basi nyinyi mna nini? Mnahukumu namna gani?
Ewe Mtume! Waambie hao washirikina: Yupo yeyote katika hao mlio wafanya washirika wa Mwenyezi Mungu mkawaabudu, awezaye kupambanua baina ya uwongofu na upotovu, akawaongoza watu kwenye Njia ya Haki? Wataemewa! Basi, je! Yupi bora kufuatwa - Mwenye kuweza kuongoa kwendea Haki au asiye weza hata kujiongoa nafsi yake? Naye huyo hawezi kumwongoa mtu, ila yeye anahitaji mtu wa kumwongoa. Hao ndio kama wakuu wa makafiri, mapadri na mamonaki ambao ndio mmewafanya ni waola mkamuacha Mwenyezi Mungu!! Nini basi kilicho kupelekeeni kukengeuka hata mkawashirikisha hawa na Mwenyezi Mungu? Na nini hali ya ajabu iliyo kusukumeni kwenye hizo hukumu na sharia za kigeni?
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (35) Sūra: Sūra Jūnus
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Ali Muchsen Al-Beruany - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Ali Muchsin Al-Birvany.

Uždaryti