Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Aaya: (74) Simoore: Simoore yuunus
ثُمَّ بَعَثۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِۦ رُسُلًا إِلَىٰ قَوۡمِهِمۡ فَجَآءُوهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ فَمَا كَانُواْ لِيُؤۡمِنُواْ بِمَا كَذَّبُواْ بِهِۦ مِن قَبۡلُۚ كَذَٰلِكَ نَطۡبَعُ عَلَىٰ قُلُوبِ ٱلۡمُعۡتَدِينَ
Kisha tukatuma, baada ya Nūḥ, Mitume kwenda kwa watu wao (Hūd, Ṣāliḥ„ Ibrāhīm, Lūṭ„ Shu'ayb na wengineo), kila Mtume Alikuja kwa watu wake kwa miujiza yenye kuonesha dalili ya utume Wake na ukweli wa yale aliyowaitia. Hawakuwa ni wenye kuyaamini wala kuyafanya yale ambayo watu wa Nūḥ na waliowatangulia miongoni mwa ummah waliopita. Na kama alivyopiga mhuri Mwenyezi Mungu juu ya nyoyo za hawa watu wasiamini, hivyo ndivyo anavyopiga mhuri juu ya nyoyo za wanaofanana na wao kati ya waliokuwa baada yao, miongoni mwa wale ambao walivuka mipaka ya Mwenyezi Mungu na wakaenda kinyume na yale, ambayo Mitume wao waliwaitia kwayo, ya kumtii Yeye, ikiwa ni mateso kwao kwa sababu ya matendo yao ya uasi.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Aaya: (74) Simoore: Simoore yuunus
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawaahili, firi ɗum ko Doktoor Abdullaay Muhammad Abuubakri. E mawɗo Naasir Kamiis.

Uddude